antimatter
JF-Expert Member
- Feb 26, 2017
- 47,274
- 126,778
Hilo wala siyo shida.. mbona wahindi Wana vitega uchumi vingi Tanzania, na hakuna muungano kati ya Tz na India?.......Lakini zaidi ya nusu ya Wazanzibari wanaishi bara na wanavitega uchumi bara,na hilo linaweza kuwa kikwazo cha kuvunja Muungano,labda utabuniwa ushirikiano wa kindugu bila nchi hizo mbili kuingilia mambo ya nchi nyingine.
Mimi staki kumungunya maneno,tukivunja muungano kwa jazba,usishangae wakaja watu na visasi kuwa wazenj wote rudi kwenu.Hilo wala siyo shida.. mbona wahindi Wana vitega uchumi vingi Tanzania, na hakuna muungano kati ya Tz na India?
Jamani Matajiri wa pemba na wengine wa ZNZ watawekeza kwenye soko gani , na hizi nyumba zao zilizoko huku bara itakuwaje??Hitaji la siku nyingi la Wazanzibari waliokuwa wengi ni kulivua na hatimaye kuondokana na koti la muungano. Huu ndio ukweli wenyewe, ni sisi Watanganyika ndio ambao hasa tunauhitaji kwa udi na uvumba.
Seif anaelekea ukingoni mkuu!
Ungemuongeza na lingine hawa hawana aibu kbs. Hakuna kauli mbaya kama ya ubaguzi eti sileti maji au sileti umeme. Hizi siasa za ajabu sana.Umeandika upuuzi, yule anayesema hapa sitaleta maji mkichagua tofauti na chama changu huyo ndiyo anahubiri umoja na kusema watatumia dola kubaki madarakani ndiyo umoja? shame on you
Kama muungano ulikuwa wa hiari, kwa nini uwashikie watu bunduki kulazimisha waendelee na ambacho hawakitaki tena?“Mimi sioni tabu kumwambia (Magufuli) tugawane mbao”. Haya ni maneno aliyoyatamka Mgombea wa Urais Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad akiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika eneo la Mkele, Mjini Magharibi visiwani Zanzibar.
Kauli hiyo ameitoa sambamba na kauli zingine nyingi ambazo zinaonesha dhamira ya dhati ya Maalim Seif Sharif Hamad kuvunja Muungano endapo tu atachaguliwa kuwa Rais katika Visiwa hivyo.
Ameendelea kusema hata kama Rais Magufuli atachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania basi atamwambia Rais Magufuli abaki na Tanganyika na yeye (Maalim Seif) Zanzibar. Hii ni kauli inayoashiria wazi kuwa Mgombea huyu hana nia njema na Muungano ambao umedumu na kuenziwa na Marais wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi Zanzibar, kwa takribani miaka 56 tangu uasisisiwe na Waasisi wake, Hayati Mzee Abeid Aman Karume na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mnamo Aprili 26, 1964.
Tunapenda kumkumbsha Maalim Seif na Chama cha ACT Wazalendo kuwa dhambi ya ubaguzi mnayotaka kuitekeleza haitawaacha salama watanzania kwani itaathiri maisha ya watanzania wa pande zote ambao kwa miaka yote wameishi na kufanya shughuli zao za kiuchumi na kijamii mahali popote bila kubaguliwa wala kubughudhiwa.
Uimara na utulivu wa Muungano huu ambao ni mkongwe zaidi barani Afrika, umekuwa wa kutolewa mfano na kuzifanya nchi nyingi kuunda umoja ikiwemo Jumuiya ya Ulaya, Jumuiya ya Afrika Mashari na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), kuzitajakwa uchache.
Ni rai yetu kwa Wazanzibari na watanzania kwa ujumla, kuwakataa viongozi wa aina ya Maalim Seif ambae hata hajaingia madarakni anaanza kuonesha wazi wazi kuwagawa watanzania. Tuchague kiongozi kutoka Chama kitakachowaunganisha watanzania na kuwapa uhuru wa kufanya shughuli zao mahali popote bila kubaguliwa wala kubughudhiwa kwa ajili ya ustawi wa maisha yao.
Kwa namna ipi?kupiga maendeleo zaidi ikiwa nje ya Muungano
Nchi ndogo yenye mafuta na gesi asilia,utalii,bahari kwa uvuvi ,uchukuzi na kilimo cha mwani,kilimo cha mazao ya karafuu nk.Ni rahisi kujiongoza na kupiga hatua haraka zaidi kuliko kwenye muungano.Kwa namna ipi?
Kwasasa ni nani anawazuia kufanya hicho unachosema?, Kuna yeyeote mwenye maamuzi juu ya hayo asiye mzanzibar?Nchi ndogo yenye mafuta na gesi asilia,utalii,bahari kwa uvuvi ,uchukuzi na kilimo cha mwani,kilimo cha mazao ya karafuu nk.Ni rahisi kujiongoza na kupiga hatua haraka zaidi kuliko kwenye muungano.
Wakiweza kuboresha sekta ya utalii kutoka watalii laki sita kwa mwaka kwa sasa hadi milioni 2 tu,ukiongezea na uchimbaji wa mafuta na gesi ni wazi nchi hii ndogo yenye watu million 2 itakuwa nchi tajiri kuliko nchi yoyote katika Afrika Mashariki.
Katika Muungano kuna mipaka yake.Kwamfano majeshi ni sharti la Muungano, majeshi yana gharama kubwa.Zanzibar akiwa nje ya Muungano anaweza kupata ulinzi kutoka baadhi ya mataifa makubwa bila yeye kugharimia kitu,labda taifa kubwa wao kugharimia ustawishaji wa Zanzibar.Kwasasa ni nani anawazuia kufanya hicho unachosema?, Kuna yeyeote mwenye maamuzi juu ya hayo asiye mzanzibar?
Wakenya wangapi wanazunguka huko jee mumeungana nao nyinyi ni WAKOLONI WEUSI hamna lolote mumezoea kunywa damu za wazanzibarMaalim Seif ndio alivyo. Ni mchochezi na mnafiki tangu enzi zake CCM.
Bila huu muungano angeweza kuzunguka bara kwa uhuru hadi watoto wake wakasoma huku?