econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 20,189
- 29,663
Nchi hii wananchi walio wengi huamini kuwa mwanasiasa hupigania maslahi yao ila nyuma ya pazia mambo ni tofauti sana.
Kipindi cha awamu ya tano kweli kulikuwa na mapungufu ya kiuongozi kama pia ilivyo sasa maana haiwezekani uongozi ukawa kamili kwa asilimia mia!
Mfano ni Zitto Kabwe kipindi cha JPM kila mara aliitisha vikao na waandishi wa habari akikosoa uongozi wa Magufuli hususani kwenye utawala bora, uchumi na mikopo, lakini leo hii kwenye utawala hui wa mama Samia Zitto huwezi kumsikia!
Wengine wanasema Zitto ni mdini sana, wengine wanasema kalambishwa asali na pia alikuwa na chuki na Magufuli baada ya kumtosa licha ya kujitutumua kubaki bungeni kwenye hotuba yake ya ufunguzi novemba 2015 baada ya CHADEMA kususia hotuba yake.
Mbowe mwenye kitu wa CHADEMA naye alikuwa mkosoaji mkubwa sana wa utawala wa Magufuli na hususani akiendeshwa na chuki yake binafsi ya ukabila na kiukanda waliyonayo viongozi mengi wa CHADEMA lakini cha kushangaza tokea atoke gerezani hakuna anachoshauri wala kukosoa serkali picha ya maisha kupanda, Chini ya kapeti Mwamba Makamba asali maisha yanaendelea kamwachia Heche anajitutumua!
Fatma Karume naye ni wale wale blahblah za hali na mambo mengine ya kutetea hali za ushoga na mambo yao binafsi ya uanaharakati pasipo kujali masrahi ya wananchi zinaendelea!
Huwezi kumuona huyu Bibi naweza kumwita akimtetea mama ntilie au mama aliyeko kijijini huko,Samia kaingia madarakani kwa vile ni mzenji wenzake kimya kabisa kana kwamba mambo yako sawa mtaani!
Wananchi lazima waamke kutegemea wanasiasa uchwara kama hawa ni kupoteza mda maana wao kikubwa washibe hakuna kingine!
Mkishindwa kazi mnasingizia upinzani