Maandamamano ya Kenya kuhamia Tanzania?

Maandamamano ya Kenya kuhamia Tanzania?

Naweza kuwa bubu(kutochukua upande) katika maudhui ya maandamano, lakini jambo kubwa na la msingi, ni kwamba ghafla Watanzania tumesahau ya Mwembechai, Zanzibar na kadhalika, kwa kitendo cha polisi kuzuia watu wasiandamane. Hilo ni kosa kubwa sawa na lile la MP's wa CCM wakiongozwa na EL na chambo wao Mudhihir kumfungia Zitto. Polisi wangeruhusu lakini wakahakikisha ulinzi ni mkali. Wangeweza hata kuwazuia wasiende ubalozi wa Kenya na badala yake waishie Jangwani ama popote na wawakilishi wao wapeleke huo waraka kwa ubalozi wa Kenya, lakini kitendo cha kuzuia watu kufanya wanachoamini ni kukiuka HAKI ya Msingi ya KIKATIBA.

Lakini pia maandamano ni kupeleka salaam kwa Wakenya kwamba yanayowakuta tunayaona na ni fundisho kwetu.

Kuhusu kuwa na upande nadhani kwa wapinzani wana haki kabisa kuwa na upande. Kwa serikali si sahihi kuwa na upande kwa sasa japo inawezekana kwa siri wako na Kibaki ama mwenzake Raila (japo ni ndoto).

Suala la utata wa kura, Watanzania hatuwezi kukwepa jumuia ya kimataifa inayoona kuna tatizo na hata Watanzania ukiwamo ubalozi unafahamu hilo.
 
Naweza kuwa bubu(kutochukua upande) katika maudhui ya maandamano, lakini jambo kubwa na la msingi, ni kwamba ghafla Watanzania tumesahau ya Mwembechai, Zanzibar na kadhalika, kwa kitendo cha polisi kuzuia watu wasiandamane. Hilo ni kosa kubwa sawa na lile la MP's wa CCM wakiongozwa na EL na chambo wao Mudhihir kumfungia Zitto. Polisi wangeruhusu lakini wakahakikisha ulinzi ni mkali. Wangeweza hata kuwazuia wasiende ubalozi wa Kenya na badala yake waishie Jangwani ama popote na wawakilishi wao wapeleke huo waraka kwa ubalozi wa Kenya, lakini kitendo cha kuzuia watu kufanya wanachoamini ni kukiuka HAKI ya Msingi ya KIKATIBA.

Lakini pia maandamano ni kupeleka salaam kwa Wakenya kwamba yanayowakuta tunayaona na ni fundisho kwetu.

Kuhusu kuwa na upande nadhani kwa wapinzani wana haki kabisa kuwa na upande. Kwa serikali si sahihi kuwa na upande kwa sasa japo inawezekana kwa siri wako na Kibaki ama mwenzake Raila (japo ni ndoto).

Suala la utata wa kura, Watanzania hatuwezi kukwepa jumuia ya kimataifa inayoona kuna tatizo na hata Watanzania ukiwamo ubalozi unafahamu hilo.

HALISI,

Umeongea mantiki. Nadhani tunahitaji kujielimisha tena na kuelewa zaidi haki zetu za msingi kama raia. Na polisi wanapaswa kujuwa mipaka na wajibu wao katika matukio kama haya. Si kazi yao kuzuia au kuruhusu maandamano. Sheria iko wazi. Kwa nini wanaivunja?

Tukumbuke pia kuwa kuandamana hakutamwondoa Mwai Kibaki Ikulu wala hakutamweka Raila madarakani. Lakini ni haki ya wanaotaka kuandamana kufanya hivyo. Wasioona mantiki ya maandamano wasiwakejeli wanaoiona. Labda ni uelewa wao tofauti wa harakati za kisiasa.

Vile vile, si kazi ya wapinzani wa Tanzania kufanya kazi ya kidiplomasia katika suala hili kama anavyopendekeza Mwanakijiji. Hii ni siasa kama nyingine. Na kwa yaliyotokea Kenya, kama kweli kungekuwa na uwezo, Kibaki si mtu wa kubembeleza. hana ridhaa ya wananchi, bali ya Kivuitu (ambaye naye ameshamgeuka).

Na kama tunavyojua, mazingira ya Kenya sasa yanafanana na ya Zanzibar, ingawa kwa viwango tofauti. Kwa bahati nzuri, matokeo ya uchaguzi wa Kenya yamekataliwa na dunia nzima. Ni Kibaki tu (labda na Masatu wetu humu) anayeamini kwamba 'alishinda kwa uhuru na haki'

Serikali yetu imeogopa kumpongeza Kibaki hadharani, lakini inasemekana Kikwete na Kibaki wameshapongezana 'kwenye simu,' na Kikwete ameshaanza kumpa mbinu za kutengeneza mwafaka kama wa Zanzibar, kusogeza muda. Sasa kuna tatizo gani kama sauti nyingine za Watanzania zitasema wazi kwamba zinalaani yanayotokea Kenya? Ikumbukwe ni kulaani wizi wa kura na ghasia zilizofuata.

