Mabalozi wa Tanzania ughaibuni

Mabalozi wa Tanzania ughaibuni

  • Thread starter Thread starter raisi
  • Start date Start date
Mambo ya kidiplomasia hayaendi hivyo Mkuu.Diplomasia kama siasa ni mchezo wa aina yake.
UK hawawezi kususia TZ kwa vile balozi Mwanaidi Maajar ni mwislam.Na kabla alikuwepo balozi Ally Mchumo and all was ok.Kadhalika sidhani kama Tanzania ikiamua kumpeleka Balozi mkristo nchi za kiislam watamsusia... ila kama alivyosema PASCO hapo juu, ni suala la kuona huo ushirikiano wenu utapata faida gani endapo mtapeleka balozi anayeweza "kukubalika all round" - nadhani nimeeleweka.

Kwa kifupi ni kwamba, wakristo huwa hawana complications za culture na misimamo (maishaa kwa ujumla) kwani wamejengwa kwenye misingi ya uhuru wa kuchagua wanachotaka. (Kama BWANA ndiye MUNGU basi mtumikieni huyo na kama Baali ni mungu mfuateni yeye). Tofauti na waislamu ambapo mambo mengi huendeshwa kwa kulazimishwa hata kile usichokipenda wewe. Na kwangu mimi naona sawa kabisa kumpeleka muislamu kuwa balozi katika nchi za kiislamu kuliko mkristo ambaye kwa hakika atateseka sana na mazingira yatakayokuwa yamemzunguka. Muislamu akipelekwa kuwa balozi nchi yoyote isipokuwa hiyo Vatican yenye element za udini it is just ok.
 
Sahihisho. Ubalozi wa Tanzania nchini Ujeremani ndiyo unawakilisha Vatican, siyo Ubalozi wa Tanzania nchini Italia.

Alaa ndio maana miaka ile yule marehumu Yohana Paulo alipowasili uwanja wa ndege tu mtu wa kwanza kumkumbuka alikua marehemu Diria.
 
Tanzania hakuna udini ila kuna kujuana.Sioni sehemu yeyote udini umetumika kwenye hii nchi ya kifisadi ila je wewe ni mwanamtandao, na mtandao wako ni wa nani. haijalishi kabila, rangi, dini, elimu, wala lugha kama wewe ni fisadi mambo kanyaga twende utapelekwa kokote na utakuwa yeyote. kama wewe unamsujudia mkulu mambo ni vilevile. Kikwete na lowasa hawakuwa dini moja. Wala kikwete na membe sio dini moja wala kabila moja.kikwete na Karamag sio kabila moja, Hivyo mimi sioni kama kuna udini kama washika dau wengi wanavyotaka kuleta ila wakati wa kampeni wanatumia vigezo vya dini kupigia kampeni misikitini na makanisani kwa sababu zao na ujinga wetu sisi wapiga kura.

Tusiogope vivuli vyetu bali fikra zetu.
 
Back
Top Bottom