M23 inaelekea Bukavu mjini

M23 inaelekea Bukavu mjini

MBOKA NA NGAI

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2025
Posts
350
Reaction score
576
Huko Kivu kusini, mwashariki mwa DRC, mpaka sasa, safari ya M23, inaelekea Bukavu mjini. Ni baada ya kuipokonya FARDC,Wazalendo,South Africa na Burundi uwanja wa ndege wa Kavumu.

Kwa hali isiyo ya kawaida, raia wengi wanaonekana kutoshitukia kukimbia makazi yao, huku wanajeshi wanaoondoka(FARDC) wakiwatisha kwa kufyatua risasi ili waongozane nao waachie mji M23 yenyewe.

1739537352371.png


1739538197545.png


View: https://x.com/i/status/1890367988055912467
 
Kwisha maneno, Mr Tshisekedi Chilombo kapanda ndenge kuelekea Paris kufanya sherehe za Valentine's day na Mke wake. Huku wanajeshi wa Burundi wakimbia na wengine kukamatwa mateka kwa wingi.👇🤣
 

Attachments

  • 20250214_145124.jpg
    20250214_145124.jpg
    146.2 KB · Views: 2
  • 20250214_144855.jpg
    20250214_144855.jpg
    36.3 KB · Views: 2
  • 20250214_144901.jpg
    20250214_144901.jpg
    34.9 KB · Views: 2
Chanzo Cha habari?
KAZI ni kipimo cha utu



 
Kwisha maneno, Mr Tshisekedi Chilombo kapanda ndenge kuelekea Paris kufanya sherehe za Valentine's day na Mke wake. Huku wanajeshi wa Burundi wakimbia na wengine kukamatwa mateka kwa wingi.👇🤣
Iseee
 
Mwanzo madai ya M23 yalikuwa kwamba jamii ya banyamulenge iliyokuwa ikiishi boma Kwa wingi ilikuwa inaonewa hivo wakaunda kundi Kwa ajili ya kujilinda , ila sasa wanaitaka Congo yote Kwa ujumla Hawa M23 Wana ajenda Yao nyuma ya pazia iweje wasisalie Goma kwanini wanaitaka Congo yote je wao ndo wanazani watakuwa watawala wazuri wa Congo?
 

DRC: M23 yaukamata Uwanja wa Ndege wa Kavumu wa Bukavu, kuelekea jijini​

Na AFP , Jeune Afrique
Iliwekwa mnamo Februari 14, 2025 14:38
Askari wa Kikosi cha Wanajeshi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC) ameketi nyuma ya lori huko Bukavu mnamo Februari 14, 2025. (Picha na Amani Alimasi / AFP)

Tarehe 14 Februari, waasi wa M23, waliudhibiti uwanja wa ndege wa Kavumu, ulioko takriban kilomita 30 kutoka mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini.​

Takriban wiki tatu baada ya kuuteka Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini, waasi wa M23 wanaendelea na harakati zao kuelekea Kivu Kusini. Lengo lao inaonekana ni kuteka jiji la Bukavu.

Mnamo tarehe 14 Februari 2025, baada ya mapigano mafupi, walichukua kwanza mji wa Katana katika eneo la Kabare kabla ya kusonga mbele kilomita kumi zaidi kutwaa udhibiti wa Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Kavumu, kulingana na vyanzo vya ndani vilivyowasiliana na jarida tajwa la kimstaifa la Jeune Afrique.

"Kavumu na mazingira yake, ikiwa ni pamoja na uwanja wa ndege, sasa iko chini ya udhibiti wa AFC/M23," msemaji wa M23 Lawrence Kanyuka aliandika kwenye mtandao wa X.


Mamlaka ya Kongo bado haijatoa maoni kuhusu matukio haya ya hivi punde, lakini mwakilishi wa jumuiya ya kiraia wa eneo hilo aliiambia jarida kubwa tajwa Jeune Afrique kwamba "FARDC [Majeshi ya Wanajeshi wa DRC] wamejiondoa."

Kavumu: umuhimu wake Kimkakati kuelekea Bukavu​

Ipo takriban kilomita 30 kutoka Bukavu, jiji kubwa zaidi katika Kivu Kusini, Kavumu inatumika kama kituo kikuu cha logistics cha jeshi la Kongo. Uwanja wake wa ndege ulikuwa muhimu kwa kurejesha askari, na kukamatwa kwake kunaondoa kikwazo cha mwisho kwenye barabara ya Bukavu.


Waasi wa M23 wanaendelea na mashambulizi yao licha ya "kusitisha mapigano mara moja" iliyoitishwa na wakuu wa nchi na serikali katika mkutano wa kilele wa Februari 8 mjini Dar es Salaam, Tanzania.

Mkutano huo ulifanyika kwa pamoja kati ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ambazo zote zinajumuisha DRC ikiwa ni mwanachama.

Katika taarifa ya tarehe 12 Februari 2025, serikali ya Kinshasa tayari ilikuwa imewalaani waasi kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano. Siku hiyo, vikosi vya M23 vilichukua udhibiti wa Ihusi katika eneo la Kalehe baada ya siku mbili za mapigano makali.
 
