Lwakatale, Silinde na wenzao wameonewa sana na kudhalilishwa sana

Lwakatale, Silinde na wenzao wameonewa sana na kudhalilishwa sana

Hizi sio nyakati za kina sultani na mwinyi kwamba amri inatoka sehemu moja tu,inatekelezwa...Karne ya 21 hii.Hadi Iran anamvimbia Marekani....Wakati wa amri amri ushapita.
Naam, CHATO ikisha-amua hakuna wa kupinga, iliamuru washughulikiwee bungeni na nje yeye atawashughulikia, ikawa, mtu akala 37 za mguu na kiuno.
Aliagiza matajiri waishi kama mashetani na maskini waishi kama malaika, na ikawa.
akaagiza, upinzani ufutwe by 2020, unafutika, kama si yeye atafutika.
 
"Kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashtaka kwa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashtaka kwa maandishi"

EGOS, UMWAMBA, UMIMI, KUONYESHANA nani Kidume zaidi etc vimetumika kwenye sakata zima na hili halihitaji kuwa sugar-coated. Kama kanuni za chama zinasema mtu lazima apewe wito wenye makosa yake na aitwe kujieleza, no matter what, lazima hilo lifanyike. Huwezi kusema "ooh, hakukuwa na haja ya kuwaita kwa kuwa walikuwa wanatoa kashfa hadharani". Chama makini kilipaswa kuonyesha njia mbadala.
 
Huyo anayewapa jeuri hana chama...CCM ina wenyewe mtadhalilika sana kisiasa msipokuwa makini

Alishasema Jiwe kuwa wakienda huko ccm watakuwa sawa na ng'ombe waliokatwa mikia!!!
 
Hawajaonewa
Watu wanafanya mzaha na maisha ya WaTz
Mbowe yupo sahihi 💯
Ondoa wahuni wapo wengine watakuja
 
Maamuzi yaliyofanywa ni ya Mwenyekiti ama kamati kuu, mbona uko kama UFUDU?
Unajua maana ya Kamati kuu? hukuona Mwenyekiti akiendesha kikao kupitia tele conference?
Ulitaka awakusanye watu wakati kisha waambie kutokana na "KOONA"?

Tatizo la UVCCMwengi hamna elimu, wenye elimu wapo matawi ya chama nje ya nchi, wakija huku ni kuchukua Ubunge tu, nyie mnabaki walamba nyayo
mbona unarukaruka.yani wewe na elimu yako ndo unamawazo ya namna hii!!.aibu sana.
nimekuuliza swali kwa nini mtu akienda kinyume na mwenyekiti mnasema kanunuliwa ?
rwakatare kanunuliwa shilingi ngapi ?
mwenyekiti anakivuruga chama kwa speed kali sana watu makini wametoka woote yamebaki makapi tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
LWAKATALE, SILINDE NA WENZAO WAMEONEWA SANA NA KUDHALILISHWA SANA

Sitaki kujadili juu ya uhalalia ua kutokuwa halali kwenda au kutokwenda Bungeni hili lingeitimishwa na sheria na Miongozo ya CHADEMA kama ingefuatwa wakati wa kuhitimisha jambo lenyewe. Mimi nitajikita kwenye sheria na kanuni zenyewe.👇🏼

KATIBA NA KANUNI ZA CHADEMA ZINASEMA NINI?

Kwanza niweke usahihi kuwa katika chama cha Siasa Katiba ndiyo sheria mama ndiyo maana marekebisho yoyote yanapofanyika hayawezi kufanywa na mtu mmoja.

Lakini kanuni ni muongozo wa chama na marekebisho yaweza kufanywa na mtu yeyote anayeruhusiwa kufanya hivyo. Mfano CHADEMA sheria inampa nafasi katibu mkuu kufanyia marekebisho kanuni za chama pale anapoona inaleta tija. Pamoja na hayo yote hakuna mtu yeyote awe kiongozi au Mwanachama mwenye mamlaka ya kwenda kinyume na ama Katiba au Kanuni.

KWANINI LWAKATALE, SILINDE NA WENGINE WAMEONEWA?
Katiba ya CHADEMA toleo la Mwaka (2019) ibara ya 5.4 na vifungu vyake inazungumzia "kukoma kwa uanachama"
Nitaweka hapa ili twende pamoja.
5.4.1. kwa kujiuzulu mwenyewe kwa hiari yake.
5.4.2 kutokana na kufariki.

Msingi wa hoja yangu ni hapa;
👇🏼
"5.4.3 Kuachishwa ama kufukuzwa na tawi lake ama ngazi nyingine ya chama,kwa mujibu wa katiba kwa kukosa sifa za kuendelea kuwa mwanachama ama kuwa na mwenendo usioendana na Itikadi,Falsafa,Madhumuni,Kanuni,Maadili na Sera za Chama. Mwanachama atakuwa na haki ya kukata rufaa kwa ngazi ya juu kama hakuridhika na adhabu hiyo."

Yawezekana kabisa pasipo chembe ya shaka kuwa Lwakatale, Silinde na wenzao wamekiuka hicho kifungu cha katiba na kupelekea kukoma uanachama.

