Lupatu: Kinga dhidi ya wachawi na uchawi

Lupatu: Kinga dhidi ya wachawi na uchawi

Kwa asie ijua Ruby, hii ndio Ruby.
Ukikutana na uzito huo, lazima ulale na kina Wema sepetu.
Zuchu mwenyewe hachomoki hapo. View attachment 1571029
Mkuu vp mpakani now wanaluhusiwa kupita, maana nilikua na jamaangu tulikua na latiba ya kuzamia huko machimboni,naomba unipe muongoze maana nasikia Islamic state wanaua raia ovyo
 
Boa tarde camaradas.

Tembea uyaone, zunguka ujifunze.

Hivyo ndivyo ninavyoanza kwa leo.

Mara nyingi nimekua msomaji tu humu ndani, ila leo kuna topic nimeisoma humu ndani iliyo nishawishi na mimi leo niandike.

Katika harakati zangu za kutafuta maisha nilijikuta naangukia Mocambique. Mocambique sikwenda kuajiriwa bali ni kuchimba madini (Ruby).

Nakumbuka huku nilikutana na Rafiki yangu anaeitwa Carlos. Mshikaji tulijuana kutokana na kufanya nae kazi (kuchimba) mara kwa mara.

Katika harakati zetu mara nyingi tulikuwa watu wa kuporora (hatupati madini)

Siku moja Carlos akanishauri twende kijijini kwao Shapa (wilaya ya Mueda, mkoa Cabo del Gado) kuna mzee ni mganga anaweza kutusaidia katika haraka zetu. Carlos yeye ni Mmakonde chale.

Baada ya kufika kijijini Shapa, Carlos akinichukua mpaka nyumbani kwa mganga (Mzee LUPATU)

Tulifika kwa mzee, tukamueleza shida yetu, na mzee akakubali kutupa dawa (ya madini). Siku ya tatu tukageuka kurudi mgodini (Nanhupo, wilaya ya Montepuez, mkoa Cabo del Gado)

Hatukumaliza wiki mbili, tukapata Gram moja na point saba (Ruby) tukaenda kulitikisa (kuuza) kwa Mtailendi.

Tukapata mgao kila mtu $17,500. US dollar. Kwa muda huo nilijikuta na Milioni thalathini sita na usheee hivi.

Baada ya mgao wetu, tukaamua kwenda kumpa shukrani yake mzee wetu (Mzee LUPATU) tena ukizingatia kutoka Mueda kwenda Namatili (boda) sio mbali, na ndio njia ambayo ninaitumia kuvuka kutoka Mocambique kuja Tanzania.

Tulifika kwa mzee LUPATU tukampa shukrani, na kila mtu akampa yule mzee 50,000 miticaish.

Baada ya shukrani, yule mzee akatuomba tulale pale kwake kisha kesho tuondoke, maana kuna kinga anataka kutupa.

Hakuna aliekataa, tulibaki pale kama alivyotaka babu yetu.

Kilipoingia kiza babu alikuja na ndoo iliyo jaa maji yenye dawa (niliona mizizi na majani ndani ya yale maji) akatuogesha kisha tukaingia kilingeni kwake. Akatoa vibao vidogo viwili, vye pembe nne, mfano wa kibiriti.

Vibao vile upande mmoja wa kibao kulikua kama kimechorwa msalaba kwa kuchongwa. Tukaamuliwa tuchanjwe damu, then damu ile ilipitishwa mule kwenye mistari iliyo chongwa kama msalaba.

Tulipomaliza zoezi lile, kila mtu akapewa kibao chake na kuruhusiwa kwenda kulala.

Kabla ya kwenda kulala mzee alitupa masharti ya dawa ile, akatuambia hii ndio LUPATU Wajukuu zangu, hamtarogwa na mtu yoyote kwenye dunia hii. Akatuambia lakini dawa hii ina masharti.

