Maandalizi ya bima kwa wote yabebwe na huduma bora pasipo kulazimishana kwa kunyimana huduma zingine za kijamii

Maandalizi ya bima kwa wote yabebwe na huduma bora pasipo kulazimishana kwa kunyimana huduma zingine za kijamii

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Kuna mtaalam mmoja huko uingereza aliwahi kusema "Jambo jema likifika kwa wajinga, hugeuka dhahama"

Mfano wa Msemo huu tunaweza kuurejelea kwenye tamthilia ya "The god must be crazy" pale ambapo Chupa iliangushwa kutoka kwenye ndege na kuokotwa na 'Bush man'!

Kwa hali yao ya ujinga, ile chupa badala ya kuhifadhia dawa na maji yao, waliona inafaa kutumika kama nyundo! Waliponda vitu vyao kwa chupa, watoto wa bushman waliitumia chupa kupigiana vichwani!

Mjinga katika jambo jema mara nyingi huharibu maana!
Condom inayotakiwa kuvaliwa sehem za siri kwa mjinga yeye ataivaa kichwani lli masikio asisikie kelele!

MPANGO WA BIMA KWA WOTE ni jambo jema sana kwa wananchi lakini Wasimamizi wa kufanikisha zoezi hili watalifanya liwe kero!

IPO mipango inafanyika BIMA kwa Wote iwe ni LAZIMA!
Kwamba Mwananchi akienda kuomba maji lazima aambatanishe na kadi ya BIMA
Kwamba akitaka TIN namba lazima aambatanishe na kadi ya BIMA
Kwamba akitaka pembejeo wamuombe utambulisho wa BIMA
Kwamba akitaka hati ya kiwanja lazima aambatanishe na kadi ya BIMA

Sehemu pekee ambayo hawatahitaji BIMA ni siku ya kupiga kura ili warudi madarakani!

Hapo unaona wazi kwamba BIMA NI JAMBO JEMA! Lakini linapofika kwa Bushman wa uongozi analigeuza kero!

Kwa utaratibu huo hawaoni kwamba wataongeza rushwa maofisini
Kwa utaratibu huo hawaoni kwamba watawanyima haki za msingi wananchi
Kwa utaratibu huo hawaoni kabisa kwamba itakuwa ni adha kubwa sana kwa wengine!

Sababu kubwa ya kufanya hivyo ETI NI KUTAKA MAKUSANYO MENGI YA WANACHAMA WA BIMA ILI WAPATE KUWAHUDUMIA WACHACHE!

Hii hoja kwa mtu asiye waza sawasawa anaweza kudhani ina mashiko.
Kuna msemo unasema "Usiporidhika kwa kidogo hata ukipata kikubwa ni Yale Yale"

Kama ulikusanya michango kwa watu 10 ukashindwa kumhudumia vyema mtu 1, Je, Utawezaje kuwahudumia watu 10mil kutoka kwenye michango ya watu milion 100?
Jibu ni kwamba huwezi kwasababu hesabu huwa haidanganyi!

USHAURI WANGU
Kama serikali ina mpango wa kuanza kutekeleza bima kwa wote kwanini ISIANZE KUWAHUDUMIA VYEMA WENYE BIMA ili iwe kivutio cha Bima kwa wote?

Kwanini nchi yangu haipendi kutumia njia ya Huduma bora kama kivutio kwa wananchi?

Nashauri Bima kwa wote iwe huru mtu aweze kuingia na kutoka mwenyewe!
NASEMA HAYO KWASABABU
Inchi yetu haina historia ya kufanya vyema, hata ikianza jambo vizuri huwa halidumu!

Tuliona hayo kwenye NIDA, Tuliona hayo kwenye mradi wa mwendokasi, tuliona hayo kwenye Uviko 19, Tuliona hayo kwenye shule za kata, tuliona hayo kwenye miamala ya simu, tuliona hayo kwenye usimamizi Mali na fedha za umma! N.k

Mtakumbuka waziri mkuu alipokemea matumizi mabaya ya "Sheria ya posho makazini maalufu per DM

Ukiambiwa kiasi cha pesa za posho pa DM kwenye vikao vya kupitisha TOZO unaweza kuzimia!

Wanajadili UOZO wanalipana VINONO

Chonde chonde nashauri Bima kwa wote ISIWE LAZIMA KWA KUNYIMANA HUDUMA ZINGINE ZA KIJAMII

Lakini kwasababu watanzia waliowengi tunapenda kusubiri kulalamika, ngoja ipitishwe ndipo tuje kutoa maoni! Sahivi ni kama halituhusu!
 
