Mabasi 38 ya kampuni ya New Force yapigwa stop na LATRA kusafiri usiku, kuanza huduma saa 12 asubuhi

Mabasi 38 ya kampuni ya New Force yapigwa stop na LATRA kusafiri usiku, kuanza huduma saa 12 asubuhi

Kampuni ya usafirishaji abiria ya NEW FORCE yapigwa stop leo kuendelea na safari zake baada ya kupata ajali mfululizo na kuthibitika kuwa wengi wa madereva wao hawajathibitishwa na mamlaka hiyo.

=======

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imesitisha ratiba ya mabasi 38 ya New Force, kufuatia mfululizo wa ajali za mabasi hayo ambapo hadi sasa takribani mabasi matano ya kampuni hiyo yamepata ajali.

Mkurugenzi Mkuu wa LATRA CPA Habibu Suluo amesema uchunguzi unaonesha kuwa Madereva wake hawajathibitishwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini.

CHANZO: EA Radio
Hatua nzuri,hata hivyo wamechelewa sana,hii kitu inahusu uhai wa watu,mmesubiri mpaka afanye ajali 5 ndio mchukue hatua,inasikitisha sana kwa kweli...
 
New force mwamba wa Kusini ngoja kampuni zingine zipate abiria nazo
 
Hatua nzuri,hata hivyo wamechelewa sana,hii kitu inahusu uhai wa watu,mmesubiri mpaka afanye ajali 5 ndio mchukue hatua,inasikitisdha sana kwa kweli...
Ya kwanza Huwa ni kosa zaidi ya hapo Huwa ni makusudi
 
Ukipigwa stop inatakiwa usimamishiwe Kila kitu kuanzia marejesho ya Kodi,nssf nk
 
Kampuni ya usafirishaji abiria ya NEW FORCE yapigwa stop leo kuendelea na safari zake baada ya kupata ajali mfululizo na kuthibitika kuwa wengi wa madereva wao hawajathibitishwa na mamlaka hiyo.

=======

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imesitisha ratiba ya mabasi 38 ya New Force, kufuatia mfululizo wa ajali za mabasi hayo ambapo hadi sasa takribani mabasi matano ya kampuni hiyo yamepata ajali.

Mkurugenzi Mkuu wa LATRA CPA Habibu Suluo amesema uchunguzi unaonesha kuwa Madereva wake hawajathibitishwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini.

CHANZO: EA Radio
Wanyang'anywe leseni kabisa
 
Basi ilo ambalo kwasasa ni kinara wa ajali limefungiwa kutoa huduma kuanzia saa 9-11 alfajiri badala yake litakua linatoka saa 12 asbh kwa uangalizi na wamepewa onyo la mwisho kabla hawajafungiwa leseni zao
 
Kampuni ya usafirishaji abiria ya NEW FORCE yapigwa stop leo kuendelea na safari zake baada ya kupata ajali mfululizo na kuthibitika kuwa wengi wa madereva wao hawajathibitishwa na mamlaka hiyo.

=======

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imefuta ratiba za saa 9.00 alfajiri na saa 11.00 alfajiri kwa mabasi 38 ya New Force Enteprises, ambapo mabasi 10 ni yale yanayoanza safari saa 9.00 alfajiri na mabasi 28 yanayoanza safari saa 11.00 alfajiri, kufuatia mfululizo wa ajali za mabasi hayo ambapo ndani ya Wiki nne (Kati ya June 06 - July 02,2023) mabasi matano yamepata ajali.

“Kuanzia tarehe 5 Julai, 2023, mabasi haya 38 yatafanya safari zake kuanzia saa 12.00 asubuhi na kuendelea hii ni kwakuwa uchunguzi wa awali wa LATRA ulibaini kuwepo kwa uvunjaji wa makusudi wa kanuni hususani kutumia ratiba za saa 9.00 alfajiri na saa 11.00 alfajiri bila dereva kuwa amethibitishwa na LATRA na pengine dereva kuwa amethibitishwa lakini hatumii mfumo wa utambuzi wa dereva (i-button) anapoendesha basi”

“Kanuni zinamtaka dereva anayeendesha basi la abiria kutumia kifaa cha utambuzi ili tuweze kuwafuatilia kwa mfumo wetu wa Kufuatilia Mwenendo wa Mabasi (VTS) yanapokuwa safarini lakini uchunguzi tulioufanya kwenye magari haya yaliyopata ajali tumebaini ukiukwaji wa sharti hilo kwa mabasi ya Kampuni ya New Force Enterprises”

“Kutokana na ukiukwaji huu, Mamlaka imeshindwa kuwatambua madereva waliokuwa wanaendesha mabasi haya ili kuweza kuwachukulia hatua au kupeleka taarifa zao Jeshi la Polisi - Kikosi cha Usalama Barabarani ili wawajibishwe kwa mujibu wa Sheria za Usalama Barabarani, pia tumebaini ukiukwaji wa ratiba za mabasi ambayo hayakuwa kwenye ratiba ya saa 9.00 alfajiri na saa 11.00 alfajiri kwa kufanya safari muda huo bila kibali cha LATRA”

Chanzo: Millard Ayo
Hivi serikali wakati inaruhusu hizi safari za usiku hawakujua kama yatatokea haya,mwanzo kilichosababisha kupiga marufuku safari za usiku zilikuwa ajari ni miaka ya tisini kabla ya elfu mbili,nashangaa wanajitoa ufahamu wanaruhusu tena wakati madreva ni hawa wenye kuendesha hovyo Kwa Kasi kama wanavuta bangi,na usiku wanaijua hakuna trafiki wa kuwauliza,kifupi ngozi nyeusi haiwezi kujiendesha mpaka isimamiwe,utashangaa watu wanagongwa magari tena kwenye zebra mchana kweupe sembuse usiku.
 
Back
Top Bottom