Lwakatare aufunika mji wa Bukoba

Lwakatare aufunika mji wa Bukoba

Kwa kuwa ushirikiano umeshindikana, wanasiasa mahiri lazima waamue uwanja wao kufanya siasa-ama CHADEMA au CUF. Kwa maoni yangu sioni kwa nini Lwakatare aendelee kubaki huko alipo. Kimsingi hana sababu!

Mbona unajichanganya, unasema wanasiasa mahiri lazima waamue kuwa CHADEMA ama CUF, halafu hapo hapo unaona Lwakatare hafai kubaki CUF.

Nikirudi kwa mada, kwa BK mjini hata uchaguzi wa 2005 huyu jamaa walimfanyizia CCM ili ashindwe. Mazingira ya siku ya kuhesabu na kutangaza kura yanaonesha hilo. CUF ina nguvu sana BK mjini.
 
Kila mchezaji ambaye anataka kuendelea kuwa bora huwa anaangalia ni timu ipi ambayo anaweza kujiunga nayo hata kama club yake wanamuhitaji sana , anachofanya ni kuitaka klabu yake kumuongezea mshahara, sasa kama CUF wameupunguza mshahara wa mchezaji wao mahiri timu nyingine zinzweza kumshawishi......
 
Mtanzania,
Haya ulioandika para ya mwisho ni kweli na huwa inafanyika. Ni lazima uelewe kila kitu kina wakati wake. Kuna wakati wa kufanya uliyosema na kuna wakati wa kukaa pamoja kuzungumzia yaliyofanyika. Kama unataka tukae shambani kila siku, ina maana hakuna siku tutapika na hakuna siku tutakula. Unaposema kila siku watu wanaandamana barabarani si kweli maana hujasema ni mara ngapi umeona haya yakifanyika. Nadhani na wewe umesukumwa tu msimamo wa ki si hasa.
Na pia ninakushauri uzungumze na raisi wetu MH. sana JMK na serikali yake ambao wao ziara zao haziishi mikoani na kimataifa. Tena hawa ufanya kwa gharama za kodi yetu wavuja jasho.
Mwisho hawa vijana si wajinga. Siasa ni sehemu ya maisha yao ni lazima waijadili. Maana walipojaribu kunyamaza kuijadili tu hapo wajanja wakaona ndio nafasi ya kuliibia taifa na wamepora kweli kweli mpaka nchi imebaki hoi.
viongozi wetu hawaoni haya kuita nchi yetu eti ni maskini. Wanashinda kuomba omba na wanaona fahari hata kututangazia kwa ufahari kwamba waliomba pesa na wamepewa au mara nyingine utasikia upuuzi kama niliosikia siku mbili zilizopita kwamba umaskini wa wazungu utatutia matatizoni! kwa nini? eti kwa sababu misaada itapungua. Huu ujinga ujinga tu. Vijana wasipojadili siasa hata kazi wanazofanya hazina maana. Ninachojua kuwa ni hakika maandamano hayo yalihusisha wote, vijana na watu wazima na ajabu wengi wanafanya kazi za vipato na kwa bidii kweli kweli.
Ebu nikuulize Mtanzania hata ukifanya kazi masaa 18 katika nchi hii ya wadanganyika kuna lolote utavuna? Sana sana utaishia hali ile ile ya umaskini tu. Na unajua kwa nini? Kwa sababu sisi ni wadanganyika na tunadanganywa na chama hiki cha majambazi. Hakika kama nchi itaendelea kuwa chini ya SISI M hatutapata maendeleo kamwe. Maana jitihada zetu wanazimaliza wao.

Mkuu Mchukia Fisadi,
Naelewa hoja yako hapo juu, ila nitatofautiana na wewe kuhusu kuchapa kazi. Ukifanya kazi masaa 18 una nafasi kubwa sana ya kufanikiwa kuliko hao wanaoshinda kwenye magenge ya majungu ya siasa.

Ni kama tunatumia muda mwingi mno kwenye mambo ambayo hayaongezi tija kwa mwananchi wa kawaida.
 
Mkuu Mchukia Fisadi,
Naelewa hoja yako hapo juu, ila nitatofautiana na wewe kuhusu kuchapa kazi. Ukifanya kazi masaa 18 una nafasi kubwa sana ya kufanikiwa kuliko hao wanaoshinda kwenye magenge ya majungu ya siasa.

Ni kama tunatumia muda mwingi mno kwenye mambo ambayo hayaongezi tija kwa mwananchi wa kawaida.

Nami nakuelewa mtz lakini wengi wamefanyakazi sana na mwisho wamekuwa frustrated na kufanya kazi kawaida.
Kama nchi hii tukiwa na system ya kulipwa kwa masaa hapo naweza kukuelewa. Lakini hii ya kushinda unaumia wakati hao wanasiasa wanapata pesa nyingi kuliko sisi! ni bora nikae kijiweni kuwasema🙂 Na nitawasema mpaka wanielewe.
Sasa basi mtz tuombe nchi hii tulipwe kwa kila saa unayofanya kazi pesa ya kueleweka uone kama watu watakimbilia katika siasa tena. Hao maprofesa, madaktari, mainjinia, waandishi wa habari n.k nakuambia hawatakwenda siasani. Maana siasani ndiko kuna malipo ya bure ambayo hatak ama mtu hajafanya kazi analipwa malipo manono.
 
