Maajabu ya msanii Saida karoli .

Una Tatizo la R na L kama Kada Mkuu
 
Hakuna wapiga kelele kama nigeria lakini ukizisikiliza ngoma zao na flow za makelele ni lazma utaipenda

Saida ana sauti nzuri lakini uziskiiza ala za ngoma ya kihaya ni lazma utapenda tu na hata jinsi ya uchezaji wake ni lazma utapenda tu ...
kama huamini sikiliza wimbo wa salome by diamond yaani zile drums ni hatari.

Ila kwa Tz kuna kipindi mziki wa asili ulikuwa unapendwa sana..unaikumbuka segere bro ,mduara na zile nyimbo za kinyamwezi za kilimanjaro band ambayo ala zake zimetumika pia katika wimbo wa kassim - somo na pia kuna mdumange wa tanga , mganda wa nyasa....

We have got alot of music genres lakini producers na wasanii sio wabunifu katika kufanya research ya ngoma na ala za muziki..tumekuwa copy and paste ..

Ila watu mpunguze chuki na wahaya ..daahhh kama kuzaliwa muhaya ni hatia
 
Na akiimba kilugha tu na mahadhi ya asili ya kihaya inanoga sana kuliko saiv anavyochanganya Mara kingereza Mara km bongo flava anatupotezea ladha, wachezaji wanacheza kisasa sana ngoma zetu zikichezwa kiasili ukiongeza maumbile ya kibantu kwa wanawake wa kihaya utafurahika moyo wako

Nyimbo zake za zamani ziko njema sana hata video zilibeba asili halisi ya bukoba sio hizi za sasa
 

Hapo kwa Sarkses man umenigusa. Nina Album zake 2, kila nikitaka kusikiliza muziki mzuri naanza nae. Falling in love, Original, Rap Attack, Devil in Me, Mawe ndo best songs kwangu.
 
Bezikale upo correct, mziki ni zaidi ya maneno. Ofkzi nyimbo ya Neria ni hatari kwa masikio ya wapenda burudani.

Akchware umesahau nyimbo ya baadhi ya Waganda akiwemo marehemu Redio.

By the way, "wahaya" ni kabila kubwa lenye wasomi wote. Kure kwetu ili uwe mkata majani wa ng'ombe zangu lazima uwe na degree ya animal feeding ya SUA au Denmark
 
muziki ni hisia hauhitaji lugha yoyote ili kuweza kuufurahia ..
mpka leo nampenda mno YONDO SISTER BUT nikikuwaga cjui Kile anacho kiimba ..vipi kuhusu Bob Marley .Michael j..na wasanii wote waliokuwa wnatamba nyakati hizo pasipo sis kutambua ufanisi wa kuzitambua lugha zao vyema ..
by the way mtoa mada wamjua JUDY BOUCHER
 
ana sauti tamu... weee huoni kwanini watu wana penda kuch kuch wakati hatuelewi....
kuna kitu kinaitwa Lugha ya mziki, sauti ya mtu na mpangilio wa wimbo ,unaweza kukufanya uupende hata kama hujui una maana gani... ila kichwani mwako unajijengea taswira kwamba huu unazungumzia hivi... na hio ndio inaitwa Hit song
 
Rugha=lugha. Kinachopendwa ni muziki wake kwa ujumla wake si lugha. Anafanya MUZIKI kwa lugha ya kihaya au muziki wenye vionjo vya kihaya na si ngoma za kihaya per se. Mbona wakongo walituimbia kilingala na lugha za kwao na muziki wao tukaupenda sana tu. Huwezi kuimba hovyo hovyo tu kama nyimbo za lugha fulani kule kanda ya ziwa halafu upendwe.
 
Hahaha... haya bhn
 
Hivi wahaya nani kawaloga
Misifa tu et watu wanapenda kihaya mpsyooo
 
Huku kwetu Mbeya tuna Awilo wa Mbeya nyimbo zake ni hit huku kwetu,ukitaka kujua Awilo ni nani subiri Mbeya City wawe na mechi hapa Mbeya
 
Wakati tunashabikia akina Pepe Kale na Kanda Bongo Man tulikuwa tunajua wanachokiimba? Kamaleiiii!
 
Saida weka mbali na watoto.
Niliipenda sauti yake tangu nipo mtoto sijui mziki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…