Maamuzi ya kamati kuu CCM kuhusu wateule itakuwa ndio fyuzi ya kulipua bomu linalotokota CCM

Maamuzi ya kamati kuu CCM kuhusu wateule itakuwa ndio fyuzi ya kulipua bomu linalotokota CCM

Huko CCM kuna bomu linatokota. Bomu hili linaitwa kwa majina tofauti. Umaarufu wake 'WAJUMBE"

Ni wazi kuwa kuna mchanganyiko wa sababu. Zikiwemo mtifuano wa CCM mpya na kongwe.

Rushwa na nguvu ya pesa.

Vita ya madaraka kuelekea 2025 ndani ya CCM.

Amini kwamba maamuzi ya Kamati kuu kuhusu wajumbe waliopitishwa yataleta madhara mbali mbali na itategemea hoja hizo tatu na vipi chama kama kilipokea taarifa sahihi kutoka chini.

Mkiwaamini TAKUKURU mjuwe wako walionunuliwa na wao vile vile wana mapenzi yao na watu wao kwenye chama.

Malalamiko ni mengi na mchanganyiko.

Kuna hatari Kamati kuu ikawa na wajumbe ambao wote wakawa na mlengo mmoja wa ama kuwa wanaunga mkono WANA CCM MPYA, ama wanaojipanga kuweka safu mpya ya madaraka baada ya utawala wa sasa na hivyo kwa namna moja ama nyengine kuathiri mchakato na kuacha uhalisia huko majimboni.

Kauli za Mwenezi Polepole sio kwamba zinaashiria kukoleza joto la kufyatuka kwa fyuzi lakini ziaashiria vile vile kuifanya fyuzi ikomae zaidi.

Huko majimboni kuna habari nyingi na kutegemea taarifa za TAKUKURU PEKEE na wale vijana wea Usalama wa chama bila kuwa na njia nyengine si rahisi UKWELI kujulikana kutokana na mazingira ya sasa.

Hapa tunataka kupima umakini wa viongozi wa CCM. Kilicho wazi kweli rushwa imetumika sana mara hii LAKINI na Fitna ya CCM mpya na Kongwe ndiyo sababu kuu. Kunahitajika maamuzi sahihi na kuwepo taarifa sahihi.

Wako watu wanaomuunga Mkono Mwenyekiti na wameshika nafasi nyeti serikalini lakini kwenye mchakato walitoa rushwa ya wazi na hao hao ndio CCM mpya. Je, jicho la haki litasimamia ukweli?

Tunasubiri muda uhukumu.

Tunawatakia maamuzi mema.

"Kweli wajumbe sio watu"


Kishada
Kuna upinzani mkubwa ndani ya CCM kuliko hata huu wa CCM na Chadema
 
Ndio tukaandika hapa ili wahusika watende haki. Hofu yangu isije ikawa taarifa walizopelekewa ikawa zilifika kwa misingi ile ile ya hizi hoja tatu hapo juu.
Hofu ya nini? ukionacho wewe ndio mwisho wako subra subra
 
Huko CCM kuna bomu linatokota. Bomu hili linaitwa kwa majina tofauti. Umaarufu wake 'WAJUMBE"

Ni wazi kuwa kuna mchanganyiko wa sababu. Zikiwemo mtifuano wa CCM mpya na kongwe.

Rushwa na nguvu ya pesa.

Vita ya madaraka kuelekea 2025 ndani ya CCM.

Amini kwamba maamuzi ya Kamati kuu kuhusu wajumbe waliopitishwa yataleta madhara mbali mbali na itategemea hoja hizo tatu na vipi chama kama kilipokea taarifa sahihi kutoka chini.

Mkiwaamini TAKUKURU mjuwe wako walionunuliwa na wao vile vile wana mapenzi yao na watu wao kwenye chama.

Malalamiko ni mengi na mchanganyiko.

Kuna hatari Kamati kuu ikawa na wajumbe ambao wote wakawa na mlengo mmoja wa ama kuwa wanaunga mkono WANA CCM MPYA, ama wanaojipanga kuweka safu mpya ya madaraka baada ya utawala wa sasa na hivyo kwa namna moja ama nyengine kuathiri mchakato na kuacha uhalisia huko majimboni.

