Mabadiliko Sudan hayakuletwa na wanasiasa. Tanzania tunadhania wapinzani ndio watatuletea mageuzi tukiwa nyuma ya keyboard zetu

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2020
Posts
4,548
Reaction score
11,901
Kule Sudan, Omari Bashir aling'olewa na maandamani ambayo hayakuwa na hayakuanzishwa na vyama vya upinzani.

Wale Gen Z sio wana siasa, ila muziki wao sio wa kitoto.

Sasa Bongo tumekaa nyuma ya Keybord tunangoja wapinzani watutengenezee maisha au watuletee mageuzi, hao wapinzani wakianza kutimukia CCM tunaanza kulalamika.

Sudan wangetegemea Vyama vya Upinzani hadi leo Omari Al bashir angekuwa Madarakani bado.

Kenya na Nguvu za Raila Odinga hajawahi fanikisha movement kama ile ya juzi kati. Ni bahati mbaya Bongo tuko nyuma ya Keybord zetu tunaangojea upinzani tuletee mageuzi.

Tutangoja sana. Vijana wa Kenya sio wajinga.
 
Iko vile Mzee 🙄🤠
 
Go straight......kwamba tufanyeje?
 
Jidanganye, kwenye siasa kila kitu hupangwa,kule Sudan usalama wa Taifa walipambana na jeshi kumlinda Al bashiri,palivyotulia jeshi likapora mamlaka,Leo jeshi linapigana lenyewe kwa lenyewe baada ya kutoafikiana namna ya kula keki
 
Jidanganye, kwenye siasa kila kitu hupangwa,kule Sudan usalama wa Taifa walipambana na jeshi kumlinda Al bashiri,palivyotulia jeshi likapora mamlaka,Leo jeshi linapigana lenyewe kwa lenyewe baada ya kutoafikiana namna ya kula keki
Nani alianzisha movement, achana na end result, unazani hata Gener Z wangeweza kutwaa ikulu ya Kenya? Bila jeshi?
 
Jidanganye, kwenye siasa kila kitu hupangwa,kule Sudan usalama wa Taifa walipambana na jeshi kumlinda Al bashiri,palivyotulia jeshi likapora mamlaka,Leo jeshi linapigana lenyewe kwa lenyewe baada ya kutoafikiana namna ya kula keki
Achana na kinacho endelea sasa hivi,
 
Nani alianzisha movement, achana na end result, unazani hata Gener Z wangeweza kutwaa ikulu ya Kenya? Bila jeshi?
Sudan ni nchi inayoongozwa kijeshi tangu na tangu,political instruments za jeshi zilipenyeza agenda ya maandamano kwa raia wakijua end game itakuaje babu,havitokei tu,yaani polisi,usalama na jeshi washundwe zuwia maandamano?..never!
 
Naunga mkono Hoja! Tusitegee hata kidogo kwa Aina ya wanasiasa hawa Malaya Malaya
 
Uko sahihi. Chimbuko la mageuzi ni wananchi. Wananchi hata leo wakitaka hii hii CCM mbovu iwe safi wanaweza kuigeuza.
 
Sahihi nakuelewa ila Bongo bado
 
GenZ wa Tz wako bize na yafuatayo
1. Mitandao
2. Miziki
3. Michezo (Mpira ndio sana)
4. Mapenzi
5. Upwiru (kutafuta pisi zenye misambwanda mikubwa)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…