Maana Halisi ya Upinzani ni hisia. Upinzani si ugomvi, si uadui, si vita wala Usaliti

Maana Halisi ya Upinzani ni hisia. Upinzani si ugomvi, si uadui, si vita wala Usaliti

Mbahili

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
281
Reaction score
525
Awali ya yote, napenda kutumia fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kunifikisha siku hii ya leo na pia sitakuwa mtenda haki bila kuwashukuru waanzilishi wa forum hii. Baada ya kusema hayo machache, ningependa kukushukuru na wewe unaetumia gharama zako kusoma uzi wangu, huenda kuna mabadiliko ninayoweza kukuletea katika fikra yako hasa nitakachojadili hapa hususan kisiasa.

Kwa kusema hayo ,napenda niende moja kwa moja kwenye mada yangu. Mada yangu nitatumia marejeo tofauti, hivyo msishangae pia. Ninaweza anza na mifano michache.

Mfano wa kwanza
Tulipokuwa wadogo na kwenda kwa wajomba zetu, namaanisha mboga saba, wanakula kwa wakati na chakula kweli kizuri, Tunakaa kwa takribani mwezi mzima. Tukirudi nyumbani ratiba inayojirudia ni ugali, maharage, chai bila vitafunwa na pasi ndeeefu( nahisi naeleweka). kuna muda kama mtoto unaweka pingamizi flani moyoni, na unamiss urudi kwa mjomba au siyo? kile kitendo cha kutoridhika na ratiba ya chakula nyumbani na ku pamiss kwa mjomba, basi huo huitwa upinzani.

Huenda sisi ni familia moja ila unagoma kula chakula hicho na kuhamasisha japo tule kama kwa mjomba.

Mfano wa pili
Katika maandiko matakatifu, tunaambiwa kilichotokea mbinguni kwa shetani kufikiri kutaka kurithi kiti cha Enzi cha Mungu, hapo tunaona Shetani na Mungu wakawa Maasimu wakubwa. Ila cha kushangaza zaidi tukisoma katika kitabu cha Ayubu tunaambiwa Shetani kakutana na Mungu na Mungu kumtambia mjakazi wake Ayubu. Haiwezekani kuwa ilikuwa mara ya kwanza kwa Mungu kukutana na Shetani, kwa sababu maongezi yao yalionekana kama huwa wanazungumza mengi sana. Tunaona kama Mungu na Shetani ni Maasimu, lakini huwa wana mazungumzo so inshort sio Maadui kama tunavyoaminishwa. Hapa Tumejifunza kumbe upinzani sio uadui?

SWALI LETU
JE, UPINZANI NI NINI?

Neno UPINZANI umetikana na kitenzi PINGA, kwa wale wenzetu wa |the school bus| wanaita be AGAINST. Upinzani ni hisia, upinzani si ugomvi, si uadui, si vita, si Usaliti. ila upinzani ni hisia. Kwa sasa tuna bunge la chama kimoja, wanazungumza lugh moja, wana mwenyekiti mmoja, wana kila kilichofanana sawa. Akina Lema, Zitto, Heche, Sugu hawapo bungeni tena. Je hili limeua chama pinzani au limewapa sifa? Tunaweza sema, Limewapa sifa, ukiwa mchunguzi wa mitandao watu hufuatilia Lema, Lissu, Mbowe waliwahi sema nini bungeni?

kwa sababu upinzani sio Chama bali upinzani ni hisia. Bungeni hawazungumzi Lugha moja kama mipango walivyoweka, wabunge wanatengeneza makundi mengine mingi ndani ya Bunge. Kuna watu wanaunda timu na sio kuwa ni wabaya, bali ndio hulka za binadamu. Huwezi mzuia mtu kuwa mpinzani sababu upinzani sio chama, sio dhambi, sio uadui. BALI UPINZANI NI HISIA.

