Mabasi ya Abood yamejaa mende

Mabasi ya Abood yamejaa mende

Malinyingi

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2013
Posts
864
Reaction score
164
Jana nilipata safari Fupi ya Kwenda na kurudi morogoro, nikiamini kuwa usafiri pekee wa uhakika Kwenda na kurudi morogoro ni Abood bus service. Wakati wa Kwenda sikushangaa sana niliona mende Kama wa tatu hivi wale wa dogo wa dogo nikiamini niuchafu wa kawaida tena labda kuna mzigo uliopandishwa ukiwa na mende hao.
nilikuja kustaajabu wakati narudi kutoka Moro kuja Dar kwa Basi lingine la kampuni hiyo hiyo nalo lina mende wengi zaidi ya wale waliokua kwenye basi lile la awali.
najiuliza inakuwaje wamiliki wa mabasi haya wanashindwa kuyafanyia usafi wakati wanapata abiria wengi tu



 
Wao wako kibiashara mabasi mengi huwa ni machafu kupindukia yanaweza kata mwezi hayajaoshwa, wacho fanya ni kuosha bodi tu tena kwa nje,
 
Wao wako kibiashara mabasi mengi huwa ni machafu kupindukia yanaweza kata mwezi hayajaoshwa, wacho fanya ni kuosha bodi tu tena kwa nje,

Hapana blaza, Abood yamezidi!!! Niliacha kupanda long time hasa yale ya kutoka mkoa hadi mkoa!! Kuna abood hizo utasema zinaenda vijijni, siti mabenchi, speaker ni masufuria basi chafu kama nini!! nilivaa shati jeupe lilifika halitamaniki utasema nimetoka Mtwara enzi zileeeeee......!!! Jamaa ajiangalie upya basi zake hovyo sana
 
Back
Top Bottom