Maambukizi ya UKIMWI na tiba zake mpaka sasa

Maambukizi ya UKIMWI na tiba zake mpaka sasa

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Ukimwi upo na bado hauponi lakini mwaka 2008 ilikuja break through kubwa kwa wagonjwa. Dawa za ARV zlionyesha uwezo wa kumaliza vidudu vyote vizungukavyo kwenye mfumo wa damu. Wanaita kufubaza vidudu kwani vilivyojificha havina uwezo wa kushambulia mwili.

Mgonjwa anaetumia dawa na kila siku ilhali amefubaza vidudu hawezi kueneza ugonjwa kwa wengine. Hili limeshafanyiwa tafiti. Kama mume mke yuko HIV+ mnaendelea kubanjuana kama kawaida.

WHO wanasisitiza watu wote wapimwe na walioathirika waanze tiba mapema. Wameona kuwa Hii ni njia ya kuzuia maambukizi mapya na hatimae kuutokomeza UKIMWI.

Muhimu mfichiane siri na mhudhurie clinic pamoja. Haina haja ya kuwaeleza wazazi, daktari wenu ndiye msiri wenu.

NB: Mmoja wenu akiwa + muwe waangalifu na extra marital affairs, michepuko na ngono zembe. Yule mgonjwa tayari immnune system yake ina mgogoro, kumletea tena makaswende na ma gonorrhoea utampa shida.
 
ila bwana kupima ukakutwa mzima kuna raha yake. yaani hata ahadi na demu mpya huifurahii kivile maana unajijua uko fiti mambo ya kuambukizwa hutaki.



hapa nna ahadi na limama ila nawaza kama limewaka hivi wiki ya 2 namzungusha tu (hapa ni baada ya kupima na kukuta nko safi)
 
Daktari awe msiri, toka lini kukawa na siri ya watu 3? Siri ni yako mwenyewe.
 
hii ni ngumu, kuna daktari nafahamiana nae alipo gundua dogo flani kitaa amewaka akanitonya nicheze mbali na mademu anao kaza yule bwana mdg
Hiyo ni safeguarding issue, daktari ameona kulinda siri ya dogo kuna override usalama wa wengine. Hata hivyo dogo alitakiwa awe kwenye tiba kama amewaka.
 
Tiba ya ukimwi imefikia hatua gani hadi hivi sasa.
Ile Dawa ya Gamora bado haijaanza kutumika ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mpaka sasa hivi inayoaminiwa ni ARV’s, kuna dawa nyingi ziko kwenye majaribio lakini majaribio yake mpaka yathibitishwe kuwa ni salama kwa matumizi ya binadamu ni mchakato mrefu unaohitaji muda na pesa. Dawa inaweza kuwepo miaka 5-10 kuanzia sasa.
Lakini ARV’s zinasogeza siku na maisha yanakwenda. Siku hizi wangonjwa wanawasomesha watoto wao na kuwaoza.
 
Kwakweli daktari hatakiwi kutoa siri za mgonjwa ila ataitoa iwapo tu kuitunza siri ile kunahatarisha usalama wa wengine.

Hujakutana na daktari akiwa baa! 🤣🤣. Wenye visonosono, kaswende, kifua kikuu, ukosefu wa nguvu za kiume, ugumba wote out! Toka lini ugumba na ukosefu wa nguvu za kiume kwa wana ndoa ukahatarisha usalama wa wengine?
🤣
 
Hujakutana na daktari akiwa baa! 🤣🤣. Wenye visonosono, kaswende, kifua kikuu, ukosefu wa nguvu za kiume, ugumba wote out! Toka lini ugumba na ukosefu wa nguvu za kiume kwa wana ndoa ukahatarisha usalama wa wengine?
🤣
Hiyo ni unethical mpedwa.
 
Back
Top Bottom