Maajabu ya maji ya kunywa katika kutibu Vidonda vya Tumbo na Bawasiri

Maajabu ya maji ya kunywa katika kutibu Vidonda vya Tumbo na Bawasiri

Kinaeleweka

Senior Member
Joined
Nov 10, 2014
Posts
153
Reaction score
121
Poleni na majukumu mbalimbali ndugu zangu,

Bila kuwapotezea muda,napenda kutoa ushuhuda juu ya umuhimu wa maji ya kunywa kama tiba katika kutibu tatizo la Vidonda vya tumbo na Bawasiri.

Tatizo la vidonda vya tumbo,kwangu lilikuwa ni la zaidi ya miaka mitano ,licha ya kujitahidi kutumia dawa mbalimbali za hospital lakini pia za asili za mimea nilizokuwa nikishauriwa na watu mbalimbali.Tatizo serious la vidonda vya tumbo lilikuwa halitokei mara kwa mara(labda mara moja kwa miezi 2) lakini lazima linipeleke hospital hata iwe usiku wa manane, nako nikifika naishia kuchomwa sindano ya kutuliza maumivu na dawa ambazo nadhani hazikuwa na msaada wowote.

Pia,niliwahi kupata changamoto ya Bawasiri na nikawa napata shida sana licha ya kushauriwa kutumia dawa za hospital na asili ili kutibu lakini sikufanikiwa kumaliza tatizo.

Tokea nimeanza kunywa maji kila siku glasi 2-3 matatizo tajwa hapo juu sijawahi kuyapata tena kwa kipindi cha miaka 2 iliyopita sasa.Licha ya kuendelea na ratiba yangu ya kutokula mchana mara kwa mara. Na pia naamini natibu magonjwa mbalimbali maana kiafya nimezidi kuwa imara.

Baada ya kugundua hilo, nimekuwa nikiwashauri watu mbalimbali kuhusu umuhimu wa kunywa maji
katika kutibu hayo magonjwa na nawahurumia sana watu wanaopoteza fedha nyingi kutafuta tiba mbalimbali za hayo magonjwa na hali hayo magonjwa yanatibika kwa maji tu.

Ndugu zangu,tujenge mazoea ya kunywa maji mara kwa mara hakika ni tiba kubwa sana kwa maradhi mbalimbali.
 
Maji yana umuhimu sana mwilini.

Kuna watu wanakaa hata siku 3 bila kinywa maji hasa dada zetu, mtu anakuambia sasa maji ninywe yanini na soda zipo.
Hakika mkuu,ni kuto kufahamu.Kuna jamaa yangu alifanyiwa operation ya Bawasiri na bado tatizo likaendelea kumtesa.Nilivompa ushauri wa kunywa maji kila siku hajalalamika tena hilo tatizo
 
Hakika mkuu,ni kuto kufahamu.Kuna jamaa yangu alifanyiwa operation ya Bawasiri na bado tatizo likaendelea kumtesa.Nilivompa ushauri wa kunywa maji kila siku hajalalamika tena hilo tatizo
Mshauri apunguze na kula vyakula vya wanga itamsaidia sana.
 
Watu maji wanajivuta sana kunywa ila soda sasa na beer wanakunywa pipa zima kwa siku.

Shemeji yako tulisumbuana sana eneo la maji nilimkazia sana awe anakunywa maji vizuri, nashukuru kwa sasa ameshakuwa kipanga eneo la maji kwanza anakubali kuwa maji yamempa mabadiliko makubwa sana eneo la afya ya mwili na akili.

So akikaa lisaa tu hajaona maji anajiskia kama mgonjwa. So kwasasa yeye ndie ananikumbusha mimi kunywa maji na anayanywa balaa.
 
Maji yana umuhimu sana mwilini.

Kuna watu wanakaa hata siku 3 bila kinywa maji hasa dada zetu, mtu anakuambia sasa maji ninywe yanini na soda zipo.
Siku 3 huyo anajitahidi, kuna m'moja anasema yeye akinywa sana maji kwa siku ni nusu glass hawezi kunywa zaidi ya hapo.

Aiseee nikamwambia ningekuwa mumeo ningekuchapa makofi.
 
Siku 3 huyo anajitahidi, kuna m'moja anasema yeye akinywa sana maji kwa siku ni nusu glass hawezi kunywa zaidi ya hapo.

Aiseee nikamwambia ningekuwa mumeo ningekuchapa makofi.
Wanajiangamiza bila kujua.
 
A glass full of warm water early in the morning before you take anything in your stomach,fanya hii,ndani ya mwezi 1 utakuja kunishukuru...
 
Watu maji wanajivuta sana kunywa ila soda sasa na beer wanakunywa pipa zima kwa siku.

Shemeji yako tulisumbuana sana eneo la maji nilimkazia sana awe anakunywa maji vizuri, nashukuru kwa sasa ameshakuwa kipanga eneo la maji kwanza anakubali kuwa maji yamempa mabadiliko makubwa sana eneo la afya ya mwili na aki sanali.

So akikaa lisaa tu hajaona maji anajiskia kama mgonjwa. So kwasasa yeye ndie ananikumbusha mimi kunywa maji na anayanywa balaa.
Hongera sana mzee kwa kulifanikisha hilo.Sio wengi wanaweza kufanya hivo na jakika kuna magonjwa mengi uneyaepuka
A glass full of warm water early in the morning before you take anything in your stomach,fanya hii,ndani ya mwezi 1 utakuja kunishukuru...
Ushauri mzuri mjuu
 
Back
Top Bottom