Elections 2010 Mabere Marando kuibukia CHADEMA?

Elections 2010 Mabere Marando kuibukia CHADEMA?

Naungana nawe Mwanakijiji kuwa Marando si TISS na wala hajawahi kuwa agent. Maagent wa TISS tunawafahamu na CHADEMA pia inawajua na wnegine tayari wapo ndani ya Chama.

Mimi nimemfahamu Marando kwa muda na nilijua kuwa atasuport CHADEMA kwenye uchaguzi toka mwezi wa tatu. Ila sikujua kuwa atajiunga rasmi kama Mwanachama.

Sasa tuongelee potentiality ya Marando:
1. kwanza kuwepo kwake kutahakikisha jimbo la Rorya linaenda CHADEMA (atakayebisha kwenye hili asubiri Octoba 31).
2. Ataisaidia sana CHADEMA kurejesha jimbo la Tarime ambalo kwa bahati mbaya sana CHADEMA ina kila dalili ya kulikosa kutokana na migongano isiyo ya lazima (infighting kati ya Mwikabe, heche na Mwera).
3. Mabere atakuwa msaada mkubwa sana kwa SLAA kwa kanda ya Ziwa maana anaheshimika sana.
4. Marando is a reputed public orator na anaweza kuteka masikio na kura za wasomi.
5. Marando hagombei uongozi wowote katika CHADEMA wala nchi so CHADEMA haina cha kupoteza.

Mimi si mshabiki wa personalities za watu ila imenibidi niseme kuweka records straight.

Uko sahihi kabisa Devils Advocate, tatizo ni kuwa wengi hawajui Marando ameplay role gani Chadema hadi leo na mahusiano yakoje kati yake na viongozi wa Chadema. Ningependa niwaulize tu kitu kimoja tu nacho ni hiki, ikiwa Uongozi wa Chadema hauoni taabu yoyote kushirikiana na Marando, wanaopinga uwepo wake Chadema wanatuambia nini - kwamba tayari leo hii hawana imani na maamuzi ya hao viongozi pamoja na kipenzi chetu Dr. Slaa ? Je wanafikiri wanamfahamu Marando kuliko Dr. Slaa, Mbowe, Zitto, Mnyika na wengineo ? Kama mnaanza kukosa imani na Dr. Slaa kwenye hili swali dogo la Marando kweli mko tayari kuwa wapiganaji anaowahitaji ?

Marando wengine tunamfahamu vizuri kuliko wengi wenu mnaomfananisha na Mrema na tuna hakika he is a big big asset kwa Chadema. Binafsi ningewaomba wana JF na hasa walioko tayari kuunga mkono jitihada za kuiondosha CCM madarakani, tuachane na haya mambo ya kuungaunga bila ushahidi kamili. Katika wasemaji wanaoweza kuvutia umati Marando ni mojawapo, he is a polished and convincing public orator ambaye ungependa umsikilize hadi mwisho akiwa jukwaani - ni wachache wenye kipaji kama chake. Huu utakuwa ni mchango wangu wa mwisho kwa sababu sitaki kuonekana kama nina ajenda iliyojificha ya namfagilia sana. Go Dr. Slaa, go !
 
Atavuruga tu kama akipewa uongozi wa ngazi ya juu, lakini akiwa mwananachama wa kawaida as I predict atavurugaje????????

Siyo kweli kuwa mwanachama wa kawaida hawezi kuvuruga. Mifano iko mingi. Anaweza kukiburuza chama mahakamani au kufanya vurugu kwenye chama hasa ikiwa ametumwa na serikali kufanya hivyo. Sasa akiwa tena wakili aliyebobea ni tatizo moja baada ya lingine. Chadema na vyama vingine viunde kamati ya uthibiti, na siyo kumpokea kila mja. Mnamkumbuka Lenin? Better few but Better!
 
Siyo kweli kuwa mwanachama wa kawaida hawezi kuvuruga. Mifano iko mingi. Anaweza kukiburuza chama mahakamani au kufanya vurugu kwenye chama hasa ikiwa ametumwa na serikali kufanya hivyo. Sasa akiwa tena wakili aliyebobea ni tatizo moja baada ya lingine. Chadema na vyama vingine viunde kamati ya uthibiti, na siyo kumpokea kila mja. Mnamkumbuka Lenin? Better few but Better!

Anaweza kukiburuza chama kortini bila makosa? Kuwa wakili aliyebobea hakumpi nafasi ya kufinyanga kesi ili mradi tu akifikishe chama mahakamani, kwa kosa lipi?

Mwanachama wa kawaida ni ngumu sana kufanya fujo kwenye chama kwa kuwa hayuko kwenye kikao cha aina yoyote ama hahusiki na kufanya maamuzi mazito yanayogusa uhai ya chama.

Watu wa kuogopa ni wale wanaokuja na wafuasi/mashabiki wao, maana wafuasi/mashabiki wanafuata mtu hawaangalii sera za chama husika. Makosa kama hayo waliyafanya zama za Mrema na hao wafuasi wakapewa uongozi, so linapokuja swala nyeti wafuasi hawaangalii hoja, bali wanaangalia huyo mtu wao msimamo wake ni upi?