Kauli za Mwenezi Polepole sio kwamba zinaashiria kukoleza joto la kufyatuka kwa fyuzi lakini ziaashiria vile vile kuifanya fyuzi ikomae zaidi.

Huko majimboni kuna habari nyingi na kutegemea taarifa za TAKUKURU PEKEE na wale vijana wea Usalama wa chama bila kuwa na njia nyengine si rahisi UKWELI kujulikana kutokana na mazingira ya sasa.

Hapa tunataka kupima umakini wa viongozi wa CCM. Kilicho wazi kweli rushwa imetumika sana mara hii LAKINI na Fitna ya CCM mpya na Kongwe ndiyo sababu kuu. Kunahitajika maamuzi sahihi na kuwepo taarifa sahihi.

Wako watu wanaomuunga Mkono Mwenyekiti na wameshika nafasi nyeti serikalini lakini kwenye mchakato walitoa rushwa ya wazi na hao hao ndio CCM mpya. Je, jicho la haki litasimamia ukweli?

Tunasubiri muda uhukumu.

Tunawatakia maamuzi mema.

"Kweli wajumbe sio watu"


Kishada
ipo hivi CCM wote walitoa Rushwa hakuna CCM hakutoa Rushwa na kama Rushwa ni kigezo chao kikuu wakipaswa kufuta mchakato wote warudie upya kabsa, mfumo huu wa CCM umezalisha fursa kwa baadhi ya Takukuru kununuliwa kutengeneza report za kuwahujumu wengine ambao hawana pesa za kuwanunua Takukuru kuzuia report za uonevu, mfumo huu umeruhusu Majungu fitna za kutengeneza kushika kasi, Kamati kuu siyo mungu siyo malaika wana mapungufu yao na wana ndugu zao marafiki zao lazima watachemsha sana kwenye hilo na chadema AcT wamewategea ili wapate CCM wenye hasira za kuonewa wapate kuwasaidia kwenye kampeni.
 
Kuna upinzani mkubwa ndani ya CCM kuliko hata huu wa CCM na Chadema
Chadema wanajua CCM watavurunda huko hasa kwenye kumfurahisha Mwakyembe Bashite ngeleja Angela kairuki na wengineo marafiki wa zidumu fikra za mwenyekiti wa CCM Taifa, chadema wanasubiria kwa hamu kubwa CCM ichemshe kupitia mfumo huo uliopitwa na wakati
 
Ukiyajua yaliyoko field huko majimboni, unasisimka. Kuna wakubwa huwezi amini imekuwa kama icon ya chama lakini amepita kwa mizengwe. Amini nakwambia baadhi ya majimbo kashfa zinarudi hadi kwa wagombea wa kitaifa. Jee najiuliza haki itatendeka?
Mfano kule misungwi mnyeti katoa Rushwa na Kitwanga katoa Rushwa hakuna ambaye hakutoa Rushwa CCM wote wametoa Rushwa hapo ndipo utaona maajabu ya Dunia
 
0715132277 sele mpigieni huyo ni msiri wa Bashite atawaelezea jinsi walivyogawa Rushwa na jinsi watakavyowahujumu wengine ambao walishinda
 
Msemaji wa chadema ana sympathise na ccm halafu unategemea ccm ishindwe?
Yaani unanipenda sana ccm kufikia hata kuishauri namna nzuri ya kupata ushindi!
Mapungufu ya kamati kuu ya CCM kwenye kuchuja majina Dodoma yameonekana kwa kila Mtanzania hata wasio vyama wala ushabiki wowote wanalijua hilo vizuri
 
