Maana na sababu za kifo kwa mwanadamu

Maana na sababu za kifo kwa mwanadamu

Hello JF Fans.!

Leo ni siku ya Ibada hasa kwa Wakristo walio wengi, lakini bado kuna ambao hatuwezi kufika Kwenye sehemu za Kusanyiko kushiriki na wenzetu katika Ibada kutona na sababu kadha wa kadha.

Nami natumia fursa hii, kuwakumbusha hasa Wakristo wenzangu na kwa Neema za Mungu hata wasio Wakristo wanaweza kupata jambo muhimu la kujifunza siku ya leo.

Ujumbe wangu umejikita juu ya KIFO CHA MWANADAMU.

Tumezoea kusikia pale panapotokea mauti, watu walio wengi hata Wakristo wakisema, Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe. Wengine wameenda mbali zaidi na kusema Yote ni Mapenzi ya Mungu. Hivyo, Vifo vyote vinavyotokea ni kwa sababu Mungu amependa.

Ni kwa muktadha huo, imepelekea kudadisi kwa kina jambo hili hasa kwa Misingi ya BIBLIA.

MAANA YA KIFO.
Mwanadamu ni Roho, Roho inayoishi katika Mwili. Roho ikiwa ndani ya Mwili, Mwanadamu huitwa Kiumbe hai. Roho ikiondoka, Mwanadamu huitwa Kiumbe Mfu. Sasa KIFO ni hali ya Roho kutengana na Mwili.

Hata hivyo, hii ni Tafsiri katika hali ya KIFO pale Roho inapotengana na Mwili.
Kiuhalisia, Mwanadamu ambaye ni Roho hafi, maana Roho haiwezi kufa, ila hujitenga tu na Mwili. Sisi Wanadamu ambao ni Roho, tutafufuliwa hapo baadae siku ya hukumu. Na watakaokuwa wamefanikiwa kuingia Mbinguni wataishi MBINGUNI Milele, watakaokuwa hawajafanikiwa, wao watatupwa kwenye Moto wa Milele.

Ifahamike kuwa, KIFO haikuwa sehemu ya maisha ya Mwanadamu. Mwanadamu alikusudiwa kuishi Milele. Kifo kilifuatia tu baada ya Mwanadamu kuwa muasi kwa Mungu.

Endapo Adam na Eva, wasingetenda makosa hapo awali, Kifo isingekuwa sehemu ya maisha ya Mwanadamu. Hebu tazama maandiko haya.

Mwanzo 3: 3 Lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.
Mwanzo 3: 19,
Kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa, kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.

Mwanzo 3:22 BWANA Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya, na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele.

Kwa ushahidi huo hapo juu, inaonesha wazi kuwa, KIFO ni kama sehemu ya adhabu kwa Mwanadamu. Imekuwa hivyo tangu awali na kuendelea hivyo mpaka YESU alipokuja Duniani, wakati wa Mitume na baada ya Mitume wale wa mwanzo.

Pamoja na kuwa kifo kipo, lakini Mwanadamu aliye mcha Mungu ameahidiwa kuishi miaka mingi zaidi. Tangu enzi za Awali, Wanadamu walio wema waliishi maisha marefu na kufikia Uzee wao.

Hebu tazama baadhi ya umri wa Wanadamu wa Kale katika BIBLIA.

Adam aliishi miaka 930 (Mwanzo 5:5)

Seth mwana wa Adam aliishi miaka 912 (Mwanzo 5:8)

Enosh aliishi miaka 905 (Mwanzo 5:11)

Ibrahimu aliishi miaka 175 (Mwa 27: 7).

Ishmael aliishi miaka 137 ( Mwa 27 : 17)

Isaka aliishi miaka 180 (Mwanzo 35: 28 ).

Siku za kuishi Yakobo zilikuwa 147 (Mwanzo 46 ).

Yusufu alikufa akiwa na umri wa miaka 110 (Mwa 50)

Lakini, inaonesha kuwa, kutokana na maasi aliyokuwa akiyatenda Mwanadamu, ndivyo siku zake zilivyokuwa zikipungua zaidi.

Mwanzo 6:3 "Basi, Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa yeye naye ni nyama; siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Baadae tunaona miaka ikipunguwa na kufikia themanini.
Zab 90: 10 Inasema " Siku za miaka yetu ni miaka sabini, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini.

Lakini, kwamapenzi ya Mungu, bado Mungu anaweza kukuongezea miaka mingi zaidi. Imeandikwa...

"Maana kwa msaada wangu,siku zako zitazidishwa,na miaka ya maisha yako itaongezwa" (Mithali 9: 11).

Imeandikwa pia katika ( Mithali 10: 27 ).
"Kumcha BWANA kwaongeza siku za mtu,Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa"

Swali la Msingi, Je Binadamu kufariki angali akiwa kijana mwenye nguvu ni Mapenzi ya Mungu kweli.? Katika kusoma kwangu BIBLIA, hakuna nilipoona Mungu akiahidi mwanadamu afariki akiwa kijana mwenye nguvu. Kila nilipokuwa nikisoma, nimeona Kifo cha ghafla kikitokea kwa Wanadamu kama tu sehemu ya adhabu kutokana na kukosea kwao. Hivyo hii ni changamoto kwetu kuwa, ukiishi kwa kufuata taratibu za Mungu, Mapenzi ya Mungu ni Mwanadamu kuishi miaka mingi, na iwapo Mwanadamu hatafuata mapenzi ya Mungu atafariki mapema zaidi.

