Lupita Nyong'o in black panther movie

Kawaida yao lazima watuzingue. Mimi mtu wa series nimetizama nyingi tu ambazo zimegiziwa Kenya na zina actors wengi wa kikenya. Nazozikumbuka kwa majina ni ile Sense8 ambayo ili'bore' kinyama afu kuna nyingine action babkubwa, Strike Back. Ukitizama nadhani ni season za tatu na nne utadhani Eastleigh, Nairobi kuna vita vikali zaidi ya kule Kismayoo, Somalia! 🙂
 
Ndio huwa anakunywa vidonge vya kupunguza maumivu kwa sababu akimaliza ku shoot anakuwa kachoka especially Panadol
 
viziwa vyake vishakuwa vikubwa hivi?
Kwenye ile muvi ya slave alikuwa na saa sita ndogo sana hapo kifuan
 
Kawida yao lazima watizingue, mimi mtu wa series nimeona nyingi tu zina episode zilizoagiziwa Kenya.

Mbona series zipo nyingi tu ambazo zimeangaza Kenya, kuna moja sikumbuki jina ila scene ya Kenya ilikua ya uwongo sana, yaani ndio nikajua hizi movies huwa hazionyeshi uhalsia. Eti jamaa wa MI-5 wakishirikiana na mwengine sijui wa CIA wanapigana marisasi na magaidi fulani mjini Nairobi, tena mchana kweupee bila wana usalama wa Kenya kuingilia.
Yaani mpigane wenyewe marisasi na kulipuana kwa vilipuzi mjini hapa...na hakuna kapolisi hata kamoja kanaonekana.
 
Jombaa, ni kuigiza tu, usipandwe na mori. 😀 Umewai kabla nifanye kaedit kiasi ila jina la hiyo series nimeitaja hapo juu.
 
Hahah hapo wamemaanisha polisi walipewa rushwa wasilete pua zao.
 
Angelina Jolie kwenye scenes fulani za Tomb Raider amezichezea kwenye mlima Kilimanjaro na Wakenya.
 
Inaitwa "strike back" kama sijakosea
 
Angelina Jolie kwenye scenes fulani za Tomb Raider amezichezea kwenye mlima Kilimanjaro na Wakenya.
Yeah, kuna scenes pia alizichapia sijui kama ni Marsabit County ila ilikuwa ni jangwani kiaina. Baada ya hapo ndo Kenya ilianza kuangaziwa sana ikifika kwenye movies, settings, storylines kama ile ya Maruge. Jombaa sijui kama unafahamu setting ya ile Lion King ni pale Hell's gate Naivasha? Nilitembea hadi hapo miaka michache iliyopita. Ile Pride Rock ukifika hapo usitoke bila kukwea hadi juu! Very nice!
 
MK254 kuna movie flani hivi hata si kuhusu Kenya, mambo ya conservation na gorilla kule Congo, mpakani mwa Rwanda. Star ni mwanamke flani hivi mzungu na sidekick wake mwanaume mwafrika, wanaishi jangwani wakitrack sokwe hao. Aisee nilipigwa na butwa walipoanza kuchapa kikikuyu hehehe. 😀 Wakimuita mwanamke huyo mchawi kwasababu ana nywele nyeupe. Hii ni baada yake kufika kijiji flani akapata watu huko wanauza nyama ya sokwe hao. Wakikuyu, sokwe, uchawi, Congo! Umeona hawa watu wanavochemshaga? Yaani laivu na wala si ishu kwao!
 

Hell's gate napafahamu tena sina hamu ya pale mahali, wacha hiyo ya kukwea pride rock, humo ndani kuna expedition fulani mnaingia kwenye aina ya miamba na mabonde yaani unafikia sehemu kwamba hamna jinsi ya kurudi nyuma na pia mnakokwenda kumekaa kihatari hatari muda wowote unaweza ukaanguka kutoka kwenye bonde na ufie mbali. Ilituchukua masaa kukamilisha maana kuna mhudumu alikua anatusaidia na kutuelekeza, ila baada ya hapo sijawahi kuwaza kurudi huko, it's a crazy death trap.....hehehe

Sehemu yenyewe inakaa kihivi

 

Hehehe!! Wapi na wapi maana haviendani.... Hawa jamaa hufanya movies bila utafiti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…