Sometime nakaa chini najiuliza hivi lupita angekuwa bongo hapa angepata kweli nafasi ya kuigiza, manake bongo movie ili upewe scene lazima uwe na bonge la shepu, sura nzuri hapo unakuwa tayari ushafuzu (sijui Kuna rushwa ya ngono) , kesho na ww msanii na ndio maana movie za kibongo hazivutii kwa sababu zinakosa uhalisia na watu makini, wenye vipaji halisi vya uigizaji ambao huongozea ubunifu ndani yake. Bila kusahau wanaume bongo movie full kujichubua na siku hizi wanachukua shombe shombe hawawezi kuigiza kazi kung'ata lipsi. Mtaani wamejazana watu kibao wanaojua kuigiza, ila kwa kuwa wanaangalia uzuri movie zao zitaendelea kukosa soko sana, mimi hapa bongo bora niangalie comedy kama akina tin white, Ringo, Senga, Pembe, Mboto nk mara nyingi naona zimebeba uhalisia kuanzia wahusika mpaka mazingira, lkn hizi movies zenu za ray, hemed PhD na wengineo hata sizikubali.