Hebu tuangalie ushahidi hapa chini.
Kwa kuwa,kila andiko lafaa kwa mafundisho na lina pumzi ya BWANA kama ilivyoandikwa katika 2 timotheo 3:16, “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki.

Hivyo basi, siku ya leo ili kufupisha andiko hili, naomba kujikita zaidi katika kitabu cha Mithali.

Kwanza kabisa, mtu mwema hawezi kuwa sawa na mtu asiye mwema. Mtu mwema ana upendeleo zaidi kwa Mungu kuliko asiye mwema. Hebu tazama ushahidi wa maandiko....

"Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA" ( Mithali 12 :2)

Hivyo, hapa chini nimejaribu kubainisha sababu sita(6) za Mwanadamu mwenye haki kuwa na haki ya kuishi siku nyingi na siku chache zaidi kwa Mwanadamu asiye na haki mbele za Mungu.

1. Wasiosikiliza kauli za Mungu.

"Mwanangu,sikiliza na kupokea kauli zangu, na miaka ya maisha yako itakuwa mingi" (Mithali 4: 10 ).

2. Wasio Haki mbele za Mungu.
"Mwenye haki hatapatikana na msiba wowote , Bali wasio haki watajazwa mabaya" 🙁Mithali 12 : 21 ).
3. Wasiosikia Maonyo ya Mungu.
"Maovu yake yeye yatampata mdhalimu, naye atashikwa kwa kamba za dhambi zake.
Atakufa huyo kwa kukosa maonyo.Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake" ( Mithali 5 : 22 - 23).

4. Msiba wa Ghafla ni kwa Waovu tu.
"Mtu muovu,msiba wa ghafula utampata.Ghafula atavunjika,bila njia ya kupona" (Mithali 6 : 12 - 16 ).

5. Wanaomchukia Mungu.
Bali anikosaye hujidharau nafsi yake mwenyewe,na wao wanichukiao hupenda mauti ( Mithali 8: 36).

6. Wasiokuwa na Ufahamu wa Neno la Mungu.
Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu ( Mithali 10: 21).

Lakini, ifahamike kuwa, hapo awali vilitokea Vifo vya Watu wenye haki, bila shaka Mungu alikuwa na kusudi lake. Hata hivyo, kwa maoni yangu, nadhani na wao pia hawakufa wakiwa vijana, bali watu wazima.

Rejea Kifo cha Yohana Mbatizaji, aliyeuwawa kwa kukatwa kichwa. Rejea pia Kifo cha Mtume Stefano aliyeuwawa kwa kupigwa mawe. Ni maoni yangu kuwa, Vifo hivi vya wenye haki vilitokea ili kutimiza maneno ya YESU mwenyewe aliposema "Msiwaogope wale wawezao kuua mwili lakini hawawezi kuua roho; ila mwogopeni yeye ambaye anaweza kuiangamiza roho na mwili katika moto wa Jehenum'' Mathayo 10: 28). Ni maoni yangu pia kuwa, Vifo hivi viliruhusiwa na Mungu kwa Wanadamu waliokuwa katika hali ya kupigania ukweli wa Mungu. Na kwamba, Mungu aliruhusu ili kuonesha kuwa, katika hali ya kulitetea NENO la Mungu, Mwanadamu awe tayari ikibidi hata kwa KIFO. Rejea pia baadhi ya msimamo wa Mtume Paul kuwa alikuwa tayari kufa kwa ajili ya YESU, na rejea pia msimamo wa akina Shadrack, Meshach na Abednego.

HITIMISHO.!
Mimi nami ni nani nipingane na maneno ya Mungu.? anayejiita Mkristo na anapingana na hoja hapo juu, atupe pia Ushahidi wa Kibiblia juu ya hoja zake.

Unaweza kujiuliza, kama Kifo katika hali ya kutokushiba umri hapa Duniani ni kwa ajili ya wasiotii maneno ya Mungu, iweje watoto wadogo wasiojua mema na mabaya wafe.? Hii ni hoja nyingine na inahitaji muda wake mwingine. Leo tuzungumzie Kifo katika muktadha wa wenye kumtii Mungu na Wasiomtii Mungu.

Unaweza pia kujiuliza, mbona flani amefariki akiwa kijana tu na alikuwa na bidii katika Mungu na Mcha Mungu. Jibu lake ni kuwa, ajuaye huyu ni Mcha Mungu ni Mungu mwenyewe, peke yake. Sisi Wanadamu hatuwezi kumjua Mcha Mungu wakweli. Hata mimi nayeandika hapa, ni Mungu pekee ajuaye kama ni Mcha Mungu au la.

Kwa ushahidi huo, huwa siafiki Watu wanaosema kuwa Vifo vya ajali, magonjwa ya kila namna hasa kwa vijana wenye nguvu ni Mapenzi ya Mungu. Hakuna ushahidi popote panapoonesha kuwa Mungu ameahidi kifo kwa kijana Mcha Mungu wa kweli. Bali KIFO haswa kile cha ghafla ni kwa ajili ya wasio mcha Mungu, kutokana na ushahidi wa maandiko hapo juu.