Mwisho, kama alivyosema Kitila, wapinzani ni Watanzania kama sisi wengine. Hata kama hatuwataki, tusifumbie macho matatizo ya wazi. Hatuhitaji kuwaunga mkono wapinzani, bali wananchi wasio na hatia wa Kenya ambao sauti zao zinazimwa na mitutu ya bunduki kwa amri ya 'piga ua.'

Zaidi ya hayo, wanayojadili wapinzani kuhusu Kenya yanatuhusu. Yanayotokea Kenya leo pia yanatuhusu. Tusiyapuuze.

P.S. Habari nilizopata sasa hivi kutoka Dar zinasema maandamano yameshindikana kama ya Uhuru Park maana polisi waliwahi na kuwa tishio kwa raia...
 
Ni matumaini yangu kuwa Watanzania watakuwa wamepuuza maandamano hayo ya yawe yameshindwa kwani ni kujaribu kujinufaisha kwa matatizo ya watu wengine. Kama wapinzani watanzania wanafikiri wana influence yoyote, wangefunga safari kwenda Kenya na kuandamana na Wakenya kuonesha mshikamano wao!
 
Ni matumaini yangu kuwa Watanzania watakuwa wamepuuza maandamano hayo ya yawe yameshindwa kwani ni kujaribu kujinufaisha kwa matatizo ya watu wengine. Kama wapinzani watanzania wanafikiri wana influence yoyote, wangefunga safari kwenda Kenya na kuandamana na Wakenya kuonesha mshikamano wao!

Mkuu, waende Kenya kufanya nini ikiwa kuandamana kwao tu unaona tatizo? Haya maandamano yasingekuwa ya wapinzani tu bali ni ya wote wanaopinga kinachoendelea kwa ndugu zetu! Amini usiamini kuna wengine kwenye chama tawala ambao wamesikitishwa na haya.
 
uongo wa baba ni msiba kwa familia
uongo (wizi) wa mwanasiasa ni msiba kwa taifa
 
hilo ndilo kosa walilolifanya.. wangeitisha maandamano ya kuombea Kenya na kuonesha mshikamano na wananchi wote wa Kenya na kujaribu kutoa msaada kwa waliopatwa na majanga, wangehusisha na CCM, taasisi za kidini n.k watu wengi wangeyaona yenye maana. Lakini wao walitaka kujitafutia sifa ya kisiasa kwa kuchagua upande wakati watu wanauana! Hawa wanaowapangia mikakati wakatimwingine wananizingua tu... ndiyo maana kuna kitu kinaitwa Hekima.. siyo kila jambo sahihi lazima lifanywe wakati fulani, wakati mwingine kwa kutumia hekima mambo sahihi yanafanywa tofauti!
 
Tanzania has once again managed to prove itself the police state it is.

Denying Tanzanians of any political persuasion to demonstrate peacefully their solidarity with the people of any country grounded in any political persuasion is a violation of the constitution and an infringement on freedoms of expression, association and movement.

Denying Tanzanians the right to peacefully demonstrate in solidarity with victims of election fraud in neighbouring Kenya is acknowledgement of vote fraud at home, and a measure of preventing this demonstration "genie" from escaping the bottle.The thinking seems to be the people should never taste the power of the statement that a well organized peaceful demonstration has, for who knows,this time they may use it agains Kibaka, next time they may use the same tactics against Kiwete.This could not be allowed.

To paraphrase LKJ

Is Tanzania a police state?
The answe lies, at your own gate
 
Ni matumaini yangu kuwa Watanzania watakuwa wamepuuza maandamano hayo ya yawe yameshindwa kwani ni kujaribu kujinufaisha kwa matatizo ya watu wengine. Kama wapinzani watanzania wanafikiri wana influence yoyote, wangefunga safari kwenda Kenya na kuandamana na Wakenya kuonesha mshikamano wao!


We need to refrain to be judgemental on every issue involving opposition in our country. We have the right to make our opinion about their thoughts and actions but I don't think if it is proper to decide what is good and bad for them.

Mbona wale waliondamana London, Scotland na kwingineko hukuwaambia wasafiri wakaungane na wenzao huko Kenya?
 
wangeitisha maandamano ya kuombea Kenya na kuonesha mshikamano na wananchi wote wa Kenya na kujaribu kutoa msaada kwa waliopatwa na majanga, wangehusisha na CCM, taasisi za kidini n.k watu wengi wangeyaona yenye maana.