Bima kwa wote ni mpango mzima! Chukua kingi ili uwahudumie wachache!
Serikali isipofanya jambo kuwa lazima wachache watachangia na itashindwa kuwapa huduma bora!

Ipeni muda serikali ikusanye kodi hata kwa mjeledi ili maendeleo yapatikane!

Bima ikiwa lazima itaongeza kutunisha mfuko haraka kuliko ikiwa Hiari
 
Ngoja tuone...
Watanzania ukiwabembeleza hajiungi! Bora iwe lazima kama kwenye magari mbona fresh tu!
Gari ikiwa haina bima hairuhusiwi kutembea barabarani!

Wewe binadam si ni bora kuliko gari na kwasababu huna plate number ya kupigwa faini dawa yako ni kunyimwa HUDUMA KAMA HUNA BIMA!
Tena waongezee hata ukitaka kuoa kama hamna bima msiruhusiwe kuoana, kama hauna bima hakuna kusafili, kama hauna bima ni marufuku kuzurula usiku!

Sisi mafundi kama hatuna bima msitupe kazi zenu kwa afya zetu
 
Watanzania ukiwabembeleza hajiungi! Bora iwe lazima kama kwenye magari mbona fresh tu!
Gari ikiwa haina bima hairuhusiwi kutembea barabarani!

Wewe binadam si ni bora kuliko gari na kwasababu huna plate number ya kupigwa faini dawa yako ni kunyimwa HUDUMA KAMA HUNA BIMA!
Tena waongezee hata ukitaka kuoa kama hamna bima msiruhusiwe kuoana, kama hauna bima hakuna kusafili, kama hauna bima ni marufuku kuzurula usiku!

Sisi mafundi kama hatuna bima msitupe kazi zenu kwa afya zetu
Unaongea kwa mhemuko! Sijakataa umuhimu wa bima, lakini nimeonyesha umuhimu wa ufanisi wa bima!
Bima siyo kadi, bima ni assurance ya service!
Watu waonyeshwe kwanza ubora wa bima wachague!
Sheria za kurazimishana ni za kikoloni!
Sasa hivi tuko kwenye ulimwengu wa kushawishiana!
Ofa kizuri upate wateja!

Huko vijijini ukiwalazimisha wawe na bima ili uwape huduma ya KIJAMII huoni ni shida?
 
Nadhani Makampuni mbalimbali yaruhusiwe kutoa Bima ya Afya ili kwe na ushindani na hata moja ikiporoka zingine zinaendelea kutoa huduma.
 
Nadhani Makampuni mbalimbali yaruhusiwe kutoa Bima ya Afya ili kwe na ushindani na hata moja ikiporoka nyinginezo zinaendelea kutoa huduma.
Control yake ni ngumu kiasi chake kwa sababu hata sasa hivi kuna Bima nyinginezo pia ukiacha NHIF, issue ni upigaji .. kwa watoa huduma, customer wenyewe anagawa bima yake itumike kwa mtu mwingine n.k, upigaji katika taasisi zenyewe e.g serikali kuu inachukua pesa za mfuko na hairudishi kwa wakati .. hapo mfuko lazima uyumbe tuu.

Au mnasemaje tuongeze tozo special kama REA ili huduma za Afya ziwe bure ???? Tutawezana ???
 
Control yake ni ngumu kiasi chake kwa sababu hata sasa hivi kuna Bima nyinginezo pia ukiacha NHIF, issue ni upigaji .. kwa watoa huduma, customer wenyewe anagawa bima yake itumike kwa mtu mwingine n.k, upigaji katika taasisi zenyewe e.g serikali kuu inachukua pesa za mfuko na hairudishi kwa wakati .. hapo mfuko lazima uyumbe tuu.

Au mnasemaje tuongeze tozo special kama REA ili huduma za Afya ziwe bure ???? Tutawezana ???
Hivi hakuna vyanzo vingine vya pesa zaidi ya TOZO?
 
Bima kwa wote ni mpango mzima! Chukua kingi ili uwahudumie wachache!
Serikali isipofanya jambo kuwa lazima wachache watachangia na itashindwa kuwapa huduma bora!

Ipeni muda serikali ikusanye kodi hata kwa mjeledi ili maendeleo yapatikane!

Bima ikiwa lazima itaongeza kutunisha mfuko haraka kuliko ikiwa Hiari
Mambo yameiva
 
Back
Top Bottom