Baada ya kusema hayo, naomba kuwasilisha na karibuni kwa michango zaidi.
Wema hufa mapema huu ni msemo ambao upo!! Lakini mungu ameumba dunia kwa ajili ya binadamu kwa hiyo dunia ni kwaajili yetu na sio kwamba tutaenda kuishi mbinguni maisha ni hapahapa hata baada ya ufufuo au dunia itabaki peke yake?
Adam ndio chanzo cha kila kitu ingebidi basi afe palepale baada ya kula tunda kwa sababu ka ikost dunia mpaka leo dhambi ile imetufikia sisi ni kama hatuna hatia huu ni mfumo ambao ni ngumu kuuepuka kwa iyo ingebidi sisi ndio tuishi miaka elfu tatu hatuna dhambi kubwa kama adam aliyeishi miaka930
 
Wema hufa mapema huu ni msemo ambao upo!!
Huu msemo ni kwa mujibu wa references zipi.? Unaweza kuelezea chanzo cha hiki unachosema ?
Lakini mungu ameumba dunia kwa ajili ya binadamu kwa hiyo dunia ni kwaajili yetu na sio kwamba tutaenda kuishi mbinguni maisha ni hapahapa hata baada ya ufufuo au dunia itabaki peke yake?
Napenda kukufahamisha kuwa, maisha ya hapa Duniani siyo mwisho wa maisha, kwa mujibu wa BIBLIA, kutakuwa na maisha mengine huko Mbinguni. Maisha hayo yatawahusu waliofanikiwa kuishi maisha ya kumcha Mungu hapa Duniani. Rejea Waebrania 9:27, "Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, baada ya kufa hukumu" .....Rejea pia, Mathayo 25: 46 "Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele"
Adam ndio chanzo cha kila kitu ingebidi basi afe palepale baada ya kula tunda kwa sababu ka ikost dunia mpaka leo dhambi ile imetufikia sisi ni kama hatuna hatia huu ni mfumo ambao ni ngumu kuuepuka kwa iyo ingebidi sisi ndio tuishi miaka elfu tatu hatuna dhambi kubwa kama adam aliyeishi miaka930
Hapa usichanganye, Baada ya Adam na Eva kutenda dhambi, ndipo suala la kifo likatokea. Tangu enzi hizo mpaka leo kifo kimefanywa sehemu ya maisha ya Mwanadamu. Rejea Mwanzo 3:22 BWANA Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya, na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele.
 
Nipe mfano mmoja specific wa death at young age ambao haujahusishwa na second law of thermodynamics.

Unafahamu kitu chochote kinacho exist katika time na kutorudi nyuma katika time tayari kiko subject ya second law of thermodynamics?

Kuna mtu gani anayefariki mdogo ambaye hajawahi ku exist katika time?

Unafahamu kwamba context ya second law of thermodynamics si kufa kwa old age tu, kwa sababu mtoto akishakuwa conveived kuanzia sekunde hiyo entropy inaongezeka from zero entropy (ya mtoto ambaye hayupo) kwenda positive entropy ya kiini kikichotungwa?

Kimsingi, chochote kilichopo ndani ya muda kikobsubject to this law.

Sasa unaweza kwenda kuwa specific zaidi jwamba mtoto kagongwa na gari ndiyo maana kafariki, lakini, hata gari kuwapo na mtoto kugingwa ni matokeo ya second law of thermidynamics, kwa sababu motion yoyote ni movement in time, na tushaona chochote kinachotokea in time ni subject to second law of thermodynamics.
ndugu Heart Wood mbona hujajibu hoja za Al-Watan? au anatumia lugha ngumu? mimi nimemuelewa lakini
 
Tatizo linakuja mtu anapoanza kuongelea vitu ambavyo hajavifanyia experiment wala kuvichunguza.

Hapo yeyote anaweza kusema chochote kuhusu chochote na kusiwe na chochote cha kumsimamisha kwa karibu aina yoyote.

Ujinga wa kuamini uwepo wa Mungu unakuja pale Mungu anapoonekana hawezekani kuwepo kwa sababu uongo wa kuwepo kwake umempa nguvu nyingi sana kiasi kwamba zile nguvu alizopewa ili aonekane ni mkuu sana na wa ajabu ndizo hizo hizo zinazoonyesha kwamba hayupo.

Kwa maneno mengine, Mungu alitungwa zamani sana kiasi kwamba kadiri maendeleo ya elimu yanavyokuja ndivyo Mungu huyo anavyozidi kuonekana anapwaya na hayupo.

Mimi nasoma sana habari za Mungu huyu. Nimekuwa nikisoma kwa interest kubwa kwa kadiri miaka 27 iliyopita.

Leo nipo sura ya pili ya "The Islamic Enlightenment:The Struggle Between Faith And Reason". Kitabu kipya kimetoka mwaka huu kwa nia ya kuwaonyesha watu wa Magharibi na dunia kwa ujumla kwamba Waislamu si ISIS tu wanaoua watu, kuna Waislamu wameelimika kitambo sana wanajua Enlightenment ideals kabla hazijafika Ulaya.

Muandishi anajaribu kuweka picha chanya ya Uislamu, lakini inambidi atumie ukweli.

Naambiwa Quran ilikataza/ inakataza kufanya "post mortem". Mtume kasema hata mtu akifa huku kala vito vya thamani akishafariki asipasuliwe. Presumably kwa sababu ya kuheshimu utu wa mtu in the spirit of the time. There are some merits to this when viewed from the context of the period. Lakini kwa mtu atakayesema the Quran is eternal atachekesha, kwa sababu mtu wa leo anatakiwa aelewe umuhimu wa "post mortem" katika kujua chanzo cha kifo ni nini na kujiandaa ili kutorudia vifo hivyo. Sasa kama The Quran is eternal, mbona inakataza kitu ambacho leo dunia inakikubali as a basic fact kama post mortem?

