"Mabeberu" Marekani waanza mbinyo kwa Tanzania. Washawishi Serikali yao na Jumuiya ya Kimataifa kuanza vikwazo na kukata misaada

Tanzania iliweza kuishawishi jumuiya ya kimataifa kuipa China "kura ya VETO" kwenye vikao vya UN wakati miaka hiyo Tanzania ikiwa bado nchi changa kabisa! Sembuse muda huu!?
Tanzania hiyo changa ndo iliyokuwa na ushawishi mkubwa hapa Africa na duniani kama unaijua Historia ya nchi Hii vizuri

Kipindi cha Nyerere siasa ndo ilikuwa jambo kubwa duniani kutokana na wave iliyokuwepo. Dunia ya sasa ni teknolojia na uwezo wa kiuchumi zaidi ambayo kwa Tanzania hatuna.
Hiyo Tanzania changa ilikuwa na uwezo wa kusema na ikasikika kuliko hiyo Tanzania iliyokomaa
 
"Mabeberu" wanatetea umma wa raia wanyonge wasio na sauti dhidi ya serikali "yao"
dah!!! inasikitisha sana..karne ya 21 hii waafrika bado hatuna uwezo wa kujitetea wenyewe mpaka tutetewe tena na wale wale waliotutawala. ni kama hakukuwa na haja ya kumwondoa mkoloni mweupe maana kikundi kidogo cha weusi wenzetu wamegeuka kuwa wakoloni weusi wanatufanyia ubaya ule ule tuliyofanyiwa na mkoloni mweupe. ni heri haya ufanyiwe na mkoloni mweupe kuliko ndugu zetu weusi. The United nations please rescue Tanzania democracy before its too late...dont wait until innocent life is compromised before you act. we are being oppressed.
 
Nchi hii itageuka kuwa Zimbabwe very soon. Stay tuned!
 
kwa hiyo unaitunishia msuli jumuiya ya kimataifa?!!! "Tansania" hii hii au nyingine?!!! ahahaaaa..aya ngoja tuone.
 
Labda bajeti yao imebana kutokana na covid, ila ni aibu kwa nchi kubwa kukiri. Huenda hapa ni kama wamepata kaupenyo ka kutua mzigo mmojawapo.
 
hivi bwana Bujibuji ni kwanini akili zenu zinawaza sana misaada?
Serikali ukisha iwekea ukusanyaji mzuri wa mapato kila kitu kinakwenda vizuri bila wasiwasi. Embu tubasirikane tuache kuwaza misaada.
mkuu kwan mpaka sasa bajeti yetu inajitegemea kwa asilimia ngapi?
 
Mkuu unauelewa walau kidogo wa siasa za vyama vingi ?
 
n
Kwa mfumo wa US itabidi uwe makini sana kwa sauti unazosikia. Kuna sauti nyingi mno na wengine mission yao ni kutoa tu sauti tofauti lakini wako United in actions. Inahitaji akili za exta miles kujua mahusiano na US yanavyofanya kazi.
nimewahi kufanya kaz na kuishi na wamerekani. hawa jamaa huwa hawapayuki. akikutamkia neno moja tu lipime sana. huwa wanamaanisha wanachokisema na plan zao siyo za miaka mitano mitano za kuiba kura..wanafikiria miaka mia moja, miaka mbili nk ijayo.
 

Tusidanganyane mambo ya marekani inapower ilikuwa wakati ule. Siku hizi Iran na North Korea wana wavimbia.

Kuna balance of power kati ya USA na China. Wazungu wakiongozwa na USA hawawezi kukubali kumuachia Mchina mwenyewe Tanzania. Itakuwa ni kumziria nguruwe shamba la mihogo. Lakini ushawishi wa Tanzania kwa Afrika hasa kusini mwa jangwa la sahara na kati wazungu hawatakubali waupoteze kwa China Kirahisi.

Sera za diplomasia yetu ya nje ni kucheza na sifa Tanzania ilizonazo ambazo huzipati kwa wengine. USA haina chake kwanza kuondoka tu kwa Trump tarajia mabadiliko makubwa ya sera za na mahusiano ya nje za USA
 
Ni kweli USA hana nguvu ila walipotaka kuondoa misaada yao kwenye shirika la afya duniani kipindi cha Corona, Dunia ilitetemeka japo kuna China na Urusi.. Unafikiria ni kwa nini ???...

OK nakubali uliyosema, ngoja niishie hapa
 
Mkuu unauelewa walau kidogo wa siasa za vyama vingi ?
Mkuu, ingependeza zaidi kama ungenijibu swali nililouliza hapo juu kwanza. Ukimaliza kunijibu, na mm nitakujibu swali uliloniuliza hapo.
 
Mkuu, ingependeza zaidi kama ungenijibu swali nililouliza hapo juu kwanza. Ukimaliza kunijibu, na mm nitakujibu swali uliloniuliza hapo.
Nilichotaka kukujibu inategemea majibu yako kwenye swali nililokuuliza ?
 
Hakuna vyama vya upinzani bungeni.
 
Hata vibaraka wa MUGABE walikuwa wakiongea kwa nyodo hivo hivo hadi pale mfumuko wa Bei ulipowashangaza
 
Naomba kuuliza, hivi serikali ikabanwa na umoja wa mataifa watakaothirika zaidi ni viongozi walioko madarakani au sie wanainchi wa kawaida?, Ukipata jibu then hakuna haja ya kuchekelea njaa na shida zinakuja wakumba wanainchi wa kawaida ukiwemo mleta uzi
 
I dont see anything strange. We all struggle. Na kama kuna mtu alitegemea kuwa salama yetu ni pesa ya msaada alibugi man. Covid has brought into the world unsolved equation

Si nyie JIWE kawaaminisha kuwa kwa kusali nchi yenu imeshinda CORONA !!! Hii ni nchi ya ABUNUWASI; toka lini ibada ikawa ndio dawa ya virus? Wananchi wakumbuke usemi wa MKWERE " Za kuambiwa changanya na za kwako" la sivyo wananchi watapukutika!!! Corona ipo Tanzania na wananchi hawana budi kuchukua tahadhari!!!
 
Ndio vizuri hiyo ndio furaha yetu itayopoza machungu ya kuibiwa kura zetu kuutafuta uhuru kuna gharama zake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…