Yaani kama vile upo bongo! Huku kazi siku hizi ni siasa, na siasa ni kazi! Kila mahala ukipita mjadala ni siasa. Na inaonekana kama vile huwezi kuchangia maendeleo mpaka uwe mwanasiasa!

Hata hivyo, haya maandamano ni changamoto kubwa kwa CUF. Maana walipomtema kwenye uongozi kiaina sidhani kama walijua nguvu yake huku Bukoba. Kimsingi Lwakatare ni nguzo nzito sana ya CUF huku bara, kiasi kwamba akinyanyua mguu akautua kwingine atakuwa ameisambaratisha kabisa nguvu ya CUF huku. If I were to be a devil's advocate, can we sustain two strong opposition political parties in TZ? Kwa kuwa ushirikiano umeshindikana, wanasiasa mahiri lazima waamue uwanja wao kufanya siasa-ama CHADEMA au CUF. Kwa maoni yangu sioni kwa nini Lwakatare aendelee kubaki huko alipo. Kimsingi hana sababu!



- Strong na ni reality.

FMES!
 
Nami nakuelewa mtz lakini wengi wamefanyakazi sana na mwisho wamekuwa frustrated na kufanya kazi kawaida.
Kama nchi hii tukiwa na system ya kulipwa kwa masaa hapo naweza kukuelewa. Lakini hii ya kushinda unaumia wakati hao wanasiasa wanapata pesa nyingi kuliko sisi! ni bora nikae kijiweni kuwasema🙂 Na nitawasema mpaka wanielewe.
Sasa basi mtz tuombe nchi hii tulipwe kwa kila saa unayofanya kazi pesa ya kueleweka uone kama watu watakimbilia katika siasa tena. Hao maprofesa, madaktari, mainjinia, waandishi wa habari n.k nakuambia hawatakwenda siasani. Maana siasani ndiko kuna malipo ya bure ambayo hatak ama mtu hajafanya kazi analipwa malipo manono.

Mchukia Fisadi,

Unataka ulipwe na nani? Unaweza kufanya kazi za kujisaidia mwenyewe na familia yako. Pia unaweza kusaidia kazi za kuendeleza jamii, sio lazima ushinde ofisini ukichapa kazi. Hata ukibaki nyumbani na watoto na kuwasaidia homework bado ni kazi yenye tija kuliko kwenda kuwashangilia/kuwabeba wanasiasa.

Kama ni uchaguzi mwaka kesho upo, tutapiga kelele sana, tutashangilia sana na pia tutazomea sana. Baada ya hapo turudi kuwajibika.
 
Mchukia Fisadi,

Unataka ulipwe na nani? Unaweza kufanya kazi za kujisaidia mwenyewe na familia yako. Pia unaweza kusaidia kazi za kuendeleza jamii, sio lazima ushinde ofisini ukichapa kazi. Hata ukibaki nyumbani na watoto na kuwasaidia homework bado ni kazi yenye tija kuliko kwenda kuwashangilia/kuwabeba wanasiasa.

Kama ni uchaguzi mwaka kesho upo, tutapiga kelele sana, tutashangilia sana na pia tutazomea sana. Baada ya hapo turudi kuwajibika.
Hatimaye nimekuelewa. Nitachapa kazi kwa bidii, na nitajihusisha na siasa at a go. Nitawajibika kikweli si mchezo. Nitaifukuzia shilingi kweli kweli na siasa sintaiacha nyuma. Mimi ni mjasiliamali wa wajasiliamali tangu miaka ya 1984 na najituma kweli. Niko kazini mara nyingi masaa 17 na 19 kila siku na naona hali inatisha. Sikati tamaa bali nitaongeza bidii kwa yote Kazi na siasa. 2010 nitaongeza bidii katika siasa angalau na mimi niukwae ubunge niingie mujengo maisha yatabidilika zaidi maana huko ndiko kwetu wanasema kuna chungu cha mboga ya wanaume😀
 
Sisi wenyewe tuliokubali kudanganywa na tukadanganyika ni WADANGANYIKA!
 