Ukisoma sana hivi vitabu utaona zamani kulikuwa na ujinga sana unakubalika tu.

Watu walikuwa hawaamini kipindupindu ni ugonjwa wa kuambukizwa, wanasema ni majini.

Sasa watu walioishi kabla ya kugunduliwa bacteria unaweza kuwasamehe kuamini kwamba majini yanaeneza magonjwa yanayosababisha vifo.

Leo hii tushajua bacteria anasababisha magonjwa ya kuambukiza, na bado watu wanaamini majini yapo na yanasababisha magonjwa na vifo.

Hawa watu tuwaweke kundi gani?

Na usiniambie hawana elimu, kwa sababu wapo kwenye mtandao na mambo yote yameandikwa kwenye mtandao.

Au kutojua Kiingereza kuna wa cost hivyo na mambo mengi hayajaandikwa Kiswahili basi wanakuwa hawana tofauti na hao watu walioishi zama za ujinga?
Mkuu hakuna zama za ujinga ila ujinga unapatikana kwa kukosekana ukweli,haya ambayo watu wanayagundua sasa yalikuwepo toka zama hizo ulizoita za ujinga ila hayakujulikana. Na hata zama yetu hii kuna mambo mengi tu hatuyajui hivyo hatuwezi kusema tutakuja kuitwa zama za ujinga endapo kizazi kijacho itayagundua yale ambayo kizazi hiki chetu hatukuyajua.
 
Hello JF Fans.!

Leo ni siku ya Ibada hasa kwa Wakristo walio wengi, lakini bado kuna ambao hatuwezi kufika Kwenye sehemu za Kusanyiko kushiriki na wenzetu katika Ibada kutona na sababu kadha wa kadha.

Nami natumia fursa hii, kuwakumbusha hasa Wakristo wenzangu na kwa Neema za Mungu hata wasio Wakristo wanaweza kupata jambo muhimu la kujifunza siku ya leo.

Ujumbe wangu umejikita juu ya KIFO CHA MWANADAMU.

Tumezoea kusikia pale panapotokea mauti, watu walio wengi hata Wakristo wakisema, Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe. Wengine wameenda mbali zaidi na kusema Yote ni Mapenzi ya Mungu. Hivyo, Vifo vyote vinavyotokea ni kwa sababu Mungu amependa.

Ni kwa muktadha huo, imepelekea kudadisi kwa kina jambo hili hasa kwa Misingi ya BIBLIA.

MAANA YA KIFO.
Mwanadamu ni Roho, Roho inayoishi katika Mwili. Roho ikiwa ndani ya Mwili, Mwanadamu huitwa Kiumbe hai. Roho ikiondoka, Mwanadamu huitwa Kiumbe Mfu. Sasa KIFO ni hali ya Roho kutengana na Mwili.

Hata hivyo, hii ni Tafsiri katika hali ya KIFO pale Roho inapotengana na Mwili.
Kiuhalisia, Mwanadamu ambaye ni Roho hafi, maana Roho haiwezi kufa, ila hujitenga tu na Mwili. Sisi Wanadamu ambao ni Roho, tutafufuliwa hapo baadae siku ya hukumu. Na watakaokuwa wamefanikiwa kuingia Mbinguni wataishi MBINGUNI Milele, watakaokuwa hawajafanikiwa, wao watatupwa kwenye Moto wa Milele.

Ifahamike kuwa, KIFO haikuwa sehemu ya maisha ya Mwanadamu. Mwanadamu alikusudiwa kuishi Milele. Kifo kilifuatia tu baada ya Mwanadamu kuwa muasi kwa Mungu.

Endapo Adam na Eva, wasingetenda makosa hapo awali, Kifo isingekuwa sehemu ya maisha ya Mwanadamu. Hebu tazama maandiko haya.

Mwanzo 3: 3 Lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.
Mwanzo 3: 19,
Kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa, kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.

Mwanzo 3:22 BWANA Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya, na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele.

Kwa ushahidi huo hapo juu, inaonesha wazi kuwa, KIFO ni kama sehemu ya adhabu kwa Mwanadamu. Imekuwa hivyo tangu awali na kuendelea hivyo mpaka YESU alipokuja Duniani, wakati wa Mitume na baada ya Mitume wale wa mwanzo.

Pamoja na kuwa kifo kipo, lakini Mwanadamu aliye mcha Mungu ameahidiwa kuishi miaka mingi zaidi. Tangu enzi za Awali, Wanadamu walio wema waliishi maisha marefu na kufikia Uzee wao.

Hebu tazama baadhi ya umri wa Wanadamu wa Kale katika BIBLIA.

Adam aliishi miaka 930 (Mwanzo 5:5)

Seth mwana wa Adam aliishi miaka 912 (Mwanzo 5:8)

Enosh aliishi miaka 905 (Mwanzo 5:11)

Ibrahimu aliishi miaka 175 (Mwa 27: 7).

Ishmael aliishi miaka 137 ( Mwa 27 : 17)

Isaka aliishi miaka 180 (Mwanzo 35: 28 ).

Siku za kuishi Yakobo zilikuwa 147 (Mwanzo 46 ).

Yusufu alikufa akiwa na umri wa miaka 110 (Mwa 50)

Lakini, inaonesha kuwa, kutokana na maasi aliyokuwa akiyatenda Mwanadamu, ndivyo siku zake zilivyokuwa zikipungua zaidi.

Mwanzo 6:3 "Basi, Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa yeye naye ni nyama; siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Baadae tunaona miaka ikipunguwa na kufikia themanini.
Zab 90: 10 Inasema " Siku za miaka yetu ni miaka sabini, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini.

