hapo kwenye saba sielewi ,wewe umesema umeamua aache kazi aamie ughaibuni ...huo mshahara wa kutumia atautoa wapi akiacha kazi?
1.Mke wangu bado atabaki kuwa mke wangu katika hari yoyote ya maisha hiwe ya shida au tabu..nakumbuka nimetoka naye katika hari ya chini sana bado tukiwa wachumba.hivyo pesa isiwe kigezo cha kututenganisha leo zipo kesho hazipo.zaidi nikiona ametoka nje ya ndoa hapo maamuzi yatakuwa mengine.
Mkuu nadhani msingi wa mada yako ulikuwa hapo juu kwenye red..lakini nashangaa umeanza na hii kauli az if kwamba sisi ndio tumekwambia kwamba mkeo 'anafuja pesa' wakati wewe ndio umetuambia..any way..
Baki to ze topiki naomba tu unifafanulie:
-kwa nini mtoto hutaki aje huko ulipo?..
-kitendo cha kufanya marekebisho katika upokeaji/utumaji wa pesa kupitia wazazi endapo mkeo atashindwa kuja huko nadhani ungekifikiria zaidi..idea nzuri ingekuwa kumpunguzia amount na yeye kukupa mchanganuo..BTW ngoja tuone hii plan A kama itawork..ikishindwa njoo tena jamvini for plan B..
Ndio maana mimi huwa in rela life situation sithubutu kumshauri mtu mambo ya ndoa; jamaa anataka kutuuzia kesi kiaina; kumbe na wewe umeliona hilo. Lol.
Uamuzi sio mbaya sana ndugu, lla bado kuna uwalakini na mambo fulani ambayo kwa mtazamo wangu yataleta madhara kwa ndoa yako unayoipenda.
- Mkeo kupatiwa hela na wazazi wako nadhani sio vizuri, itamjengea imani na roho mbaya kwa wazazi: Mi nafikiri kwenye hili bora umtumie hela yeye mwenyewe na umuamrishe kiasi fulani cha pesa yeye ndio apeleke kwa wazazi. kama hii itashindikana labda uamue hiyo awali ambayo mi binafsi nadhani sio salama.
- Suala la mke kuacha kazi pia sidhani kama ni sahii sana labda utuambie huko ughaibuni unategemea kukaa kwa muda gani. kama ni miaka 2 au 3 bora mkeo aendelee na kazi yake kama kawaida. kumbuka kumleta huko mkeo utajiongezea gharama za maisha.