14 February 2025

Gavana wa Kivu Kusini Atoroka kutoka Bukavu​

1739555637916.jpeg

Picha maktaba : Gavana mheshimiwa Jean-Jacques Parusi Sadiki akiongea tarehe 8 February 2025


Wasiwasi unazidi kuongezeka miongoni mwa wakaazi wa Bukavu. "Hali ni mbaya sana," mkazi wa eneo hilo aliiambia jarida la lugha la kifaransa la Jeune Afrique. "Lakini mimi na familia yangu tumeamua kubakia hapahapa kusubiria hati yetu chini ya utawala wa M23 ."


Kulingana na habari zetu, gavana wa Kivu Kusini, Jean-Jacques Parusi Sadiki, aliondoka mjini kimya kimya Alhamisi usiku. Siku nne tu zilizopita, alikuwa amehimiza utulivu huku uvumi ukienea kuhusu waasi hao kusonga mbele kuelekea Bukavu .


Kulingana na Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu 3,000 wameuawa katika mapigano yaliyosababisha kuanguka kwa Goma mwishoni mwa Januari 2025.


Wakati huo huo, makanisa ya Kikatoliki na Kiprotestanti yanashauriana na wadau mbalimbali kutafuta suluhu la amani. Tarehe 13 Februari 2025, wajumbe kutoka makundi hayo mawili ya kidini walikutana na Rais wa Rwanda mheshimiwa Paul Kagame.

Siku moja kabla, walikuwa wamefanya mazungumzo na viongozi wa M23 huko Goma. Ujumbe wao ulianza mkutano tarehe 3 Februari 2025 huko Kinshasa na Rais Félix Tshisekedi, kabla ya mikutano na viongozi wa upinzani akiwemo Martin Fayulu-ambaye amekuwa akishinikiza kuwepo kwa mazungumzo ya kisiasa yanayoongozwa na kanisa-na Delly Sesanga, pamoja na wanachama wa mashirika ya kiraia.
 

14 February 2025​

Kinshasa, DR Congo

Waasi wa M23 wauteka uwanja wa ndege wa Kavumba huko Kivu Kusini​



20240209173532454847_IMG-20240209-WA0021.jpg

Picha maktaba : Mwonekano wa ndege katika uwanja wa ndege wa Kavumba mjini Bukavu (Kivu Kusini), Jumatatu Februari 5, 2024.
Redio Okapi/Ph. Freddy Lufulwabo

Uwanja wa ndege wa Kavumba huko Kivu Kusini ulikuwa chini ya udhibiti wa waasi wa M23, wanaoungwa mkono na Rwanda, mwanzoni mwa Ijumaa mchana. Waasi pia walivamia kituo cha biashara katika mji wa Kavumba (kilomita 30 kutoka Bukavu), vyanzo vya ndani vinaripoti.

Ilikuwa ni kutoka mji wa Kabamba katika eneo la Irhambi Katana ambapo waasi na washirika wao, wanajeshi wa Rwanda, waliingia katika eneo la Kabare asubuhi ya Ijumaa, Februari 14.

Siku ya Alhamisi, Februari 13, Vikosi vya Wanajeshi vya DRC na washirika wake waliweka upinzani mkali katika eneo la Kalehe dhidi ya waasi ambao tayari walikuwa wakijaribu kudhibiti uwanja wa ndege.


Vyanzo vya upatanishi vya Kavumu vinaripoti kuwa kutoka Katana hadi Kavumu, hakukuwa na makabiliano.


Juhudi zote za kuwasiliana na mamlaka ya kijeshi katika kambi ya Nyamunyunyi iliyoko karibu na uwanja wa ndege wa Kavumba hazikufua dafu.

Source : Radio Okapi
 
Sasa kile kikao cha SADC na EAC kilikuwa na maana gani kama waasi wanasonga mbele kuelekea Bukavu?

Uganda, Tanzania, Kenya, Malawi, Rwanda, South Africa, Somalia wote walisisitiza mazungumzo ya maridhiano mezani lakini watawala wa Bujumbura Burundi na Kinshasa DR Congo wao hawakutaka mapendekezo ya nchi hizo 8 wakiamini watashinda kwa risasi na mabomu.

Sasa nchi hizo 8 wameamua wawe watazamaji kuona kama Bujumbura na Kinshasa wataweza kushinda katika uwanja wa mapambano walioutaka.
 
Sasa kile kikao cha SADC na EAC kilikuwa na maana gani kama waasi wanasonga mbele kuelekea Bukavu?
Jamani, kuna kitu bado hamjaelewa. UN iliposema M23 inazidi jeshi lake uwezo, na kumbuka ndo anajifanya asikali Polisi wa dunia hii, huoni nyuma yake kuna jambo? Kama serikali ilishanyanganywa ardhi yake, hao hao wa UN wakaendelea kuoperate hapo hapo, jiulize ni kwa makubaliano na nani. Hii vita ina unafiki mkubwa sana. Jiulize warundi Elfu 10 waliopelekwa kuhakikisha uwanja wa ndege huo hauanguki, vita hivyo vya kitoto?
 
Back
Top Bottom