Lakini, kwamapenzi ya Mungu, bado Mungu anaweza kukuongezea miaka mingi zaidi. Imeandikwa...

"Maana kwa msaada wangu,siku zako zitazidishwa,na miaka ya maisha yako itaongezwa" (Mithali 9: 11).

Imeandikwa pia katika ( Mithali 10: 27 ).
"Kumcha BWANA kwaongeza siku za mtu,Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa"

Swali la Msingi, Je Binadamu kufariki angali akiwa kijana mwenye nguvu ni Mapenzi ya Mungu kweli.? Katika kusoma kwangu BIBLIA, hakuna nilipoona Mungu akiahidi mwanadamu afariki akiwa kijana mwenye nguvu. Kila nilipokuwa nikisoma, nimeona Kifo cha ghafla kikitokea kwa Wanadamu kama tu sehemu ya adhabu kutokana na kukosea kwao. Hivyo hii ni changamoto kwetu kuwa, ukiishi kwa kufuata taratibu za Mungu, Mapenzi ya Mungu ni Mwanadamu kuishi miaka mingi, na iwapo Mwanadamu hatafuata mapenzi ya Mungu atafariki mapema zaidi.

Hebu tuangalie ushahidi hapa chini.
Kwa kuwa,kila andiko lafaa kwa mafundisho na lina pumzi ya BWANA kama ilivyoandikwa katika 2 timotheo 3:16, “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki.

Hivyo basi, siku ya leo ili kufupisha andiko hili, naomba kujikita zaidi katika kitabu cha Mithali.

Kwanza kabisa, mtu mwema hawezi kuwa sawa na mtu asiye mwema. Mtu mwema ana upendeleo zaidi kwa Mungu kuliko asiye mwema. Hebu tazama ushahidi wa maandiko....

"Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA" ( Mithali 12 :2)

Hivyo, hapa chini nimejaribu kubainisha sababu sita(6) za Mwanadamu mwenye haki kuwa na haki ya kuishi siku nyingi na siku chache zaidi kwa Mwanadamu asiye na haki mbele za Mungu.

1. Wasiosikiliza kauli za Mungu.

"Mwanangu,sikiliza na kupokea kauli zangu, na miaka ya maisha yako itakuwa mingi" (Mithali 4: 10 ).

2. Wasio Haki mbele za Mungu.
"Mwenye haki hatapatikana na msiba wowote , Bali wasio haki watajazwa mabaya" 🙁Mithali 12 : 21 ).
3. Wasiosikia Maonyo ya Mungu.
"Maovu yake yeye yatampata mdhalimu, naye atashikwa kwa kamba za dhambi zake.
Atakufa huyo kwa kukosa maonyo.Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake" ( Mithali 5 : 22 - 23).

4. Msiba wa Ghafla ni kwa Waovu tu.
"Mtu muovu,msiba wa ghafula utampata.Ghafula atavunjika,bila njia ya kupona" (Mithali 6 : 12 - 16 ).

5. Wanaomchukia Mungu.
Bali anikosaye hujidharau nafsi yake mwenyewe,na wao wanichukiao hupenda mauti ( Mithali 8: 36).

6. Wasiokuwa na Ufahamu wa Neno la Mungu.
Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu ( Mithali 10: 21).

Lakini, ifahamike kuwa, hapo awali vilitokea Vifo vya Watu wenye haki, bila shaka Mungu alikuwa na kusudi lake. Hata hivyo, kwa maoni yangu, nadhani na wao pia hawakufa wakiwa vijana, bali watu wazima.

Rejea Kifo cha Yohana Mbatizaji, aliyeuwawa kwa kukatwa kichwa. Rejea pia Kifo cha Mtume Stefano aliyeuwawa kwa kupigwa mawe. Ni maoni yangu kuwa, Vifo hivi vya wenye haki vilitokea ili kutimiza maneno ya YESU mwenyewe aliposema "Msiwaogope wale wawezao kuua mwili lakini hawawezi kuua roho; ila mwogopeni yeye ambaye anaweza kuiangamiza roho na mwili katika moto wa Jehenum'' Mathayo 10: 28). Ni maoni yangu pia kuwa, Vifo hivi viliruhusiwa na Mungu kwa Wanadamu waliokuwa katika hali ya kupigania ukweli wa Mungu. Na kwamba, Mungu aliruhusu ili kuonesha kuwa, katika hali ya kulitetea NENO la Mungu, Mwanadamu awe tayari ikibidi hata kwa KIFO. Rejea pia baadhi ya msimamo wa Mtume Paul kuwa alikuwa tayari kufa kwa ajili ya YESU, na rejea pia msimamo wa akina Shadrack, Meshach na Abednego.

HITIMISHO.!
Mimi nami ni nani nipingane na maneno ya Mungu.? anayejiita Mkristo na anapingana na hoja hapo juu, atupe pia Ushahidi wa Kibiblia juu ya hoja zake.

Unaweza kujiuliza, kama Kifo katika hali ya kutokushiba umri hapa Duniani ni kwa ajili ya wasiotii maneno ya Mungu, iweje watoto wadogo wasiojua mema na mabaya wafe.? Hii ni hoja nyingine na inahitaji muda wake mwingine. Leo tuzungumzie Kifo katika muktadha wa wenye kumtii Mungu na Wasiomtii Mungu.

