Mabadiliko ya mtaala yasisahau kuzifuta kozi ambazo hazitoi ajira kwa wahitimu wa vyuo

Mabadiliko ya mtaala yasisahau kuzifuta kozi ambazo hazitoi ajira kwa wahitimu wa vyuo

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
Kuna utitiri wa kozi zinafundishwa vyuoni zinazosababisha unemployment rate katika taifa letu kukua kwa kasi.

Nabadala yake watoto wanahitimu hizo kozi wanabaki hawana ajira lawama zote zinabaki kwa serikali.

Tupo kwenye mchakato wa kubadili mtaala wetu ili uendane na mazingira yetu. Basi tusisahau kuzifuta kozi hizo. Na kozi zote ambazo hazitoi ajira zinajulikana. Wenzangu watazitaja hapa na hata sekretarieti ya ajira inazifahamu kozi hizo.

Kama kuzivuta haiwezekani tunaweza kuziunganisha na kozi nyingine.

Na bila kusahau udhibiti wa idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa kila mwaka. Kuna baadhi ya vyuo vinachukua idadi kubwa ya wanafunzi kwenye kozi zao. Hili nalo ni tatizo tunakua na idadi kubwa ya wahitimu kuliko uhitaji.

Naomba huu uzi usiondolewe kwenye jukwaa hili la siasa ili tupate kuujadili.
 
Kozi gani mkuu hazina ajira, au nchi ndio haizalishi ajira na kufungua fursa za kujiajiri kwa wa hitimu
Ahsante umeongeza point ya kukuza ajira, hicho ndio nilisema kuhusu kuilaumu serikali.
Zipo kozi kwa kipindi hichi zinatakiwa zifutwe zimeeshakuwa na watu wengi kuliko uhitaji. Na zingine ni sehemu za kozi nyingine.
 
Ahsante umeongeza point ya kukuza ajira, hicho ndio nilisema kuhusu kuilaumu serikali.
Zipo kozi kwa kipindi hichi zinatakiwa zifutwe zimeeshakuwa na watu wengi kuliko uhitaji. Na zingine ni sehemu za kozi nyingine.
Unaona kama kozi gani mkuu ? fahamu Tanzania ni pana sana na haijafikiwa na ujuzi wa kielimu wa aina nyingi.. usipime kuona kozi zimejitolesha kwa kuangalia Dar es Salaam n mikoa mikubwa tu..
 
Lengo la elimu siyo kuajiriwa. Hii mentality tuifute katika zama na kizazi hiki ili kipambane kutafuta fursa za kujiajiri kwa kutumia elimu. Na tuondokane na fikra za kusoma ili kupata ajira.

Mtu asome kozi yoyote ili ayapate maarifa anayoyahitaji ktk kuzipata fursa za kujiajiri.
 
Lengo la elimu siyo kuajiriwa. Hii mentality tuifute katika zama na kizazi hiki ili kipambane kutafuta fursa za kujiajiri kwa kutumia elimu. Na tuondokane na fikra za kusoma ili kupata ajira.

Mtu asome kozi yoyote ili ayapate maarifa anayoyahitaji ktk kuzipata fursa za kujiajiri.
Nafamilia zetu hata mtaji wa genge shida watupe na mikopo ya biashara
 
huwezi tenganisha elimu na kuajiriwa na kujiajiri pia. Sio kila mtu anaweza kujiajiri na sio kila mtu wa kuajiri. Kikubwa kuwa mazingira rafiki kwa wote
Lengo la elimu siyo kuajiriwa. Hii mentality tuifute katika zama na kizazi hiki ili kipambane kutafuta fursa za kujiajiri kwa kutumia elimu. Na tuondokane na fikra za kusoma ili kupata ajira.

Mtu asome kozi yoyote ili ayapate maarifa anayoyahitaji ktk kuzipata fursa za kujiajiri.
 
Back
Top Bottom