1 Usiende nayo kwenye shughuli yoyote ile, iwe harusi ama maziko.

2 Ukifika popote (ugenini) unatakiwa uwaambie wenyeji kuwa una kinga dhidi ya uchawi, hivyo hairuhusiwi kwa mtu yeyote kugusa uchawi mpaka utakapo ondoka.

3 Ukitaka kulala na mwanamke, iache nje (nje ya mlango)

Chengine, alituambia kuwa, hiyo dawa inafanya kazi umbali wa nyumba kumi kutoka kushoto, nyumba kumi kulia, nyumba kumi mbele ya nyumba, nyumba kumi nyuma ya nyumba.


Siku iliyo fuata mimi na Carlos tukaondoka, kila mtu akielekea kwao.

Carlos nilimuacha kwao Mueda, mimi nikavuka boda nikaingia nyumbani Tanzania. Nilipofika home, nikawaambia ndugu zangu hasa watu wazima. Pale home, mzee kuliko wote ni mama yangu mkubwa.

Hii ni nyumba ya familia (akina mama wamerithi nyumba ya baba yao) Kuna watu wengi sana.

Basi baada ya mapokezi, uchovu wa safari ilinibidi nipumzike kidogo (nililala)

Nilivyoamka jua lilikua limeshazama, hivyo jioni ilisha ingia.
Nikatumia muda huo kuwaambia wale waliokuwepo siku hiyo.
Nakumbuka alikua Mama mkubwa, dada yangu wa kwanza kuzaliwa, Mjomba pamoja na madogo walio kuwepo hapo.

Nilinza kwa kuwaambia kuwa nina dawa ya uchawi, hivyo kama kuna mchawi basi asichezee uchawi wake mpaka mimi nitakapoondoka.

Niliongea kimasihara kwakua nilitegemea nyumbani hakuna mchawi.

Mama yangu mkubwa akaomba nimuoneshe hiyo kinga (dawa).
Nikaingia mfukoni nikakitoa kile kibao. Kila mtu alicheka na kusema Mocambique wanaamini sana uchawi.

Usiku uliingia na kila mmoja akaenda zake kulala.

Siku ya pili palipokucha nikaelekea zangu Karikoo, kwenda kuchenji Dollar zangu. (Kariakoo Bazar )

Siku hiyo nakumbuka nilikula sana mtungi, nikarudi home usiku sana kama mida ya saa sita hivi usiku.
Nilipo fika home, kwa uchovu wa pombe nikajilaza kitandani, mara hazikupita dakika nyingi nikaanza kuona chumba kina mwekua mwekua, yani kama mtu kashika kioo anakizungusha mule ndani.

Nikaamka, mara ya kwanza nilidhani ni pombe labda, lakini jinsi muda ulivyokua unaenda ile hali ndio ilikua inazidi.

Ilipita kama dakika 20 hivi huku ile hali ya kumulika ikiendelea, mara nikasikia Pah! Yani kama mtu kapasua chupa ya bia vile.

Baada ya ule mlio, ule mwanga wa kioo mule ndani ukapotea.
Usingizi ulinichuka mpaka asubuhi.

Cha ajabu naamka asubuhi nakuta watu pale home wamejawa na huzuni, nilivyouliza naambiwa mama yako mkubwa kaanguka jana usiku mlangoni kwake akitokea chooni, hivyo kawaishwa hospital Temeke.

Samahani ndugu zangu.
Hii story nilipanga kuimaliza leo leo, ila kuna hudhuru imenikuta, hivyo nitaimalizia baadae ama kesho.
Naomba munisamehe.

Kwakua chenji nilikua
Malizia mkuu,
 
Mama alikitazama kile kibao muda kama dakika 5 hivi, mpaka nikajistukia na kumuuliza mama, mbona anakiangalia sana?
"Mwanangu hichi kitu ni kikubwa wewe bado ni mtoto, kitupe kitakuletea madhara"

"Hiki ndicho kilicho waua dada yangu na kaka yangu"
Mama aliendelea kuongea huku machozi yakimtoka, mpaka mimi mwenyewe nikashikwa na wenge.
Aliendelea kuniambia, mpaka Kule kijijini watu wamesha jua kua ni mimi ndie nilie sababisha vifo vya Mama mkubwa na mjomba.