Unaweza pia kujiuliza, mbona flani amefariki akiwa kijana tu na alikuwa na bidii katika Mungu na Mcha Mungu. Jibu lake ni kuwa, ajuaye huyu ni Mcha Mungu ni Mungu mwenyewe, peke yake. Sisi Wanadamu hatuwezi kumjua Mcha Mungu wakweli. Hata mimi nayeandika hapa, ni Mungu pekee ajuaye kama ni Mcha Mungu au la.

Kwa ushahidi huo, huwa siafiki Watu wanaosema kuwa Vifo vya ajali, magonjwa ya kila namna hasa kwa vijana wenye nguvu ni Mapenzi ya Mungu. Hakuna ushahidi popote panapoonesha kuwa Mungu ameahidi kifo kwa kijana Mcha Mungu wa kweli. Bali KIFO haswa kile cha ghafla ni kwa ajili ya wasio mcha Mungu, kutokana na ushahidi wa maandiko hapo juu.

Baada ya kusema hayo, naomba kuwasilisha na karibuni kwa michango zaidi.
tupe sababu ya kifo kwa viumbe wengine ambao hawakutenda dhambi
 
Mambo mengine sio yakukaa mnaya tafakari. mtukuja kuwa vichaa. kikubwa endelea na imani ya dini ulio ikuta kwa wazazi wako huku ukitenda mema na ukajiepusha na mabaya. mengine tuyaachage ivo ivo.
 
Mambo mengine sio yakukaa mnaya tafakari. mtukuja kuwa vichaa. kikubwa endelea na imani ya dini ulio ikuta kwa wazazi wako huku ukitenda mema na ukajiepusha na mabaya. mengine tuyaachage ivo ivo.
Usipende kuwaambukiza watu wote uvivu wa kufikiri Kama ulionao wewe.
 
Hello JF Fans.!

Leo ni siku ya Ibada hasa kwa Wakristo walio wengi, lakini bado kuna ambao hatuwezi kufika Kwenye sehemu za Kusanyiko kushiriki na wenzetu katika Ibada kutona na sababu kadha wa kadha.

Nami natumia fursa hii, kuwakumbusha hasa Wakristo wenzangu na kwa Neema za Mungu hata wasio Wakristo wanaweza kupata jambo muhimu la kujifunza siku ya leo.

Ujumbe wangu umejikita juu ya KIFO CHA MWANADAMU.

Tumezoea kusikia pale panapotokea mauti, watu walio wengi hata Wakristo wakisema, Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe. Wengine wameenda mbali zaidi na kusema Yote ni Mapenzi ya Mungu. Hivyo, Vifo vyote vinavyotokea ni kwa sababu Mungu amependa.

Ni kwa muktadha huo, imepelekea kudadisi kwa kina jambo hili hasa kwa Misingi ya BIBLIA.

MAANA YA KIFO.
Mwanadamu ni Roho, Roho inayoishi katika Mwili. Roho ikiwa ndani ya Mwili, Mwanadamu huitwa Kiumbe hai. Roho ikiondoka, Mwanadamu huitwa Kiumbe Mfu. Sasa KIFO ni hali ya Roho kutengana na Mwili.

Hata hivyo, hii ni Tafsiri katika hali ya KIFO pale Roho inapotengana na Mwili.
Kiuhalisia, Mwanadamu ambaye ni Roho hafi, maana Roho haiwezi kufa, ila hujitenga tu na Mwili. Sisi Wanadamu ambao ni Roho, tutafufuliwa hapo baadae siku ya hukumu. Na watakaokuwa wamefanikiwa kuingia Mbinguni wataishi MBINGUNI Milele, watakaokuwa hawajafanikiwa, wao watatupwa kwenye Moto wa Milele.

Ifahamike kuwa, KIFO haikuwa sehemu ya maisha ya Mwanadamu. Mwanadamu alikusudiwa kuishi Milele. Kifo kilifuatia tu baada ya Mwanadamu kuwa muasi kwa Mungu.

Endapo Adam na Eva, wasingetenda makosa hapo awali, Kifo isingekuwa sehemu ya maisha ya Mwanadamu. Hebu tazama maandiko haya.

Mwanzo 3: 3 Lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.
Mwanzo 3: 19,
Kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa, kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.

Mwanzo 3:22 BWANA Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya, na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele.

Kwa ushahidi huo hapo juu, inaonesha wazi kuwa, KIFO ni kama sehemu ya adhabu kwa Mwanadamu. Imekuwa hivyo tangu awali na kuendelea hivyo mpaka YESU alipokuja Duniani, wakati wa Mitume na baada ya Mitume wale wa mwanzo.

Pamoja na kuwa kifo kipo, lakini Mwanadamu aliye mcha Mungu ameahidiwa kuishi miaka mingi zaidi. Tangu enzi za Awali, Wanadamu walio wema waliishi maisha marefu na kufikia Uzee wao.

Hebu tazama baadhi ya umri wa Wanadamu wa Kale katika BIBLIA.

Adam aliishi miaka 930 (Mwanzo 5:5)

Seth mwana wa Adam aliishi miaka 912 (Mwanzo 5:8)

Enosh aliishi miaka 905 (Mwanzo 5:11)

Ibrahimu aliishi miaka 175 (Mwa 27: 7).

Ishmael aliishi miaka 137 ( Mwa 27 : 17)

Isaka aliishi miaka 180 (Mwanzo 35: 28 ).

Siku za kuishi Yakobo zilikuwa 147 (Mwanzo 46 ).

