Maandamanao ya kudai pombe

Maandamanao ya kudai pombe

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
IMG-20240401-WA0026.jpg
Kwa mujibu wa Kamusi ya Karne ya 21 iliyoandikwa na kuchapishwa na LONGHORN, Maana ya Maandamano ni "msururu wa watu wanaotembea kuelekea mahali Fulani kwa lengo maalum."

Kwa umri wangu huu babu yenu nimeshaona maandamano mengi ya kupinga, ya kudai na yakuunga mkono jambo Fulani lakini sijawahi kusikia maandamano ya kudai pombe

ILA ninachoweza kusema ni kuwa umuhimu wa kitu anaujua mtumiaji na hali hiyo ilipelekewa watumiaji wa pombe nchini Marekani kuaandaa maandamano ya kudai pombe

"TUNATAKA POMBEEE"
TUNATAKA TULEWEEEE
TUNATAKA BIAAAA"

Huenda hizo ndio zilikuwa sauti zao walizozitoa kipindi cha maandamano hayo

Kutokana na kukithiri Kwa maovu katika jamii ya wamarekani, baadhi ya viongozi wa dini na umoja wa kina mama walio kwenye harakati waliishauri serikali iliyopo madarakani wafungie pombe (PROHIBITION)

Wao waliamini ulevi umechangia kwa kiasi kikubwa sana kuongeza Rushwa katika jamii, kuongeza uhalifu, wanaume kutelekeza familia zao, na watu kutoheshimu sheria

Mawazo hayo yaliingia moja kwa moja kwenye kichwa cha aliyekuwa Rais wa Marekani kwa wakati huo (1920) Bwana Woodrow Wilson na kusaini muswada wa kuzuia utumiaji wa pombe, usafirishaji wa pombe na uzalishaji WA pombe kuanzia mwaka 1920 na sheria hiyo ilidumu kwa zaidi ya miaka 10...japo sio pombe zote zilifungiwa kuna baadhi ya wine hazikufungiwa kwa sabab ya shughul za kidini na pombe kwa ajil ya tiba

Malengo ya kufungia pombe yalikuwa mazuri lakin kwa bahati mbaya njia walizotumia zilikuwa mbaya zaidi kwa sababu hawakupata kile walichotarajia. Yaani baada ya kufungia walitarajia rushwa ipungue, uhalifu upungue, watu wajielekeze kwenye kufanya mambo ya msingi zaidi

lakini hali haikuwa hivyo mambo yakawa mabaya zaidi uhalifu ukaongezeka, watu wakatafute vilevi vyengine kama cocaine, opium na bangi na watu wakakosa ajira kutokana na viwanda kufungwa, rushwa ikaongezeka maradufu, biashara ya pombe za kienyeji ikashamiri zaidi, maelfu ya watu kufariki, makundi ya kihalifu yakaongezeka zaid kwa sabab wao ndio wakawa wameishikilia biashara hiyo ya pombe na baya Zaidi maandamano ya watu kudai pombe yakazuka

Kupiga tu marufuku ya pombe kulisababishia serikal ipoteze zaidi ya dola za kimarekani bilion 11 huku wakitumia zaid ya dola za kimarekan million 300 kwa ajili ya kuitekeleza sheria hiyo

Tar 5/12/1933 Raisi wa Marekan Bwana Franklin D. Roosevelt aliruhusu pombe

Je, kwa mfano pombe ingezuiliwa hapa Tanzania, ni rafiki yako yupi usingemkosa kwenye maandamano ya kudai pombe?
 
Walevi sijui huwa wanafurahia nini kufakamia mataputapu?
 
Wambea hua mnafaidi nini?Kusengenya?
Unakunywa pombe kisha unaishia kujikojolea kojolea au kulala mitaroni, huwa mnafaidi nini kubugia vitu vichungu hadi mnakunja ndita?
 
Pombe si mbaya imeshauriwa inyweke kwa kiasi.Ukiona pombe imeanza kukuendesha /kukupelekesha hii inatwa pombe mufirisi..Acha mara moja yatakayokukuta kwenye maisha usilaumu mtu...
 
Back
Top Bottom