Hata watoto wa mjomba wamechukizwa na kitu hicho.
Basi mama akiniomba nikitupe kile kibao.


Mama hakukaa akaondoka kwake, huku nyuma akiniacha na mawazo kibao kichwani.


Kwa kweli nilikaa kama wiki mbili tu lakini nikawa tayari nisha sababisha vifo zaidi ya saba.
Maana ukiachilia kifo cha mama mkubwa pamoja na mjomba, pia hapa mtaani kuna vifo vitatu vya majirani, na vyote vina fanana.

Maana wote kabla ya kufa hutokwa na damu sehumu zote za siri, na wote wamenitaja kwamba chanzo cha kifo Chao ni mimi.

Siku moja nilitulia sehem peke yangu nikajiuliza maswali, nikaona ngoja niende kwa rafiki yangu Yombo dovya (huyu jamaa tume maliza wote yombo dovya primary school)

Nilivyo fika kwake, sikumficha, nimamweleza mkasa mzima, chakushangaza na yeye akaniambia hata hapo kwao kuna vifo vya wazee wawili viliongozana kipindi nilipo peleka begi langu kwao.


Nikarudi home, nakukata shauri kwamba lazima hiki kibao (kinga) nikitupe.

Siku moja, mtaani hapo kulikua na kigodoro, nikala mtungii nikasema leo lazima nikitupe hiki kibao.
Mala baada ya kukubali mtungi nikaongoza mpaka lelini, nikakitoa kile kibao nakukirusha kwa mbali.

Nikarudi zangu home na kujilaza kitandani na usingizi ukanipitia.

Asubuhi nilipo amka, nishaoga maji yangu nikatoa suruali nyingine nikavaa, nikaitoa ile suruali niliyo ivaa jana nakuanza kutoa vitu muhimu.

Nikazama mfuko wa kwanza nikatoa simu, mfuko mwengine nikatoa waleti, sasa nikawa nacheki mifuko ya nyuma ili nicheki kama kuna chenji chenji, katika angaika angaika zangu nakitoa tena kile kibao (ile kinga niliyo itupa jana yake kwenye kigodoro) kwanza nilipagawa nusu ya kudata.


Nakumbuka hiyo siku, nilipanga na mtu (dalali) niende nikaangalie kiwanja Mbande, lakini kutokana na tukio hilo ilinibidi nimpigie jamaa simu nakumuomba aniwie radhi kwa siku hiyo, kwani nilishindwa hata kutoka nje kwa siku hiyo.


MUENDELEE KUNI SAMEHE, MAMBO NI MENGI MUDA NI MDOGO. HATA KESHO NAWEZA NIKAMALIZIA. NITARUDI.
Kwahiyo jamaa tumesoma shule moja yaan Yombo Dovya au Jitihada, haya malizia story hiyo
 
Poa Mzee.
Walipo rudi na yule mzee, hata mimi nilikua tayari nisha toka nje, tayari kusaidia kazi za hapa na pale.
Nakumbuka mimi na jamaa flani tuliingia alipo lala maiti nakuanza kutoa vitu vilivyo mle ndani.

Yule mzee alipo fika akaingia mpaka chumba alicho lala maiti, (nahisi kuna mila zilifanyika humo.
Kama dakika 30 yule mzee akatoka mle ndani.

Shauku yangu kubwa ilikua ni kujua kua mwenyeji wangu yuko nae vipi yule malehemu?

Nilitamani kumuuliza lakini nilishindwa kutokana na hali aliyo kua nayo.

Mala, kukaanza kupambazuka, nikashukuru.

Nikajifanya kama nakwenda dukani kununua sigara, lakini akili yangu ili niambia niwahi kugonga paspoti yangu nitembee.
Nilivyo fika pale magresheni, kalibu kuna kiduka, nikanunua sigara nikalipua.