Hiyo ni ishara njema nakumbuka kule Pemba mambo yaluvyoanza kuwageukia CCM yalikuwa hivyo hivyo ,hapo si jingine ila ni kuamka kwa baadhi ya WaTanzania aidha naweza kuona sababu moja ya huyu Lwakatare asikuwepo katika ukubwa ni kuwa Lipumba ameona iko haja ya Lwakatare kurudi nyumbani na kuweka kambi au na ili kupambana na hila za CCM natumai inawezekana kabisa ni mikakati ile iliyowafanya wale wenye nguvu za mapambano kurudi sehemu zao ili kuanzisha au kufufua nguvu ,tumeona Mbowe ,Slaa ,Mrema nao kama sijakosea wameamua kurudi kwenye vyanzo vyao ili kuimarisha upinzani.
CCM inajua wazi haikushinda kwa haki kule kwa Lwakatare na hivyo hivyo sehemu nyengi ,hila zilizotumika ni kuipunguzia nguvu CUF ndani ya Bunge kwa kuwanyima wabunge kwa kuona kule Zanzibar huwaga inakomba viti vyote ,lakini tunapoelekea sasa ni kubaya zaidi kwa CCM aidha kama wanahitaji ushindi watumie njia yao ile ile waliyotumia Zanzibar ya kupora masanduku ya kura ,kwa Tanzania ya leo na ugumu unavyozidi basi CCM kwa kweli kila siku zinavyokwenda basi hali inazidi kuwawia vigumu. Hongera wananchi wa Bukoba.
 
Hivi ITV ilionyesha hizi sherehe live au ni kutafuta udaku tu kule ZenjCUF walivipiga marufuku vyombo vya habari vinavihudhuria halafu visionyeshe kitu katika luninga.Nakumbuka vuguvugu la kuanguka kwa Sultani CCM kule Zanzibar ,CUF mwisho halafu sherehe zao hazina dogo wataranda mji mzima na kukomba watu utafikiri mdundiko ajabu hiki Chama kinapendwa mpaka na watoto wachanga ,yaani mtoto anaanza kusema unamsikia CHI YU EF ,au uongo jamani ?
 
Ni ishara nzuri sana kwa Bwana Lwakatare lakini sijui ile kesi yake ya uchaguzi na mheshimiwa Kagasheki inaweza kumyima nafasi ya kugombea ubunge mwaka 2010.

Lwakatare alikuwa na kesi ya kujerui / kufanyafujo mara baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa.

Iwapo alikutwa na hatia mheshimiwa Lwakatare hatakuwa na sifa za kugombea ubunge katika uchaguzi mkuu mwaka 2010.Ninavyojua Lwakatare alishindwa labda kama atakuwa amekata rufaa.
 
Hee!!!

IMEKUWAJE TENA JAMANI! SI TULIAMBIWA HAPA KUWA LWAKATARE ANAHAMIA CHADEMA? LINI TENA KABADILI UAMUZI WA KUENDELEA KUWA CUF? PIA TUMEAMBIWA KUWA CUF NI CHAMA CHA WAPEMBA SASA HUKO BUKOBA PIA KUNA WAPEMBA!! JAMANI MAALIM SEIF WACHA KUSAFIRISHA MAMLUKI TOKA PEMBA HADI BUKOBA! SASA NA WEWE UMEANZA KUIGA TABIA ZA CCM ZA KULETA MAMLUKI WA KURA TOKA BARA HADI VISIWANI! AU HAYA YA SASA NDIO UTEKELEZAJI WA MAAZIMIO YENU YA CUF KUWA "NGOMA ITAKAVYO PIGWA NDIVYO MUTAKAVYO ICHEZA"?

Zilikuwa ni tetesi tu ndugu yangu. Mwenyewe katangaza kuwa atabaki CUF na alisema hawezi kuwaangusha wanachama waliompatia Ujumbe wa halimashauri kuu kwa kura nyingi sana kisa eti hajateuliwa kuwa kwenye safu ya juu ya uongozi.
 
Lwakatare alikuwa na kesi ya kujerui / kufanyafujo mara baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa.

Iwapo alikutwa na hatia mheshimiwa Lwakatare hatakuwa na sifa za kugombea ubunge katika uchaguzi mkuu mwaka 2010.Ninavyojua Lwakatare alishindwa labda kama atakuwa amekata rufaa.

Kesi ya kujeruhi ya Lwakatare alilipa faini yakaisha sasa hiyo inamzuia vipi kugombea?
Keshi yake ya kupinga matokeo pia alishindwa lakini ali appeal mahakama ya rufaa.
 
Na kesi yake ile ya polisi kumvua nguo na kumbakiza na chupi iliishia wapi ,mkiambiwa polisi wanaitumikia CCM mnaangua kilio ,ila siasa katika nchi zetu hizi ina bei kweli kweli na viongozi kama akina Lwakatale wamekubali kuinunua kwa bei yeyote ile.Sasa hata kama mahakama zikiamua hawezi basi yeye anaweza kuwaelekeza wananchi wamchagua nani na zaidi kuwa watu hawapendi mtu wanapenda sera za Chama mtarajiwa wa kuiongoza Nchi hii ,hiyo ndio hazina ya Mtanzania kubadili Chama Tawala.
 
Kumbe huyu naye alivuliwa nguo? Mbona Ismail Jussa katika maelezo yake kuwa viongozi wa CUF ni wapambanaji kuliko wa CHADEMA hakumtaja huyu? Naona aliwataja wazanzibar zaidi. Kwani nani amewaambia kuwa polisi ni wa CCM? CCM ina green guards bwana

........ndiyohiyo
 
Never underestimate Kagasheki,the guy is shrewd and well loaded!
 
Back
Top Bottom