Maajabu ya jiji la Kampala

Maajabu ya jiji la Kampala

Kwenye Watanzania kuheshimika na kuunga mkono kwa asilimia zote, nakuunga mkono kwa asilimia zote. Uhamiaji hawakunihoji ipasavyo, ni kama vile walinitarajia kupita hapo muda niliopita.
Nakubaliana na wewe. Uhamiaji pale mutukula wanawaheshimu sana waTZ. Hawawakagui kabisa. By the way dereva wangu alinipeleka hadi kwenye taxi terminal pale mutukula
 
Ongezea kuwa asubuhi wanakula katogo na siyo chai na vitumbua kama Dar
Katogo ikoje mkuu? Mara ya kwanza kwenda kupata "breakfast" kwa mama lishe, nilipouliza kilichopo, niliambiwa kuna IRISH (viazi mviringo), MATOKE (ndizi), RICE (pilau), na vitu vingine ambavyo sivikumbuki. Nilichagua mchanganyiko wa IRISH, MATOKE, RICE, & MEAT, nikasindikizia na BLACK TEA. Ukumbuke hapo ilikuwa ni Asubuhi, nafikiri saa mbili Asubuhi.
 
Kuhusu vimini hata Africa magharabi nchi kama Ghana, Nigeria n.k wanavaa sana vimini mpaka nikawa najiuliza ndio kwanza vimeingia huku kwao au maana kitu kikiwa kigeni huvaliwa sana hata Bongo mwanzo ilikuwa hvyo.
Nafikiri ni suala la utamaduni na malezi!
 
Kuhusu vimini hata Africa magharabi nchi kama Ghana, Nigeria n.k wanavaa sana vimini mpaka nikawa najiuliza ndio kwanza vimeingia huku kwao au maana kitu kikiwa kigeni huvaliwa sana hata Bongo mwanzo ilikuwa hvyo.
Nafikiri ni suala la utamaduni na malezi!
 
13. Kwa baadhi ya niliongea nao, hasa wale waliokwishafika Tanzania, wanaamini Serikali ya Tanzania inawajali raia wake kuliko ya Uganda😄. Mfano mojawapo waliotumia ni gharama za Internet. Wanadai internet ya Tanzania ni nafuu sana ukilinganisha na ya Uganda
Ni kweli serikali yetu huku ni oyaoya sana.
 
Nimesoma huko Uganda shule moja inaitwa Eagle's Nest iko meko hapo Kati Kati ya jiji karibu na ikulu ya kabaka, miaka ya 2006 - 2009. Nilipapenda ug.

Kwangu Kampala ndo jiji namba moja. Manyabo wa kule Wana nyash za hataree.
Ulienda huko kusaka elimu badala kusifu mfumo wao wa elimu ukarudi na sifa za nyash....! Tutaijenga nchi yetu kwa mtindo huu kweli!!
 
Nimeanza kuelewa kwanini iddi amini aliitaka kagera. Yani kwa hayo maneno iko ni kihaya kabsaaaaa. Yani mhaya anaishi uganda bila shida ya lugha kabsa.
Ni kawaida kwa makabila ya mpakani kuwa na muingiliano wa kiutamaduni na mfanano wa lugha:
1. Wanadai wa Tanzania na Kenya
2. Wakurya wa Tanzania na Kenya
3. Wajaluo wa Tanzania na Kenya
4. Wahangaza wa Ngara wanasikilizana na Wanyarwanda
5. Waha wa Kigoma wanasikilizana na Warundi
6. Wahaya wa Bukoba wanasikilizana na Waganda
7. Wamakonde wa Tanzania wanasikilizana na watu wa Msumbiji
8. N.k., n.k.
 
Wale jamaa wakiona una amatanza (Tsh) watataka kila kitu ununue kwa tsh sio ela yao
Kumbe Tsh ni AMATANZA?

Naona mmeamua kunifundisha Kiganda!

Hela yetu ina thamani kuzidi yao. Hiyo inamaanisha uchumi wa Tz upo juu dhidi ya uchumi wa Uganda?
 
Umenikumbusha mbali MNO!!
Kuna bar mojo ilikua mjini kati ikiitwa SEX PUB palikua ni fire 🔥. Kampala murunjinyo ssebo!!
Nitarudi.
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Kuhusu boda boda - hao ndo walianza hiyo Biashara na neno boda boda limetokea huko .

"SEKIDO"

Sebo - mwanume
Nyabo - mwanamke
Ichintu chomkazi
Kaunga kamuogo
Esente - PESA.

Kiganda ni moja ya lugha nzuri Sana Ina ladha fulani.

Nb kuhusu HIV/AIDS uwe makini wao wanaiita slim .

Na mwisho abarikiwe Nyerere watz wanaheshimika Sana
Watanzania tunapendwa sana hasa nchi za Uganda, kenya, Rwanda, Zambia, Burundi,congo Malawi n.k .. mwanamke wa hizo nchi ukimwambia Mimi ni mtanzania fasta wanakubali..
 
Nimekipata. Nimekiona kinavyoandaliwa. Nimenunua kwa Ugx 2,000 maeneo ya Mulago.

Hii hapa ikiwa imeshawekwa kwenye mfuko mweupe.
Sasa jaribu na kabalagala mara nyingi inapatikana stendi ya mjini kati iliyokama shimoni hivi ukizunguka unapata ni kama buku tu iko kama bagia wanaita PaN Cake's sasa tulikuwa tunakunywa coke zile emori ndogo huko zipo sana uliza yoyote utapata tume tumia sana enzi hizo tunajitafuta. hahahah very nice...
 
Sasa jaribu na kabalagala mara nyingi inapatikana stendi ya mjini kati iliyokama shimoni hivi ukizunguka unapata ni kama buku tu iko kama bagia wanaita PaN Cake's sasa tulikuwa tunakunywa coke zile emori ndogo huko zipo sana uliza yoyote utapata tume tumia sana enzi hizo tunajitafuta. hahahah very nice...
Watu mna mauzoefu na majiji ya watu mapema basi😄

Hivi hayo mavyakula yao tukiyafanyia "marketing" Bongo hayatakubalika?
 
Back
Top Bottom