Kipindi naendelea kuvuta sigara, mala kaja mteja pale dukani, nakuanza kumpa habari za msiba yule muuza duka.

Nasikia, "malehemu kafa kwa kujipiga uchawi" nikaona ohooo, ngoja niingie kwa afsa uhamiaji nikagonge mie.

Nilipo gongewa tu paspoti yangu nikachukua tonda safari ya kwenda mtoni (Ruvuma)
Kuna kitu kilikua kinaniuma sana moyoni mwanangu.
Kitendo cha kuondoka bila kuaga, ukizingatia jamaa alini karimu kama ndugu yake, njia nzima nilitembea nikiraani.

Nilivuka Ruvuma, nikaenda mpaka magresheni ya Mocambique nikagonga paspoti yangu na kuingia ndani ya gari tayari kuitafuta Mueda.

Kama mida ya saa 6 mchana nikawa nishaingia Mueda.
Siku chelewa nikachuka gari iendayo Montepuez nikashuka Shapa.

Nilivyo shuka Shapa, (nyumba ya mzee LUPATU ipo barabani kabisa) nikaingia mpaka ndani na kumkuta mzee.

Mzee alipo niona alifurahi sana, akaniuliza maswala ya Tanzania, na kunitania hapa na pale (Wandengereko & wamakonde ni watani )

Nilijiuza naanzaje kumwambia kua nimekuja kuirudisha ile kinga?

Lakini nikikumbuka yale matukio, niki kumbuka mama yangu alivyo nihusia niirushe nilipo itoa, nika jipa moyo kumkabili huyu mzee.

Nikamwambia " babu nimeirudisha dawa yako, nitawamaliza Wandengereko"
Kwakua ni mtani alicheka na kuniambia, "unge wamaliza kweli, nyinyi Wandengereko ni wachawi sana".

Nilitulia pale mpaka jioni.
Kiza kilipo anza akaniita uwani na ndoo ya maji (Dawa) akaniogesha kama mwanzo.

Akanichukua tena mpaka kilingeni, nakuniamuru nikirudushe kile kibao kwenye ungo.

Kwenye ungo nilivikuta vile vibao vingii, na mimi nikakiacha humo kwenye ungo.

Kwakua ni usiku nili lala mpaka hasbuh.
Palipo kucha nikamuaga mzee kuwa naondoka.

Kwa mas hara yule mzee akaniomba anipe dawa nyingine.
Hii sio kinga, bali ni ndago ya utajiri (chuma ulete)

Yani aliniambia anipe nyoka atakae kuwa na uwezo wa kuingia madukani na kichota pesa na kuniletea.
Tena mpaka dawa yenyewe alinionyesha, yani ni kama kamba, lakini aliniambia kuna maelekezo akinipa basi hiyo kamba inaweza kugeuka nyoka na kuingia duka lolote na kuniletea pesa.

Siku taka hata kumchelewesha, nilimkatalia, na kumwambia mimi bado ni mdogo, sintaweza kuvitumia vitu hivyo.

Mida ya saa 2 asubuhi, gari ikapita nikaingia nakurudi zangu mgodini.

MWISHO.
 
Walipo rudi na yule mzee, hata mimi nilikua tayari nisha toka nje, tayari kusaidia kazi za hapa na pale.
Nakumbuka mimi na jamaa flani tuliingia alipo lala maiti nakuanza kutoa vitu vilivyo mle ndani.

Yule mzee alipo fika akaingia mpaka chumba alicho lala maiti, (nahisi kuna mila zilifanyika humo.
Kama dakika 30 yule mzee akatoka mle ndani.

Shauku yangu kubwa ilikua ni kujua kua mwenyeji wangu yuko nae vipi yule malehemu?

Nilitamani kumuuliza lakini nilishindwa kutokana na hali aliyo kua nayo.

Mala, kukaanza kupambazuka, nikashukuru.

Nikajifanya kama nakwenda dukani kununua sigara, lakini akili yangu ili niambia niwahi kugonga paspoti yangu nitembee.
Nilivyo fika pale magresheni, kalibu kuna kiduka, nikanunua sigara nikalipua.

