Maandamano ya CHADEMA Mbeya: Lissu asema hatujamkimbia Makonda kwenye Mdahalo, ni jambazi anatakiwa kuwa gerezani

Maandamano ya CHADEMA Mbeya: Lissu asema hatujamkimbia Makonda kwenye Mdahalo, ni jambazi anatakiwa kuwa gerezani

Lissu ni mwanasheria tena nguli, anapoita Makonda ni jambazi, muuaji inamaana hakuna Sheria inayoweza kutusaidia kumpeleka mahakamani Makonda mpaka Serikali ya CCM itakapoamua yenyewe?

Tunasemaga tumeziambia taasisi za kimataifa kuibana mbavu Tanzania kiasi cha kunyimwa msaada ili tu Mbowe awe huru na demkorasia ya maandamano iruhusiwe, tumeshindwaje kuziomba hizo taasisi za kimataifa kuibana mbavu GOT na uchunguzi huru dhidi ya shambulio Lissu ukafanyika pamoja na mtu tunayemlabel muuaji akahukumiwa.
 
Lucas Mwashambwa ni muda umepita tangu tulipokuarifu kuwa tutakuwa wageni wako, leo tupo Uyole wewe mwenyeji wetu haupo lakini kuna watoto wa shule wametuambia ulionekana kwenye milima inayoitazama Uyole, milima ya Kawetere.
Lucas Mwashambwa wewe ni mdau wetu muhimu sana kwenye siasa za mkoa wa Mbeya ila unatushangaza kuwa kamanda muoga hivyo tofauti na ulivyokuwa kwenye mazoezi wakati mabomu yakilipuliwa wewe ulikuwa unacheza ngoma za kisafwa unatuambi eti unapata midadi! Leo mabomu hayajalipuliwa wewe tayari uko kwenye milima ya Kawetere kwenye barabara iliyo kina kirefu katika Afrika kutoka usawa wa bahari.
Lucas Mwashambwa kwaheri lakini ujumbe wa salamu tunauacha kwa chifu Lyoto, teremka mapema kabla ukungu na baridi havijakukuta.
 
Mpo uyole gani? Mbona siwaoni mkuu?
Screenshot_2024-02-20-14-02-29-1.png
 
mdororo wa maandamano ya mahangaiko waonekana mbeya...
 
Maandamano ya CHADEMA yanaendelea Mbeya sasa hivi


Tundu Lissu:

- Tutaandamana mpaka tutakapopata Katiba mpya, mfumo mpya wa uchaguzi, mpaka tutakapowaondoa madarakani hawa wanaotunyonya.

- Hatuandamani kwa sababu tunataka kujifurahisha, au kufanya mazoezi, tunaandamana sababu tuna hasira na hiyo hasira ndiyo itakayoleta mabadiliko. Tunaandamana kwasababu njia za mazungumzo zimekataliwa, mlango mmoja ukifungwa mingine lazima ifunguliwe kwahiyo njia ya maandamano ni njia ya shinikizo kwa wale waliokataa meza ya mazungumzo.

Akijibu kuhusu madai ya Makonda kuwa CHADEMA ndio waliokataa maridhiano Lissu amesema, Mimi kwenye maridhiano sijauona Makonda nimemuona kinana, Mzanzibari Spika na wengine kwenye maradhiano. Hawa ndio wanaweza kuzungumza kimejadiliwa kitu gani na tumeshindwana kwenye kitu gani, sio Paul Makonda.

Akijibu kuhusu Makonda kusema amewakimbia kwenye Mdahalo Lissu amesema, "Sisi tutakaaje na mhalifu yule, sisi tutakaaje na muuaji yule, kuteka watu nyara, kuvamia vituo vya televisheni kama clouds tutakaaje na mtu anayepaswa kuwekwa gerezani? Na haya ni kwa uthibitisho wa mambo aliyofanya na anayotuhumiwa kuyafanya, ndio maana Wamarekani wamempiga marufuku kwenda Marekani, ni mhalifu, hatuwezi kukaa na jambazi. Watanzania wajue kwamba hatuwezi kukaa na jambazi.

Mwabukusi

Wanatuambia wamebinafsisha bandari lakini ukweli ni kwamba wameziuza. Tutaendelea kupiga kelele na kukataa mikataba hii sababu mikata hii taitendei haki kama Watanganyika.

Swala la bandari halijaisha mahakamani, mahakama ilisema imefungwa mikono, mahakama ilisema sheria imekiukwa, sisi tunataka mikono ifunguliwe na bandari isrudishwe kwa watanganyika. Suala hili halijatulia bado bado kwani tumekata rufaa, hata wao hawajatulia ndio maana wamewadanganya watanzania kuwa wamefanya maerekbisho. Mimi nawauliza kama wamefanya marekebisho watuambie lini IGA ilienda bungeni ambao bunge, ikatambua unquestionable terms zote katika wizara husika, lini zilifika mbele ya baraza la mawaziri na kufanyiwa kazi, lini zilikwenda bungeni na kufanyiwa kazi, na lini zilikwenda Dubai kujadiliwa na kusaniwa? Hawasemi ukweli, jambo la bandari bado sana kuisha.