CCM hakuna msafi wa kumnyoshea mwenzake kidole na mda huu walioshindwa kura za maoni wengi wapo Dodoma hata walioshinda nao wapo Dodoma kutafuta fursa za kuwashawishi wajumbe wa kamati kuu wawaunge mkono, fursa za wajumbe sasa imehamia kwa wajumbe wa Kamati kuu kasoro mwenyekiti labda lakini hata yeye ana rafiki zake ambao anataka wawe wabunge ili baadae waje kupitisha Sheria ya kuwa na Rais wa milele kama china
 
ipo hivi CCM wote walitoa Rushwa hakuna CCM hakutoa Rushwa na kama Rushwa ni kigezo chao kikuu wakipaswa kufuta mchakato wote warudie upya kabsa, mfumo huu wa CCM umezalisha fursa kwa baadhi ya Takukuru kununuliwa kutengeneza report za kuwahujumu wengine ambao hawana pesa za kuwanunua Takukuru kuzuia report za uonevu, mfumo huu umeruhusu Majungu fitna za kutengeneza kushika kasi, Kamati kuu siyo mungu siyo malaika wana mapungufu yao na wana ndugu zao marafiki zao lazima watachemsha sana kwenye hilo na chadema AcT wamewategea ili wapate CCM wenye hasira za kuonewa wapate kuwasaidia kwenye kampeni.
Mimi nilishtuka jana Mwenyekiti kuanza kumpigia kampeni Ndugai, Hivi katika hali ile hata kama kuna ripoti ya kukiukwa kwa taratibu kweli Ndugai ataweza kushughulikiwa? wakati mwengine tuweke hakiba ya maneno rohoni, si kila kitu kinapaswa klusemwa hadharani.
 
Zipo kesi nyingi tu za malalamiko. Tatizo hilo Bomu la ' WAJUMBE" na Huko Kamati kuu liko. "WAJUMBE sio watu bwana iwe kwa level yoyote ile.

Kitu kimoja ambacho kiko wazi CCM rushwa imeshindikana. Hadi TAKUKURU nao baadhi wamenunuliwa.
 
ipo hivi CCM wote walitoa Rushwa hakuna CCM hakutoa Rushwa na kama Rushwa ni kigezo chao kikuu wakipaswa kufuta mchakato wote warudie upya kabsa, mfumo huu wa CCM umezalisha fursa kwa baadhi ya Takukuru kununuliwa kutengeneza report za kuwahujumu wengine ambao hawana pesa za kuwanunua Takukuru kuzuia report za uonevu, mfumo huu umeruhusu Majungu fitna za kutengeneza kushika kasi, Kamati kuu siyo mungu siyo malaika wana mapungufu yao na wana ndugu zao marafiki zao lazima watachemsha sana kwenye hilo na chadema AcT wamewategea ili wapate CCM wenye hasira za kuonewa wapate kuwasaidia kwenye kampeni.
Hiyo gut haipo, ni shida. Timu ya Kishada inakusanya taarifa tutakuja kuzitolea ufafanuzi baadae. Tunasubiri haki itendeke kwanza.
 
Mambo ya ccm mwaka huu yapo interesting mpaka wapinzani mnafuatilia kweli mwaka huu magafuli anapita bila shida.
Kitu kichafu na kinukacho hakiwezi kupita mbele yako usihoji.
CCM inanuka rushwa kwa kiwango cha juu kabisa katika historia yake.
Kwa wale wanaccm asili wanasema wazi kabisa kuwa CCM mpya ya Magufuli na Bashiru imeoza imevunda kwa rushwa.
Halafu huyo ndio mnakuja na story eti anapambana na rushwa?
Mbona mnawafanya watu mafala kiasi hicho?
Serikali inayoundwa na chama kibovu namna hiyo lazima iwe mbovu pia.
Kimya kilikuwa kingi, ngojeni kampeni zianze na hakuna wa kumfunga MTU mdomo ndio mtayajua mengi.
 
Msemaji wa chadema ana sympathise na ccm halafu unategemea ccm ishindwe?
Yaani unanipenda sana ccm kufikia hata kuishauri namna nzuri ya kupata ushindi!
Hajasema hayo ili mshinde, Bali chama chenu kisife ili kuwa na chama pinzani chenye nguvu ya kuisimamia vyema serikali yaani CCM.
Dalili za wazi ni CCM kuvurugana kwa hizi rushwa na uchawi
 
Hi maada ni puzzle, hasa jamaa mmoja akiongea kwenye maziko ya Mkapa ilinitafakarisha sana analo jambo ndani yake, hasa kwa wafukunyufu kumhusu mtaelewa
 
Back
Top Bottom