Maamuzi haya ya serikali yana mapungufu.

Maamuzi haya ya serikali yana mapungufu.

Tikerra

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2008
Posts
1,702
Reaction score
147
Serikali imetangaza kwamba kuanzia sasa watoto wa shule wasiingie kwenye vijiwe vya kuonyeshea TV.Naipongeza serikali kwa kuelewa kwamba vijiwe hivyo vinachangia katika uharibifu wa maadili, lakini mbona kwa kuchelewa sana?Hata hivyo hatua hiyo ni ndogo sana.Ninaloshauri mimi ni kwamba serikali iende mbali zaidi.Ihakikishe kwamba vituo vya Television na Radio havitoi matangazo yeyote yanayopotosha maadili,na pia makampuni ya biashara nayo hayasambazi matangazo yanayochangia katika uhamasishaji wa ngono na upotoshaji wa maadili.Tukumbuke kwamba upotoshaji huo hautokei kwenye vijiwe vya kuonyeshea kanda za video na matangazo ya television tu, bali unatokea hata majumbani.
 
Serikali imetangaza kwamba kuanzia sasa watoto wa shule wasiingie kwenye vijiwe vya kuonyeshea TV.Naipongeza serikali kwa kuelewa kwamba vijiwe hivyo vinachangia katika uharibifu wa maadili, lakini mbona kwa kuchelewa sana?Hata hivyo hatua hiyo ni ndogo sana.Ninaloshauri mimi ni kwamba serikali iende mbali zaidi.Ihakikishe kwamba vituo vya Television na Radio havitoi matangazo yeyote yanayopotosha maadili,na pia makampuni ya biashara nayo hayasambazi matangazo yanayochangia katika uhamasishaji wa ngono na upotoshaji wa maadili.Tukumbuke kwamba upotoshaji huo hautokei kwenye vijiwe vya kuonyeshea kanda za video na matangazo ya television tu, bali unatokea hata majumbani.

Tikerra, hilo silo jambo la ajabu kwa serikali yetu. Kuna msemo: Nyoka huuma afikiapo. Yaani, hiyo ni namna serikali yetu inavyotenda. Siyo rahisi, kuziba ufa bali kujenga ukuta! Na ukiangalia mambo mengi yanaenda hivyo.

Kulikuwa na fununu wiki hii kuwa kuna kiwanda fulani hapa jijini kinatoa moshi unaoathiri wakazi wa eneo fulani. Lakini nilisikia kuwa "Hakuna taafira kama hiyo" badala ya kusema watafuatilia. Halafu kuna kiwanda kingine pale Mbagala Mission kinaharibu mazingira na pia moshi wake unaathiri wakazi wa eneo hilo, maana kiko katikati ya makazi ya watu. Lakini hutasikia neno lolote kutoka serikalini.

Labda kutakapoanza kutokea magonjwa ya ajabu ndiyo serikali itajifanya inawajali watu. Kwa hiyo, hata hilo la TV au filamu fulani zisizofaa kwa watoto lilishasemwa muda mrefu tu, lakini huko mitaani bado zinaonyeshwa na watendaji wa serikali wapo. Kelele kutoka baa zilizo katikati ya makazi ya watu bado zinaendelea lakini hakuna kinachofanyika.

Ndiyo, maana mimi naona watoto wakishaharibika na baadaye serikali kujifanya inajali sana, naona imejitahidi sana kwani haiwezi kuzuia kabla mpaka uharibifu utokee. Hiyo ndiyo NGUVU MPYA, KASI MPYA NA ARI MPYA!
 
Back
Top Bottom