Yusufu alikufa akiwa na umri wa miaka 110 (Mwa 50)

Lakini, inaonesha kuwa, kutokana na maasi aliyokuwa akiyatenda Mwanadamu, ndivyo siku zake zilivyokuwa zikipungua zaidi.

Mwanzo 6:3 "Basi, Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa yeye naye ni nyama; siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Baadae tunaona miaka ikipunguwa na kufikia themanini.
Zab 90: 10 Inasema " Siku za miaka yetu ni miaka sabini, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini.

Lakini, kwamapenzi ya Mungu, bado Mungu anaweza kukuongezea miaka mingi zaidi. Imeandikwa...

"Maana kwa msaada wangu,siku zako zitazidishwa,na miaka ya maisha yako itaongezwa" (Mithali 9: 11).

Imeandikwa pia katika ( Mithali 10: 27 ).
"Kumcha BWANA kwaongeza siku za mtu,Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa"

Swali la Msingi, Je Binadamu kufariki angali akiwa kijana mwenye nguvu ni Mapenzi ya Mungu kweli.? Katika kusoma kwangu BIBLIA, hakuna nilipoona Mungu akiahidi mwanadamu afariki akiwa kijana mwenye nguvu. Kila nilipokuwa nikisoma, nimeona Kifo cha ghafla kikitokea kwa Wanadamu kama tu sehemu ya adhabu kutokana na kukosea kwao. Hivyo hii ni changamoto kwetu kuwa, ukiishi kwa kufuata taratibu za Mungu, Mapenzi ya Mungu ni Mwanadamu kuishi miaka mingi, na iwapo Mwanadamu hatafuata mapenzi ya Mungu atafariki mapema zaidi.

Hebu tuangalie ushahidi hapa chini.
Kwa kuwa,kila andiko lafaa kwa mafundisho na lina pumzi ya BWANA kama ilivyoandikwa katika 2 timotheo 3:16, “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki.

Hivyo basi, siku ya leo ili kufupisha andiko hili, naomba kujikita zaidi katika kitabu cha Mithali.

Kwanza kabisa, mtu mwema hawezi kuwa sawa na mtu asiye mwema. Mtu mwema ana upendeleo zaidi kwa Mungu kuliko asiye mwema. Hebu tazama ushahidi wa maandiko....

"Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA" ( Mithali 12 :2)

Hivyo, hapa chini nimejaribu kubainisha sababu sita(6) za Mwanadamu mwenye haki kuwa na haki ya kuishi siku nyingi na siku chache zaidi kwa Mwanadamu asiye na haki mbele za Mungu.

1. Wasiosikiliza kauli za Mungu.

"Mwanangu,sikiliza na kupokea kauli zangu, na miaka ya maisha yako itakuwa mingi" (Mithali 4: 10 ).

2. Wasio Haki mbele za Mungu.
"Mwenye haki hatapatikana na msiba wowote , Bali wasio haki watajazwa mabaya" 🙁Mithali 12 : 21 ).
3. Wasiosikia Maonyo ya Mungu.
"Maovu yake yeye yatampata mdhalimu, naye atashikwa kwa kamba za dhambi zake.
Atakufa huyo kwa kukosa maonyo.Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake" ( Mithali 5 : 22 - 23).

4. Msiba wa Ghafla ni kwa Waovu tu.
"Mtu muovu,msiba wa ghafula utampata.Ghafula atavunjika,bila njia ya kupona" (Mithali 6 : 12 - 16 ).

5. Wanaomchukia Mungu.
Bali anikosaye hujidharau nafsi yake mwenyewe,na wao wanichukiao hupenda mauti ( Mithali 8: 36).

6. Wasiokuwa na Ufahamu wa Neno la Mungu.
Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu ( Mithali 10: 21).

Lakini, ifahamike kuwa, hapo awali vilitokea Vifo vya Watu wenye haki, bila shaka Mungu alikuwa na kusudi lake. Hata hivyo, kwa maoni yangu, nadhani na wao pia hawakufa wakiwa vijana, bali watu wazima.

Rejea Kifo cha Yohana Mbatizaji, aliyeuwawa kwa kukatwa kichwa. Rejea pia Kifo cha Mtume Stefano aliyeuwawa kwa kupigwa mawe. Ni maoni yangu kuwa, Vifo hivi vya wenye haki vilitokea ili kutimiza maneno ya YESU mwenyewe aliposema "Msiwaogope wale wawezao kuua mwili lakini hawawezi kuua roho; ila mwogopeni yeye ambaye anaweza kuiangamiza roho na mwili katika moto wa Jehenum'' Mathayo 10: 28). Ni maoni yangu pia kuwa, Vifo hivi viliruhusiwa na Mungu kwa Wanadamu waliokuwa katika hali ya kupigania ukweli wa Mungu. Na kwamba, Mungu aliruhusu ili kuonesha kuwa, katika hali ya kulitetea NENO la Mungu, Mwanadamu awe tayari ikibidi hata kwa KIFO. Rejea pia baadhi ya msimamo wa Mtume Paul kuwa alikuwa tayari kufa kwa ajili ya YESU, na rejea pia msimamo wa akina Shadrack, Meshach na Abednego.

HITIMISHO.!
Mimi nami ni nani nipingane na maneno ya Mungu.? anayejiita Mkristo na anapingana na hoja hapo juu, atupe pia Ushahidi wa Kibiblia juu ya hoja zake.