Naomba kuwasilisha, unaweza nipata kwa njia ya email kama [hermanwilliam06@gmail.com]
 
Huwezi kuwa mpo kwenye vita afu mwenzako enageuka nyuma, mnajua kitakachomkuta!
 
Upinzani kwenye siasa sio kupinga mwenzio anachofanya ni kuwa mbadala.

Mfano mwenzio anafuata siasa ya ujamaa wewe humpingi katika hjilo lake bali unanadi lako kwa wananchi unasema mimi mlemgo wa ubepari na unautetea huo ubepari wako kwa nguvu zote na yule mwingine anautetea ujamaa wake kwa nguvu zote pasipo kuingiliana mjamaa asianze ohh ubepari mbaya sababu moja mbili tatu hapana yeye akazane kuongelea uzuri wa huo ujamaa wake na bepari akomae kupinga ujamaa ohh mbaya sababu moja mbili tati asimamie hoja yake tu.

Huko nyuma tulishaanza kupata mwelekeo vyama vilikuwa vikijipambanua mfano CHADEMA ilijipambanua wazi kuwa chama kipinga ufisadi na kilipendwa kikaonekana wazi kiko tofauti na CCM UKIULIZA MTU chadema INASIMAMIA NINI kama chama cha upinzani hakuna alikuwa awez kukujibu kuwa kipo pale kuipinga CCM hakuna wanakujibu kinapinga ufisadi.

Kilipomchukua Lowasa kiliyemwita fisadi kikapoteza mwelekeo kikageuka kazi yake kupinga CCM! Kikaishiwa pumzi!

Hadi leo hii mwananchi wa kawaida hata haelewi kazi za vyama vya upinzani ni nini? vimepoteza mwelekeo havieleweki hata agenda yao nini? vinasubiri tukio litokee wadakie na vi press conference koko vyao!! ila ukweli havina agenda.
 
Upinzani kwenye siasa sio kupinga mwenzio anachofanya ni kuwa mbadala

Mfano mwenzio anafuata siasa ya ujamaa wewe humpingi katika hjilo lake bali unanadi lako kwa wananchi unasema mimi mlemgo wa ubepari na unautetea huo ubepari wako kwa nguvu zote na yule mwingine anautetea ujamaa wake kwa nguvu zote pasipo kuingiliana mjamaa asianze ohh ubepari mbaya sababu moja mbili tatu hapana yeye akazane kuongelea uzuri wa huo ujamaa wake na bepari akomae kupinga ujamaa ohh mbaya sababu moja mbili tati asimamie hoja yake tu.

Huko nyuma tulishaanza kupata mwelekeo vyama vilikuwa vikijipambanua mfano CHADEMA ilijipambanua wazi kuwa chama kipinga ufisadi na kilipendwa kikaonekana wazi kiko tofauti na CCM UKIULIZA MTU chadema INASIMAMIA NINI kama chama cha upinzani hakuna alikuwa awez kukujibu kuwa kipo pale kuipinga CCM hakuna wanakujibu kinapinga ufisadi

Kilipomchukua Lowasa kiliyemwita fisadi kikapoteza mwelekeo kikageuka kazi yake kupinga CCM!!! Kikaishiwa pumzi!!

Hadi leo hii mwananchi wa kawaida hata haelewi kazi za vyama vya upinzani ni nini? vimepoteza mwelekeo havieleweki hata agenda yao nini? vinasubiri tukio litokee wadakie na vi press conference koko vyao!! ila ukweli havina agenda
Mwenzio hapo juu amekuchambulia ili umeze tu wewe bado unatapika!? Watu pori still at large!
 
Upinzani lengo lake kuu ni kujenga na si kubomoa kama alivyoaminishwa Magufuli na chama chake, tumeona jinsi nchi ilivyopaa kwa kasi kuanzia 1995 hadi 2015 huku upendo, udugu na amani vikitamalaki bila hisia zozote za chuki, lakini baada ya kutuletea tapeli wa siasa amevuruga kila kitu.
 
Back
Top Bottom