Maandamano hali vipi huko
 
Hatuandamani kwa sababu tunataka kujifurahisha, au kufanya mazoezi, tunaandamana sababu tuna hasira na hiyo hasira ndiyo itakayoleta mabadiliko. Tunaandamana kwasababu njia za mazungumzo zimekataliwa, mlango mmoja ukifungwa mingine lazima ifunguliwe kwahiyo njia ya maandamano ni njia ya shinikizo kwa wale waliokataa meza ya mazungumzo
Hii inanikumbusha Nyimbo kali ya Peter Tosh ya "Don't Close Door behind you"
 
Kwa kuongelea Kwa uzuri au ubaya,

Unatoa coverage ya maandamano Kwa kujua na kutojua!!
ukweli lazma usemwe wazi,

na hili liko wazi kabisa kutoka mbeya...

wamekataa kubebwa ufala...
 
Maandamano ya CHADEMA yanaendelea Mbeya sasa hivi


Tundu Lissu:

- Tutaandamana mpaka tutakapopata Katiba mpya, mfumo mpya wa uchaguzi, mpaka tutakapowaondoa madarakani hawa wanaotunyonya.

- Hatuandamani kwa sababu tunataka kujifurahisha, au kufanya mazoezi, tunaandamana sababu tuna hasira na hiyo hasira ndiyo itakayoleta mabadiliko. Tunaandamana kwasababu njia za mazungumzo zimekataliwa, mlango mmoja ukifungwa mingine lazima ifunguliwe kwahiyo njia ya maandamano ni njia ya shinikizo kwa wale waliokataa meza ya mazungumzo.

Akijibu kuhusu madai ya Makonda kuwa CHADEMA ndio waliokataa maridhiano Lissu amesema, Mimi kwenye maridhiano sijauona Makonda nimemuona kinana, Mzanzibari Spika na wengine kwenye maradhiano. Hawa ndio wanaweza kuzungumza kimejadiliwa kitu gani na tumeshindwana kwenye kitu gani, sio Paul Makonda.

Akijibu kuhusu Makonda kusema amewakimbia kwenye Mdahalo Lissu amesema, "Sisi tutakaaje na mhalifu yule, sisi tutakaaje na muuaji yule, kuteka watu nyara, kuvamia vituo vya televisheni kama clouds tutakaaje na mtu anayepaswa kuwekwa gerezani? Na haya ni kwa uthibitisho wa mambo aliyofanya na anayotuhumiwa kuyafanya, ndio maana Wamarekani wamempiga marufuku kwenda Marekani, ni mhalifu, hatuwezi kukaa na jambazi. Watanzania wajue kwamba hatuwezi kukaa na jambazi.

Mwabukusi

Wanatuambia wamebinafsisha bandari lakini ukweli ni kwamba wameziuza. Tutaendelea kupiga kelele na kukataa mikataba hii sababu mikata hii taitendei haki kama Watanganyika.

Swala la bandari halijaisha mahakamani, mahakama ilisema imefungwa mikono, mahakama ilisema sheria imekiukwa, sisi tunataka mikono ifunguliwe na bandari isrudishwe kwa watanganyika. Suala hili halijatulia bado bado kwani tumekata rufaa, hata wao hawajatulia ndio maana wamewadanganya watanzania kuwa wamefanya maerekbisho. Mimi nawauliza kama wamefanya marekebisho watuambie lini IGA ilienda bungeni ambao bunge, ikatambua unquestionable terms zote katika wizara husika, lini zilifika mbele ya baraza la mawaziri na kufanyiwa kazi, lini zilikwenda bungeni na kufanyiwa kazi, na lini zilikwenda Dubai kujadiliwa na kusaniwa? Hawasemi ukweli, jambo la bandari bado sana kuisha.

LISSU NI MJINGA KABISA ATENGENEZE EVIDENCE AMPELEKE MAHAKAMANI, SHERIA ZINARUHUSU, OTHERWISE MAKONDA ANAWEZA KUFUNGUA SHAURI LA KUITWA JAMBAZI, LIKIMTAKA LISSU ATHIBITISHE, MAKONDA HII NI LOOP HOLE, BURUZENI MAHAKAMANI MROPOKAJI ILI AUTHIBITISHIE UMMA JUU YA UJAMBAZI ULIONAO, A GOLDEN CHANCE HII. WALAAH.
 
Back
Top Bottom