Pre GE2025 Maajabu ya Msigwa ni kwamba kukosana kwake na Mbowe kumefanya mambo yote aliyoyachukia ndani ya CCM kwa miaka mingi yabadilike ghafla na kuwa mazuri!

Pre GE2025 Maajabu ya Msigwa ni kwamba kukosana kwake na Mbowe kumefanya mambo yote aliyoyachukia ndani ya CCM kwa miaka mingi yabadilike ghafla na kuwa mazuri!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Msigwa kwa muda mrefu sana amekuwa na msimamo mkali dhidi ya CCM, msimamo ambao ulitokana na orodha ndefu ya mambo ambayo hakuyapenda sana ndani ya CCM, pamoja na watu wenyewe wa CCM. Lakini sasa, akakorofishana na Mbowe, au tuseme akashindwa uchaguzi ndani ya Chadema na ikawa kichocheo cha badiliko kubwa kwa Msigwa tunaemfahamu.

Sasa suala la kujiuliza, au hasa la kumuuliza Msigwa ni kwamba, yale mambo ambayo hukuyapenda ndani ya CCM, au watu ambao hukuwapenda ndani ya CCM na aliona hawafai kuwa viongozi wa Tanzania, kushindwa kwake uchaguzi ndani ya Chadema, au kukorofishana kwake na Mbowe, kumeyabadilisha au kuwabadilisha watu hao na kufanya sasa yawe mazuri wawe viongozi wazuri?

Kwa mfano, kama Msigwa hakumpenda Bashe kwa uongo kwa Bunge juu ya vibali vya sukari, kukorofishana na Mbowe kunabadilisha uongo aliosema Bashe na kuufanya uwe ukweli? Au kama Msigwa hakumpenda Samia kutokana na mkataba wa bandari kwa DP World, sasa anampenda Samia na Mkataba wa DP World kwa sababu ameshindwa uchaguzi Chadema?

Msigwa anaweza kusema kuna mambo yamebadilika ghafla ndani ya Chadema ndio maana ameondoka, lakini zaidi tungependa kujua ni mambo gani yamebadilishwa ghafla ndani ya CCM na kuanza kuipenda CCM dhidi ya Chadema, au ni unafiki na umalaya wa kisiasa tu tunaoshuhudia hapa?

Ningemwelewa Msigwa kama angeondoka Chadema na kutulia nyumabani, lakini sio kwenda kwenye CCM alikowadosoa kwamuda wote huu. Kwa kufanya hivyo hastahili hata heshima ya kuitwa mchungaji katika unafiki kama huo.
 
Nilivyomwelewa ni kwamba ametimkia Sisiemu, si kwa lengo kuu la kimaslahi binafsi, bali kuwaguyuguzia mulemule wahasimu wake wa muda wote.

Huu mkakati wake ni kama nimeuelewa vile.

Kaulimbiu yake sasa ni kwamba adui usimwogope; mfuate kulekule aliko.

Hongera sana PM. Mwakani dai basi fomu ya urais ili tujue kweli unamaanisha.
 
Ukipitia hapa utaacha kumshangaa msigwa
Msigwa kwa muda mrefu sana amekuwa na msimamo mkali dhidi ya CCM, msimamo ambao ulitokana na orodha ndefu ya mambo ambayo hakuyapenda sana ndani ya CCM, pamoja na watu wenyewe wa CCM. Lakini sasa, akakorofishana na Mbowe, au tuseme akashindwa uchaguzi ndani ya Chadema na ikawa kichocheo cha badiliko kubwa kwa Msigwa tunaemfahamu.

Sasa suala la kujiuliza, au hasa la kumuuliza Msigwa ni kwamba, yale mambo ambayo hukuyapenda ndani ya CCM, au watu ambao hukuwapenda ndani ya CCM na aliona hawafai kuwa viongozi wa Tanzania, kushindwa kwake uchaguzi ndani ya Chadema, au kukorofishana kwake na Mbowe, kumeyabadilisha au kuwabadilisha watu hao na kufanya sasa yawe mazuri wawe viongozi wazuri?

Kwa mfano, kama Msigwa hakumpenda Bashe kwa uongo kwa Bunge juu ya vibali vya sukari, kukorofishana na Mbowe kunabadilisha uongo aliosema Bashe na kuufanya uwe ukweli? Au kama Msigwa hakumpenda Samia kutokana na mkataba wa bandari kwa DP World, sasa anampenda Samia na Mkataba wa DP World kwa sababu ameshindwa uchagugi Chadema?

Msigwa anaweza kusema kuna mambo yakebadilika ghafla ndani ya Chadema ndio maana ameondoka, lakini zaidi tungependa kujua ni mambo gani yamebadilishwa ghafla ndani ya CCM na kuanza kuipenda CCM dhidi ya Chadema, au ni unafiki na umalaya wa kisiasa tu tunaoshuhudia hapa?


