Mabalozi wapya wanolewa

Mabalozi wapya wanolewa

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Mabalozi wapya wanolewa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amefungua rasmi mafunzo kwa mabalozi wapya yenye kuwaongezea uelewa na ujuzi kabla ya kuelekea katika vituo vyao nje ya nchi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam Mhe. Waziri Kombo amewaasa mabalozi hao kutambua kuwa nafasi waliyopata inawafanya wao kuwa wawakilishi wa kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika nchi wanazoenda na hivyo wawe mstari wa mbele kukuza ushirikiano kati ya nchi yao na nchi mwenyeji kwa kuzingatia maslahi ya Taifa.

Waziri Kombo amewataka mabalozi hao kutambua kuwa zipo changamoto katika vituo wanavyoenda na wahakikishe wanaziondoa au kuzipunguza kwa kiwango kikubwa changamoto hizo.

Aidha, Mhe. Waziri Kombo amewahimiza mabalozi hao kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu yao na kuiagiza Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Wizarani kuhakikisha mafunzo hayo yanakuwa ya kina na yagusie intelijensia ya uchumi, diplomasia ya umma na mfumo wa PEPMIS.

Kwa upande wake mtoa mafunzo, Balozi Charles Sanga amewaeleza Mabalozi hao wapya kufanya rejea katika nyaraka zote muhimu ikiwemo Waraka wa Rais wa mwaka 1964 ili kuelewa namna ya kuwasiliana na mabalozi wengine.

Pia amewasisitiza wenza wa mabalozi wakawe washauri wazuri kwa wenza wao wanapotekeleza majukumu yao katika vituo walivyopangiwa.
 

Attachments

  • FB_IMG_1741626299930.jpg
    FB_IMG_1741626299930.jpg
    21.1 KB · Views: 2
  • FB_IMG_1741626295171.jpg
    FB_IMG_1741626295171.jpg
    33.7 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626297747.jpg
    FB_IMG_1741626297747.jpg
    32.5 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626308370.jpg
    FB_IMG_1741626308370.jpg
    28.6 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626310735.jpg
    FB_IMG_1741626310735.jpg
    23 KB · Views: 2
  • FB_IMG_1741626320790.jpg
    FB_IMG_1741626320790.jpg
    24.7 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626318577.jpg
    FB_IMG_1741626318577.jpg
    37 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626315949.jpg
    FB_IMG_1741626315949.jpg
    15.9 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626304688.jpg
    FB_IMG_1741626304688.jpg
    29.1 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626302157.jpg
    FB_IMG_1741626302157.jpg
    36.2 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626313392.jpg
    FB_IMG_1741626313392.jpg
    27.2 KB · Views: 1
  • FB_IMG_1741626322760.jpg
    FB_IMG_1741626322760.jpg
    50.7 KB · Views: 1
Mabalozi wapya wanolewa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amefungua rasmi mafunzo kwa mabalozi wapya yenye kuwaongezea uelewa na ujuzi kabla ya kuelekea katika vituo vyao nje ya nchi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam Mhe. Waziri Kombo amewaasa mabalozi hao kutambua kuwa nafasi waliyopata inawafanya wao kuwa wawakilishi wa kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika nchi wanazoenda na hivyo wawe mstari wa mbele kukuza ushirikiano kati ya nchi yao na nchi mwenyeji kwa kuzingatia maslahi ya Taifa.

Waziri Kombo amewataka mabalozi hao kutambua kuwa zipo changamoto katika vituo wanavyoenda na wahakikishe wanaziondoa au kuzipunguza kwa kiwango kikubwa changamoto hizo.

Aidha, Mhe. Waziri Kombo amewahimiza mabalozi hao kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu yao na kuiagiza Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Wizarani kuhakikisha mafunzo hayo yanakuwa ya kina na yagusie intelijensia ya uchumi, diplomasia ya umma na mfumo wa PEPMIS.

Kwa upande wake mtoa mafunzo, Balozi Charles Sanga amewaeleza Mabalozi hao wapya kufanya rejea katika nyaraka zote muhimu ikiwemo Waraka wa Rais wa mwaka 1964 ili kuelewa namna ya kuwasiliana na mabalozi wengine.

Pia amewasisitiza wenza wa mabalozi wakawe washauri wazuri kwa wenza wao wanapotekeleza majukumu yao katika vituo walivyopangiwa.
..wangeweza kupeleka makao makuu musoma labda wangeridhika
 
Back
Top Bottom