Kipindi naendelea kuvuta sigara, mala kaja mteja pale dukani, nakuanza kumpa habari za msiba yule muuza duka.

Nasikia, "malehemu kafa kwa kujipiga uchawi" nikaona ohooo, ngoja niingie kwa afsa uhamiaji nikagonge mie.

Nilipo gongewa tu paspoti yangu nikachukua tonda safari ya kwenda mtoni (Ruvuma)
Kuna kitu kilikua kinaniuma sana moyoni mwanangu.
Kitendo cha kuondoka bila kuaga, ukizingatia jamaa alini karimu kama ndugu yake, njia nzima nilitembea nikiraani.

Nilivuka Ruvuma, nikaenda mpaka magresheni ya Mocambique nikagonga paspoti yangu na kuingia ndani ya gari tayari kuitafuta Mueda.

Kama mida ya saa 6 mchana nikawa nishaingia Mueda.
Siku chelewa nikachuka gari iendayo Montepuez nikashuka Shapa.

Nilivyo shuka Shapa, (nyumba ya mzee LUPATU ipo barabani kabisa) nikaingia mpaka ndani na kumkuta mzee.

Mzee alipo niona alifurahi sana, akaniuliza maswala ya Tanzania, na kunitania hapa na pale (Wandengereko & wamakonde ni watani )

Nilijiuza naanzaje kumwambia kua nimekuja kuirudisha ile kinga?

Lakini nikikumbuka yale matukio, niki kumbuka mama yangu alivyo nihusia niirushe nilipo itoa, nika jipa moyo kumkabili huyu mzee.

Nikamwambia " babu nimeirudisha dawa yako, nitawamaliza Wandengereko"
Kwakua ni mtani alicheka na kuniambia, "unge wamaliza kweli, nyinyi Wandengereko ni wachawi sana".

Nilitulia pale mpaka jioni.
Kiza kilipo anza akaniita uwani na ndoo ya maji (Dawa) akaniogesha kama mwanzo.

Akanichukua tena mpaka kilingeni, nakuniamuru nikirudushe kile kibao kwenye ungo.

Kwenye ungo nilivikuta vile vibao vingii, na mimi nikakiacha humo kwenye ungo.

Kwakua ni usiku nili lala mpaka hasbuh.
Palipo kucha nikamuaga mzee kuwa naondoka.

Kwa mas hara yule mzee akaniomba anipe dawa nyingine.
Hii sio kinga, bali ni ndago ya utajiri (chuma ulete)

Yani aliniambia anipe nyoka atakae kuwa na uwezo wa kuingia madukani na kichota pesa na kuniletea.
Tena mpaka dawa yenyewe alinionyesha, yani ni kama kamba, lakini aliniambia kuna maelekezo akinipa basi hiyo kamba inaweza kugeuka nyoka na kuingia duka lolote na kuniletea pesa.

Siku taka hata kumchelewesha, nilimkatalia, na kumwambia mimi bado ni mdogo, sintaweza kuvitumia vitu hivyo.

Mida ya saa 2 asubuhi, gari ikapita nikaingia nakurudi zangu mgodini.

MWISHO.
Mods waunganishe hii thread...
 
Kilicho nisukuma kuirudisha, ni kwanza mama yangu mzazi alikua hataki nitembee na kitu hicho (kumbuka usipo msikiliza mama yako, hiyo ni laana)

Pili ni mauza uza ya ile dawa.
Usiku, ikitaka kufanya kazi inaanza kumwekua mwekua, mpaka kero.

Nakitendo cha kuitupa (Mala mbili) na kila nikiitupa ina rudi tena, hapo ndipo ilipo kua inani kata mate.

Kiufupi hata wewe, ungeiogopa.
Mimi nisingerudisha hiyo dawa mpaka niombwe na raia tena kwa magoti.Wachawi walaaniwe.
 
Back
Top Bottom