Unaweza kujiuliza, kama Kifo katika hali ya kutokushiba umri hapa Duniani ni kwa ajili ya wasiotii maneno ya Mungu, iweje watoto wadogo wasiojua mema na mabaya wafe.? Hii ni hoja nyingine na inahitaji muda wake mwingine. Leo tuzungumzie Kifo katika muktadha wa wenye kumtii Mungu na Wasiomtii Mungu.

Unaweza pia kujiuliza, mbona flani amefariki akiwa kijana tu na alikuwa na bidii katika Mungu na Mcha Mungu. Jibu lake ni kuwa, ajuaye huyu ni Mcha Mungu ni Mungu mwenyewe, peke yake. Sisi Wanadamu hatuwezi kumjua Mcha Mungu wakweli. Hata mimi nayeandika hapa, ni Mungu pekee ajuaye kama ni Mcha Mungu au la.

Kwa ushahidi huo, huwa siafiki Watu wanaosema kuwa Vifo vya ajali, magonjwa ya kila namna hasa kwa vijana wenye nguvu ni Mapenzi ya Mungu. Hakuna ushahidi popote panapoonesha kuwa Mungu ameahidi kifo kwa kijana Mcha Mungu wa kweli. Bali KIFO haswa kile cha ghafla ni kwa ajili ya wasio mcha Mungu, kutokana na ushahidi wa maandiko hapo juu.

Baada ya kusema hayo, naomba kuwasilisha na karibuni kwa michango zaidi.
Maana ya kifo ni kitu chochote kilicho hai kushindwa kuyamuda mazingira yanayokizunguka.

Kwanza lazima ujue kuwa kifo hakipo kwa watu tu. Kifo ni kwaajili ya kitu chochote kilicho hai. Yaani kitu kilicho hai kikishindwa kuyahimili mazingira kwa wakati huo na kuamua kukubali kushindwa, ndio huitwa kifo.

Mfano samaki ukimtoa kwenye maji ukamuweka nchi kavu. Atashindwa kuyahimili mazingira kwa wakati huo na kupoteza uhai.

By the way, Mimi siamini uwepo wa kuumbwa na huyo Mungu wenu
 
Maana ya kifo ni kitu chochote kilicho hai kushindwa kuyamuda mazingira yanayokizunguka.

Kwanza lazima ujue kuwa kifo hakipo kwa watu tu. Kifo ni kwaajili ya kitu chochote kilicho hai. Yaani kitu kilicho hai kikishindwa kuyahimili mazingira kwa wakati huo na kuamua kukubali kushindwa, ndio huitwa kifo.

Mfano samaki ukimtoa kwenye maji ukamuweka nchi kavu. Atashindwa kuyahimili mazingira kwa wakati huo na kupoteza uhai.

By the way, Mimi siamini uwepo wa kuumbwa na huyo Mungu wenu
Umeielewa mada.? Hapa tunazungumza Kifo kwà Mwanadamu n'a si hao Samaki et al,

By the way, maisha ya viumbe wengine huwezi kuyalinganisha n'a maisha ya Mwanadamu. Vivyo Hivyo, Kifo kwà Mwanadamu si sawa n'a kifo kwa Viumbe wengine. Samaki anaweza kusema uongo ? Anaweza kazini n'a kufanya uasherati ? Anaweza kusaidia Maskini n'a Wajane ?

Kutokukubalina kwako juu ya uwepo wa Mungu haiwezi kuwa Fact ya Mungu kutokuwepo. Umejipa muda kiasi gani kujifunza kuhusu uwepo wa Mungu ?
 
Ukishaanza tu kujiuliza ni kwanini kuna kanuni ya kwenda mbele kwa muda lakini hakuna uwezekano wa kurudisha nyuma muda kitu kinachosababisha watu wasiweze kurekebisha yaliyokwisha kutokea au kifo unaanza kidogo kuelekea kwenye mantiki.....

Kuanza kutafuta sababu ndipo utaanza kuona mambo mengine makubwa kabisa....

Ninauogopa sana ujinga unaoonekana ujinga maana kila tunavyoona tunaendelea ndivyo tunavyoingia machakani....

Yale ambayo "hawataki" yajulikane yangeweza kusaidia sana,tatizo mamlaka wanayo "wao" na hatuwezi kuwanyang\anya kwa sasa....

Wameweza kufanya ujinga uonekane werevu na werevu ukaonekana ujinga.....
 
Usipende kuwaambukiza watu wote uvivu wa kufikiri Kama ulionao wewe.
sasa ukisha fikiri unanufaika na nini? kama siokupoteza muda. wasomi wenyewe na elimu zao hawajawai kukaa wanatafakari kifo, sembuse wew utakuta hapo form4 ikizidi sana6. kakwambia nani mipango ya MUNGU niyakujadiliwa?? acha uboya
 
sasa ukisha fikiri unanufaika na nini? kama siokupoteza muda. wasomi wenyewe na elimu zao hawajawai kukaa wanatafakari kifo, sembuse wew utakuta hapo form4 ikizidi sana6. kakwambia nani mipango ya MUNGU niyakujadiliwa?? acha uboya
1). Herufi ya kila mwanzo wa sentesi na baada ya kituo kikubwa huanza kwa herufi kubwa.
2). Siokupoteza = siyo kupoteza.
3). Hawajawai = hawajawahi
4). Wew = wewe
5). Haiihitaji kuwa msomi kutafakari masuala ya kifo.
 
Nimeipenda, hata Zaburi ya 91 inatoa ahadi ya kuishi miaka mingi kwa sababu ya kumcha Mungu "Kwa kuwa amenijua Jina Langu, kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonesha wokovu Wangu"
 
Back
Top Bottom