Mabasi yamegeuka kuwa mabanda ya machinjio

Mabasi yamegeuka kuwa mabanda ya machinjio

Mkanganyiko kukanganya

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2022
Posts
1,204
Reaction score
5,053
Haya mabasi yamegeuka kuwa mabanda ya machinjio na kuwapa abiria ulemavu wa maisha.

Hawa madereva ni sikio la kufa daima na sio mambo ya kusadikika, wenyewe tunayaona huko road wanavyoyafyatua mabasi. Mfano:

~ Ukiwa na kagari kadogo utaletewa basi hapo nyuma honi zote, taa kali, kama muoga utapagawa presha au uingie mtaroni.

~ Wao wanajua ku overtake popote ni haki yao, kama unakuja kwa mbele hawajali hasa ukiwa na kagari kadogo, itabidi kuingia porini kuepuka kifo.

Huko maporini mwendo wao ni roho kiganjani, dereva ni mwendo wa kusimamia tu, kwao ni marufuku kubaki nyuma ya gari lingine hasa aone bus mwenzie mbele; yaani hatameza mate mpaka ampite 😂😂.

Mabasi ya wilayani utakuta juu limebeba kilemba cha mizigo mizito, ndani abiria, ilihali barabara ni mbovu na ni milima, bado gali linapigwa mwendo hatari.

IGP na Rais wameshawaonya mara kadhaa ila wanaviburi na dharau na mara nyingi ajali ikitokea madereva hawafi, wanasepa😂😂.

Ingefaa ifike mahala tupate wanaume wachache kutoka JWTZ waratibu zoezi hili angalau kwa miezi sita tu, then tuone matokeo.
 
Uzembe wa madereva.
Ubovu wa barabara.
Poor maintenance
 
Haya mabasi yamegeuka kuwa mabanda ya machinjio na kuwapa abiria ulemavu wa maisha

Hawa madereva ni sikio la kufa daima na sio mambo ya kusadikika wenyewe tunayaona huko road wanavyo yafyatua mabasi, mfano:

.Ukiwa na kagari kadogo utaletewa basi hapo nyuma honi zote taa kali km muoga utapagawa presha au uingie mtaroni

.Wao wanajua kuovatek popote ni haki yao kama unakuja kwa mbele hawajali hasa ukiwa na kagari kadogo itabidi kuingia porini kuepuka kifo
.Huko maporini mwendo wao ni roho kiganjani, dreva ni mwendo wa kusmamia tu, kwao ni marufuku kubaki nyuma ya gari lingine hasa aone bus mwenzie mbele yaan hata meza mate mpk ampite [emoji23][emoji23]

.Mabasi ya wilayani utakuta juu limebeba kilemba cha mizigo mizito ndani abiria ilihali barabara ni mbovu na ni milima bado gali linapigwa mwendo hatari

IGP na Mh Rais wameshawaonya mara kadhaa ila wanaviburi na dharau na mara nyingi ajali ikitokea madreva hawafi wanasepa[emoji23][emoji23]

Ingefaa ifike mahala tupate wanaume wachache kutoka JWTZ waratibu zoezi hili angalau kwa miezi sita tu then tuone matokeo
tatizo awapigwi faini hata boda boda bajaji ni hatari sana taizo rushwa madereva walishwa zoeshwa rushwa
 
Imenipa shida sana kuuelewa uzi wake jamaa,maana kichwa cha habari na habari yenyewe haviendani kabisa
 
Sijui ni mimi peke yangu ninayeona heading na content zinatofautiana !
mimi nilicho gundua huyu jamaa ame tumia hiyo headline ili kuwa vuta watu watamani kusoma habari kamili na bila kupepesa macho hata mimi nime vutwa kusoma ili nijue mabasi yame geukaje mabanda ya video ila nilipo soma nime elewa jamaa alikuwa anataka kuki fikisha kwa wa somaji
 
Sisi ndio abiria tusichoke kuongea mpaka madereva wabadili tabia
 
Back
Top Bottom