"Mabeberu" Marekani waanza mbinyo kwa Tanzania. Washawishi Serikali yao na Jumuiya ya Kimataifa kuanza vikwazo na kukata misaada

Hangaikia maisha yako, kwa mfano ukiwekewa vikwazo unapata nini? Machafuko yakitokea usalama wako uko wapi? Hao mabeberu watapoteza nini? Shida zote ni kwako unayepumua shida, unayekohoa shida na ujinga kwakushindwa kujishughulisha na badala yake umekalia kuandika kuichafua Serikarikali
 
Kwani Tanzania bado inategemea misaada kama wengi wanavyofikiria. Leteni stats basi tuone kama kweli Tanzania haiwezi ku-tick. Hatuwezi kuwa taifa la omba omba.

 
Mkuu kuna siku umelala njaa au umeenda hospitali ukashindwa kutibiwa au umeenda chuo ukakosa kusoma sababu USA wamepunguza misaada?wao nao wana kitimu timu chao acha chuki fanya kazi, Lissu na timu yake hawatakuletea ugali mezani ,kama njaa ni yako na mkeo.
 
Hakuna vyama vya upinzani bungeni.
Sizungumzii bunge la sasa hivi lenye kijani.
Rejea kwenye post, niliandika hivi:


Asante kwa kunielewesha maana ya demokrasia. Bado nina swali mwaaalimu japo swali langu halihusiani na bunge la sasa hivi Tanzania .

Swali ni hili, kama maamuzi ya nchi za kidemokrasia yanafanywa na wananchi na sio mtu mmoja na vibaraka zake, sasa inakuaje kule bungeni kuna vyama vya upinzani na chama tawala, ilihali vyama vya upinzani ni wananchi na chama tawala ni wananchi??

Mbona chama tawala ndio kinafanya maamuzi ya mwisho huko bungeni hata kama wabunge wa vyama vya upinzani wamepinga hoja?? Sasa demokrasia iko wapi hapo??
 
Nilichotaka kukujibu inategemea majibu yako kwenye swali nililokuuliza ?
Sawa mkuu. Kwa uelewa wangu mm, siasa ya mfumo wa vyama vingi ni aina ya demokrasia ya ushindani wa kisiasa ili kuleta maendeleo katika nchi. Pia ni pale ambapo nchi inakuwa na vyama vingi vya kisiasa na kila chama kinakua na sera zake. Chama tawala huchaguliwa na wananchi kwa kutumia sanduku la kura.

Pia nimeelimishwa, demokrasia means “hatma na maamuzi ya nchi uamuliwa na wananchi na sio mtu mmoja na vibaraka zake”

Sasa naomba unijibu maswali niliyoyauliza hapo👇🏾.
Kama maamuzi ya nchi za kidemokrasia yanafanywa na wananchi na sio mtu mmoja na vibaraka zake, sasa inakuaje kule bungeni kuna vyama vya upinzani na chama tawala, ilihali vyama vya upinzani ni wananchi na chama tawala ni wananchi!!

Inakuaje chama tawala ndio kinafanya maamuzi ya mwisho huko bungeni hata kama wabunge wa vyama vya upinzani wamepinga hoja?? Kwani, hawa waliopinga hoja si ni wananchi pia?? Sasa demokrasia iko wapi hapo??
Majibu tafadhali.
 
Kwahiyo mkuu bora Saudia Arabia kuna demokrasia kuliko bongo?
Inategemea wewe unaelewaje demokrasia ni kitu gani
Kwa ujumla Saudi Arabia na nchi zote zenye utajiri wa mafuta watu wake hawana shida ya maisha kabisa na wala hawajihusishi na siasa kabisa
 
Duh! Mpaka nimecheka kama huu ndio uchambuzi wa msomi. Watanzania tuna matatizo makubwa ya akili. Endeleeni kumdanganya jiwe
Kwa sababu wewe siyo msomi ndiyo maana unaamua mambo kwa hisia; unafikir kwa kutumia tui la nazio badala ya ya ubongo.
 
Unaweza kujenga hivyo vyote bila kuua raia wenye mitazamo tofauti na wewe.

Ni unyama kuamini kuwa ni wewe pekee unayestahili kufikiri na kutenda kwajili ya wengine
Taariza kuua raia wenye mitazamo tofauti linakuzwa sana kwa vile halipo kabisa. Sijaona operation yoyote inayoendeshwa na serikal kuua watu wanaopingana na mtazamo wake; inapotokea kiongozi mmoja wa upinzani akashambuliwa, haina maana kuwa anashambuliwa na serikali kwa vile kumekuwa na taarifa pia za viongozi wa CCM kushambuliwa na kuuwawa.
 
Si wenyewe kwa hali ya uchumi wetu tumshakuwa level ya donors...alisikika mataga 1[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nchi maskini ikianza kujikomboa kiuchumi Mabeberu hutafuta mbinu za kuiwekea vikwazo. Wameshindwa kumuwekea vikwazo Museveni na Kagame ambao ni kama maraisi wa maisha leo waje waitolee macho TZ yetu kisa ni rasilimali zetu. Hatudanganyiki. Mbona uchaguzi wa Marekani hadi sasa bado kizungumkuti na hatusikii kelele za demkrasia ? Waoinzani wa Tanzania ni chanzo cha upuuzi huu. Wameshindwa kihalali wanabaki kutapatapa.
 
Dua la kuku halimpati mwewe. Wewe huwezi ukajua kuliko serikali inavyojua, unajisumbua tu na viposti vyako vya kitoto.
 
Siku hizi zinatumwa drones kwa utaratibu mzuri tu
 
Unapenda sana kusaidiwa kila kitu na Mabeberu utachelewa sana, Sasa hivi tumepata Raisi asiyependa kutegemea Mabeberu,ni mwendo wa kuchapa kazi tu sisi wenyewe na tutasimama! Je umeshajiuliza Kama kesho ukiamka na Ukakuta USA yote imesombwa na kimbunga utasemaje!? Au na wwe mtegemea USA ndiyo saa hiyohiyo na wwe utazima Mazima!?
 
Hakuna mtu anapenda kua tegemezi lakini huo Ndio uhalisia
Tuache kujidanganya eti tumepata rais asiehitaji misaada..... Mbona anaichukua?
Anyway muda ukifika Ndio tutajua kua Hao ni mabeberu au ni nchi wahisani
 
Inategemea wewe unaelewaje demokrasia ni kitu gani
Kwa ujumla Saudi Arabia na nchi zote zenye utajiri wa mafuta watu wake hawana shida ya maisha kabisa na wala hawajihusishi na siasa kabisa
Yani hata kuwa na uhuru wa kukosoa,mfano kama alivyokuwa yule mwaandishi Jamal kashoggi ambaye alikuwa akikosoa utawala wa Saudia.
 
Ben Sanane yuko wapi ?
Mazrui yuko wapi ?
Azory Gwanda yuko wapi
Kanguye yuko wapi ?
Alphonce mawazo yuko wapi ?
Uliona kwenye uchaguzi yaliyotokea huko Zanzibar na Tanzania ?

Na yote haya serikali iko kimya tukisema serikali imeyaridhia yafanyike tutakuwa tunakosea ?

Tukisema kuwa serikali ni incompetent imeshindwa kupambana na wahalifu wanaoteka raia tutakuwa tunakosea?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…