Nini kilipaswa kufanyika kwa mujibu wa katiba hiyohiyo ya CHADEMA?
👇🏼
Ibara ya ;
5.4.4 Bila kuathiri kifungu cha 5.4.3 cha Katiba Kamati Kuu inaweza kumuachisha ama kumfukuza mwanachama yeyote kwa mujibu wa Kanuni za Chama

Nikweli Kamati kuu inayomamlaka kamili na nguvu zote kuwafukuza Lwakatale, Silinde na wenzao na imefanya hivyo. Tatizo kubwa nini hasa? Kwanini waendelee kulalamika? Kwanini jamii inawatetea? Ni kosa la Spika wa Bunge? Nikweli kosa ni CCM? Hapana hayo yote hayawezi kuwa matatizo.

TATIZO NI KAMATI KUU CHINI YA MWENYEKITI WANGU MH FREEMAN MBOWE
Tuone Kanuni za Chama CHADEMA zinasemaje kuhusu kuwachukulia hatua za kinidhamu kwa Kiongozi kama Lwakatale, Silinde na wenzao;
👇🏼
Kanuni za chama
6.5.6 Kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashtakak wa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashtaka kwa maandishi.

6.5.7 kiongozi muhusika, zaidi ya utetezi wa maandishi,atapewa nafasi ya kujieleza bayana mbele ya kikao cha mamlaka ya nidham

6.5.9 Kiongozi aliyeadhibiwa atapewa taarifa ya msingi ya maamuzi ya mamlaka ya nidhamu ilik umuwezeaha kuamua kukata rufani au la.

Sasa ndugu zangu!
Hapo Lwakatare , Silinde na wenzao wanakosa gani? Tusijadili masuala haya kishabiki na kuweka kanuni na miongozo yetu pembeni. Kwanini tunaacha kutoa boriti kubwa kwenye mboni za macho yetu na tunakwenda kuhangaika na kibanzi kidogo pembezoni mwa jicho la Spika? Hivi kama tungefuata taratibu stahiki na miongozo ya chama katika kuhitimisha safari ya wenzetu ndani ya chama kulikuwa na tatiz gani?

Ndugu yangu Tundu Lissu nakuheshimu sana sana kiongozi kwanini hukushauri hili jambo la kisheria wakati wewe ni muumini mkubwa wa kuchukia matumizi mabovu na uvunjwaji wa Sheria? Kaka yangu Lema utu wa mwanadamu na kheshima kwa hawa wenzetu waliokiuka maagizo na tamko la chama kwanini hujawatetea?
Ndugu zangu, zamani tulikuwa tunaanza na Mungu kisha tunamaliza na Mungu kwenye hili la akina Lwakatale, Silinde na wenzie mlipata hasira kiasi gani hata mlishindwa Kuanza na Mungu kisha kumaliza na Mungu ili kuweka kumbukumbu sahihi? Kaka yangu Mchungaji Msigwa hapa neno la kichungaji katika ugawaji wa haki linasema nini hasa,tumeamua kufanya yaleyale ya akina Pilato enzi za kesi ya Yesu? Dada yangu Halima hapo vipi, Mbona kama hapajakaa sawa? Myika kaka wewe ni katibu Mkuu cheo ambacho najua unakimudu maana umekulia hapo lakini unawezaje kujitokeza kutangaza maazimio ambayo kwadhamira ya dhati kabisa unajua yanahila ndani yake? Hata kama ni kuwachoka wenzenu kwanini msifuate sheria mbona bado ninyin diyo wenye mamlaka na madaraka ya kuhitimisha hayo hofu ya nini?

Mshaurini Mwenyekiti vizuri hizi frastruations za kisiasa zisifanye muumizane kwa namna hii. Tanzania bado tunahitaji upinzani makini na wenye weredi ili kujenga na kuendeleza siasa za ushindani.

Baraza la vijana Bavicha kisima cha tafakuri lilifutwa? Au ndiyo kila jambo litakalo fanywa na kuamriwa na kamati kuu linakuwa sahihi? Wale ni wanadamu waambieni hii fukuzana bila kufuata taratibu utakua mchezo utawanogea kesho yenu itakua ngumu sana hasa kufikiri tofauti na wakubwa.

Hawa tunao washughulikia leo bila kufuata taratibu na kanuni zetu niwenzetu tumeumia pamoja, tulilala pamoja na tulimaliza pamoja. Siyo lazima kuwatunza wanapokosea lakini kufuata sheria kuna shida gani ili kuhitimisha vyema?

Haya, sasa leo tunawezaje kufungua katiba ili kumzodoa Spika wakati tumejaa Uchafu na dhurma kwenye mikono yetu? Kuna pahala hapajakaa sawa.

WAPENDA DEMOKRASIA KEMEENI HILI KWANI KIMYA CHETU NI HATARI KWETU NA KWADEMOKRASIA YETU, KULIKO KELELE ZA MAADUI WA DEMOKRASIA YETU.