JamiiForums-72271314.jpg~2.jpg
JamiiForums-2089014366.jpg
 
Unaweza kumwona Msigwa kama mtu ambaye amekuwa akiishi na rafiki yake kwa miaka mingi, na kuna jirani yao ambaye wanamchukia na kumdharau kwa sababu ya tabia zake mbovu zisizo za kistaarabu. Lakini siku ambayo huyo mtu anakwaruzana na rafiki yake wanaeishi pamoja, anaamua kumkimbia rafiki yake na kwenda kuishi na huyo jirani mwenye tabia mbovu zisizokubalika, na mbaya zaidi anaanza kumsifia katika jamii! Sasa hili linaweza kufanywa na mtu ambaye hayuyo vizuri kichwani.
 
😆😆😆😆😆 Siasa bwana
Tanzania hatuna wanasiasa kabisa. Hawa wabunge wetu, mawaziri wetu, sioni mwanasiasa pale. Anzia Ikulu, njoo kwenye Bunge, njoo kwenye baraza la mawaziri, kama kuna wanasiasa labda ni watano au sita. Wengine wote ni opportunist tu, wapo pale kutafuta fursa, na ndio maana matajiri wa Tanzania wanapatikana kupitia siasa.

Hebu niambie nani katika hawa viongozi wa CCM sijui, ACT wazalaendo nk unamwona ni mwanasiasa? Labda mtu kama Tundu Lissu nitakubali, Kafulila ndio, Zungu sawa, Lipumba yupo, Pole Pole, Mbowe ndio, Mpina kweli, Zitto sawa, na wengine wawili watatu. Lakini mtu serious unakaa unamwona Tulia, Msukuma, January Makamba, Nape, Bashe, unawaita wanasiasa? That is a joke.
 
Anakubalije kuhongwa kibwege? Mamluki huyo
Ninachotamani kufanya ni kukutana nae, nimwambie nipe orodha ya mambo ambayo ukiwa Chadema huyuyapenda kabisa, na uliona kwa mambo hayo CCM hawakufaa kabisa kuwa chama kinachoendesha nchi.

Kisha nimuulize kwamba sasa katika yote haya kwenye orodha yako, ni yepi yamebadilika ghafla na sasa CCM kimekuwa chama bora kwako unachostahili kukiunga mkono na kukisifia kwa wananchi.
 
CCM OYEEEEEE

MAMA MITANO TENA 😃😃😃😃😃
Miaka mitano tena ya uhuni huu wa kisiasa? Imenishitua sana kuona eti Msigwa anaingia ukumbuni, Raisi na Makamu wa Raisi na Waziri Mkuu sijui na nani, wanaanza kuimba tuna imani na Msigwa!

Yaani viongozi kama hawa wa kitaifa wako serious wanaimba tuna imani na mtu ambaye kila mwenye akili anaona ni ndumila kuwili asie na msimamo na huyo ndio mnaimba tuna imani naye, hivi nyie ni wanasiasa serious kweli, tuwaamini kuiongoza nchi hii kama watu makini?
 
Miaka mitano tena ya uhuni huu wa kisiasa? Imenishitua sana kuona eti Msigwa anaingia ukumbuni, Raisi na Makamu wa Raisi na Waziri Mkuu sijui na nani, wanaanza kuimba tuna imani na Msigwa!

Yaani viongozi kama hawa wa kitaifa wako serious wanaimba tuna imani na mtu ambaye kila mwenye akili anaona ni ndumila kuwili asie na msimamo na huyo ndio mnaimba tuna imani naye, hivi nyie ni wanasiasa serious kweli, tuwaamini kuiongoza nchi hii kama watu makini?
😃😃😃😃😃😃 NDiyo viongozi wetu Sasa
 
Mpaka anayekutumia anashangaa "Hee kumbe hili jamaa jinga kiasi hiki? Sasa huu ujinga lilificha wapi siku zote"
 
Unaweza kumwona Msigwa kama mtu ambaye amekuwa akiishi na rafiki yake kwa miaka mingi, na kuna jirani yao ambaye wanamchukia na kumdharau kwa sababu ya tabia zake mbovu zisizo za kistaarabu. Lakini siku ambayo huyo mtu anakwaruzana na rafiki yake wanaeishi pamoja, anaamua kumkimbia rafiki yake na kwenda kuishi na huyo jirani mwenye tabia mbovu zisizokubalika, na mbaya zaidi anaanza kumsifia katika jamii! Sasa hili linaweza kufanywa na mtu ambaye hayuyo vizuri kichwani.
Kama hao marafiki walikuwa wakidanganyana tu kuhusu ubaya wa jirani?

Labda mtimkaji amegundua hilo na kwamba mbaya wao halisi ni yule aliyekuwa akijifanya rafiki wa kweli.
 
Back
Top Bottom