By the time wote hawa wamekaa na kukubaliana wangapi wamekufa? Wenye uchungu wangejiunga badala ya kukaa ku'split hairs' kuhusu utaratibu sahihi wa kufuata na kungoja barua za mwaliko! Kwenye msiba hakuna mwaliko.
 
hili siyo suala la msiba... impression ambayo nilikuwa nayo niliposikia habari hii na leo iko confirmed na baadhi ya vyombo vya habari, maandamano yalikuwa na lengo la kumuunga mkono Raila. Ni tofauti na maandamano ya kutaka amani irejee na kuwataka wahusika wote (Raila na Kibaki) wote watumie nafasi na uwezo wao kuhakikisha kuwa amani inarejea Kenya.

Kitendo cha kutaka upinzani wa TAnzania utumike kuhalalisha madai ya Raila haukuwa uamuzi wa busara hasa wakati huu ambapo hali bado haijatulia nchini. Hekima inatusukuma kuamini kuwa badala ya kujitokeza na kujaribu kuchochea madai ya upande mmoja itakuwa ni vizuri kama tungejitokeza na kuzitaja pande zote mbili zikae chini without preconditions na watafute suluhu kwanza kabisa katika kurejesha amani na utulivu na pili kuamua nini cha kufanya ambapo nothing should be off the table.

Sijatoa hukumu bali nimeelezea my own take na kama wao hawakutlia chini na kufikiri kwa makini matokeo ya maamuzi yao hayo Polisi wamesaidia kuonesha ukosefu wa hekima. Siyo kila kitu kinaenda na maandamano!
 
We na wewe bana...kaa huna la kusema bora ukae kimya tu.
 
Wahenga husema 'Kuishi kwingi, uone mengi!'
Yaani siku hizi polisi wa Tanzania ndio wanaowaamulia wanasiasi ni lipi jambo la 'hekima' na kuliruhusu; na kama hawaoni 'hekima' wanazuia?

Wapinzani walikuwa na kila haki ya kuandamana na kumuunga mkono yeyote bila ya hekima ya polisi au CCM kuwaruhusu; mradi tu kama maandamano hayakuwa ya kuleta fujo.

Jamani, mbona sasa tunarudi kinyumenyume hatua nyingi tu?

There must be something wrong somewhere in our system.
 
hahaha.. TAtizo nilikuwa na la kusema nikashindwa kukaa kimya. Ila naona wewe ndiyo huna la kusema.
 
Wahenga husema 'Kuishi kwingi, uone mengi!'
Yaani siku hizi polisi wa Tanzania ndio wanaowaamulia wanasiasi ni lipi jambo la 'hekima' na kuliruhusu; na kama hawaoni 'hekima' wanazuia?

Wapinzani walikuwa na kila haki ya kuandamana na kumuunga mkono yeyote bila ya hekima ya polisi au CCM kuwaruhusu; mradi tu kama maandamano hayakuwa ya kuleta fujo.

Jamani, mbona sasa tunarudi kinyumenyume hatua nyingi tu?

There must be something wrong somewhere in our system.

Kalamu, utaona kuwa sijagusia uwezo wa Polisi kuamua uhalali wa maandamano. Binafsi ningefurahi wawaache waandamane na wananchi wenyewe waamue kuyapa maandamano hayo nguvu au la. HIvyo kupinga kwangu maandamano hayo hakutokani na sababu za Polisi, binafsi naamini kuwa maandamano hayo yalikuwa ill conceived and untimely. Kama unataka kufanya kitu chenye matokeo ni bora upange vizuri na uandae mkakati mzuri. Wao walitaka kufanya maandamano ili waonekana kuwa na "mshikamano" without weighing the political implications of such a move.

At a time as such as this, Kenyans don't need "solidarity walk" and "fiery speeches" that could fan the flame of hatred, revenge and violence. Kenyans need people who would understand the delicate nature of the political atmosphere in Kenya.

While I believe that the opposition has every right to demonstrate for any reason or for no reason, I believe however, in this case, their demonstrations were ill advised.
 
hahaha.. TAtizo nilikuwa na la kusema nikashindwa kukaa kimya. Ila naona wewe ndiyo huna la kusema.

Kwikwikwiwkiiiii...tatizo ningekuwa sina la kusema ningekaa kimya na nisingesema nilichosema kwani asiye na lakusema hukaa kimya.
 
sasa akikaa kimya ni kwa sababu hana la kusema au kwa vile ameshasema? Anayekaa kimya wakati analo la kusema ni mtu ambaye haeleweki kwani anabakia kudhaniwa kuwa ana "lake".. so bora kusema kuliko kimya na kufikiria tu..
 
Haya bana mi ngoja niende zangu Red Lobster...nina ki-date mwenzio....we endelea tu kukaa mtandaoni.....kwikwikwiiiiiii
 
Back
Top Bottom