Philipo Mwakibinga
0758910403
Mkuu walifanya kile wanachokiona kinafaa kama watu wazima,na Chama chao kikafanya kinacho wafaa ngoma drop,Acha wengine katika majimbo yao wachukue fulsa na watachukua kweli,uchaguzi Mkuu sio mchezo kipindi hicho kila MTU anakua anapambana na hali yake.Na tabiri mwaka huu kesi za washiriki ubunge za kupinga matokeo mahakamani zinaweza kua nyingi hadi kuvunja record maana hakuna mgombea atakae kubali kuporwa ushindi wakati ana ushahidi wa kutosha na ushindi wake moto utawaka.
Na ndo maana huwa nashangaa mdau humu jamvin akisema wabunge wa chama tawala watarudisha majimbo yote.Hakuna kitu kama icho maana wakati unapanga ili kwamba tiyari umemaliza kazi mwenzako anakua tiyari ana mipango zaidi ya iyo.
SISI wengine tunasubili mgombea binafsi sijui itakua lini sijui mpaka yesu akirejea!!
 
Mtoa nada nyumbani kwako mmekubaliana wewe na familia yako(mkeo na watoto) kwamba hakuna kutoka nje kwa Nia njema. Mara paap mkeo katika nje Tena we umekaa barazani kwako unamuona akitoka.

Kisha anamkuta jirani yako anasema " huyu fala kaamua tu nisitoke, mi nimeamua kutoka".... Utafanya maamuzi gani?

Lakini pia tumeona waliotoroka quarantine walifuatwa na polisi na kukamatwa.

Hayo yalikuwa maamuzi ya wote hivyo wote walipaswa kuyatii pasipo na uvunjifu wa taratibu Kama wanavyokubalianaga kutoka bungeni pale kuliwa na Jambo lililokuwa na maslahi mapana ya taifa.

Chadema are right.

Mbona hata CCM wamemfukuza MEMBE
 
Mtoa nada nyumbani kwako mmekubaliana wewe na familia yako(mkeo na watoto) kwamba hakuna kutoka nje kwa Nia njema. Mara paap mkeo katika nje Tena we umekaa barazani kwako unamuona akitoka.

Kisha anamkuta jirani yako anasema " huyu fala kaamua tu nisitoke, mi nimeamua kutoka".... Utafanya maamuzi gani?

Lakini pia tumeona waliotoroka quarantine walifuatwa na polisi na kukamatwa.

Hayo yalikuwa maamuzi ya wote hivyo wote walipaswa kuyatii pasipo na uvunjifu wa taratibu Kama wanavyokubalianaga kutoka bungeni pale kuliwa na Jambo lililokuwa na maslahi mapana ya taifa.

Chadema are right.

Mbona hata CCM wamemfukuza MEMBE

KUNYA anye kuku akinya bata KAHARISHA
 
“Nimepokea maamuzi ya Kamati Kuu CHADEMA na imenitaka nitoe malezo (ya kuingia Bungeni kinyume na agizo la Chama), niseme kwa hatua ya sasa nimepokea agizo la Chama, na ni kwanini nilifanya hivyo nafikiri Chama nitakiambia, kama nitaona kuna sababu ya kuwaelezea jamii au wapiga kura wangu hiyo itakuwa hatua nyingine”-Peter Lijualikali, Mbunge Kilombero.
 
Mimi naona umeandika ujinga mtupu, hivi kweli Selasini aliposema tena ndani ya Bunge, kuwa nimehamia NCCR Mageuzi, lakini nitabaki Chadema kwa ajili ya kumalizia ubunge wangu. Kwako wewe kichwa maji hukuelewa kuwa ashajifukuzisha chama?
Hivi alivyoongea Silinde, kuwa alichaguliwa na wananchi sio chama, na hata akiondoka Chadema atagombea kwa chama kingine. Je? Hukuona kuwa amekidhalilisha chama?
Hivi nikuulize Komu alivyosema atagombea ubunge kwa tiketi ya NCCR, hukuona kama amejiondoa kwenye chama?
Lwakatare aliongelea bungeni kuhusu kustaafu ubunge na siasa, pamoja na kujivua nafasi zote za chama, hapo huoni kuwa aliongelea mambo ya chama sehemu isio sahihi, kwani wewe lini umekuwa mwanachama wa CDM? Acha kutuletea utopolo wako hapa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli Wamekikosea Chama na viongozi. Tatizo ni TARATIBU za kikatiba hazikufuatwa. Wataalam wa Sheria wanasema " unfair termination"
Watarudishiwa uanachama kwa sababu TARATIBU hazikufuatwa.
 
"Kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashtaka kwa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashtaka kwa maandishi"

EGOS, UMWAMBA, UMIMI, KUONYESHANA nani Kidume zaidi etc vimetumika kwenye sakata zima na hili halihitaji kuwa sugar-coated. Kama kanuni za chama zinasema mtu lazima apewe wito wenye makosa yake na aitwe kujieleza, no matter what, lazima hilo lifanyike. Huwezi kusema "ooh, hakukuwa na haja ya kuwaita kwa kuwa walikuwa wanatoa kashfa hadharani". Chama makini kilipaswa kuonyesha njia mbadala.
Unfair Termination
 
Back
Top Bottom