Marando ametamka wazi kwamba hataki kugombea Ubunge wala hataki uongozi ndani ya CHADEMA, anachotaka yeye ni kuwaongezea nguvu CHADEMA.

Pamoja na hayo, kila chama kina taratibu zake, nina imani CHADEMA ni watu makini sana na hivyo kabla ya kumruhusu kuingia kwenye Timu ya Kampeni watakuwa wamefanya vetting ya kiwango cha kwao na kujiridhisha kwamba Marando ana nia njema au la.

Kitu kingine ambacho tunasahau ni kwamba, ukiona watu maarufu kama Marando wanatangaza kuhamia chama fulani lazima anakuwa alishaongea na top brass ya chama husika na wamekubaliana na kwamba chama hakina tatizo. Kwa hiyo baraza la wadhamini na baraza la wazee wanajua, kamati kuu inajua na wameishafanya uchunguzi wao wa kina na kujiridhisha kwamba wanamkaribisha. Asingeweza kukurupuka bila kupata go ahead ya top brass ya CHADEMA.
 
Ama kweli mipandikizi imejaa JF. Cha kupoza moyo ni kuwa idadi ya Wazalendo JF bado ni kubwa zaidi na mipandikizi inajulikana kwa magamba yao. Enzi za huko nyuma ilikuwa inasemwa nusu ya WaTz walikuwa ni mashushushu. Wanafanyia ushushushu ile nusu iliyosalia. Gharama zote hizo ili kudumisha ulaji wa watu wachache tu? Ndiyo maana nchi nyingine huwezi kuwa kiongozi kama wewe ni njaa kali.
 
Nampa MIA kwa MIA kwani kule alipo NCCR aliyekuwa mbaya mnamjua na mvurugaji kwani Mrema ni KADA wa CCM na mimi ni Swahiba wangu nalijua hilo anayo kadi tokea TANU sasa ilipokuwa sasa huko TLP mnaona kunavyofukuta lakini angalia NCCR kwa Mabere Kimya. Msidanganyike na MAGAZETI ya BONGO noma kwa kuchafuliana kwani wakiandika ukweli watu hawanunui, MH.MABERE MARANDO MIMI NIPO NA WEWE BEGA KWA BEGA SAFI SANA LETE CHACHU KWA CHADEMA, HAO WALIOKOMENT AGAINST NA WEWE NI KADA WA SISIEMU. BIG UP MTU MZIMA
 
Nfikiri Watanzania tuna matatizo makubwa sana, kama kweli watu wanasema Marando asikubaliwe CHADEMA eti atakisambaratisha inanisikitisha sana. Inaoonyesha jinsi ambavyo watanzania waanamini katika personality (mtu) zaidi kuliko mfumo. Kama CHADEMA kitavurugwa na Marando asiye na uongozi wowote ndani ya Chama basi hicho chama chenyewe hakifai.

Kwa maana nyingine mashabiki wa CHADEMA mnaomhofia Marando mnatupa signal tusio wanachama wa CHADEMA kuwa chama chenu dhaifu sana ( fragile). Yaani mtu mmoja asambaratishe chama?. Mimi naona Marando ni rasimali kubwa sana kwa CHADEMA kulingana na jinsi mtakaavyomtumia. Mimi nadhani kuna watu hatari zaidi ndani ya CHADEMA kuliko Marando.

Nyerere alipokufa watanzania walikuwa wanasema nchi imekwisha nani atakemea viongozi, nani atafanya hivi, sijui vikao vya CCM vitakuwaje bila Nyerere etc. Hata leo utawasikia watu wanasema Nyerere angekuwepo haya yasingetokea. Mimi nasema wanaosema hivyo bila kujijua wanaonyesha jinsi gani Nyerere alikuwa na mapungufu, maana kiongozi mzuri ni yule anayejenga mfumo ambao hata yeye asipokuwepo mambo yanaenda bila shida.

CHADEMA nafikiri kina mfumo unaoshughulikia watu au matatizo yanotaka kukivuruga chama chao bila matatizo. Mfano ni jinsi walivyoshughulikia suala la Chacha Wangwe na ule mtafaruku wa Zitto Kabwe.

Hata kama kuna watu wana hofu na Marando, mpeni benefit of doubt, msimuhukumu kwa mambo ya 1996 ambayo leo tunaona kabisa kuwa chanzo alikuwa ni Mrema, maana kama watu wanavyosema mtu anaweza kujificha asijulikane kuwa ni mlozi, lakini anapokaribia kufa lazima itakuwa wazi tu.

Wiki ijayo CCM tutaanza ku off load wengine jiandaeni kuwapokea.....................................wengine ni vifaa ile mbaya maana hata Slaa tulimtema sasa tu(najuta)
 
Namkumbuka Marando alipotuhamasisha kuandamana kwenda ikulu toka viwanja vya jangwani, nakumbuka tukiwa mstari wa mbele huku tumeshikana mikono tulipofika maeneo ya DIT iliyokuwa Dar Tech FFU waliokuwa wamejipanga mbele yetu barabara ya Bibi Titi wakatoa kitambaa chekundu. Nakumbuka vizuri baada ya mabomu kupigwa tulivyoruka lile geti la Dar Tech na Marando tukajikuta tumo ndani ya uzio wa Dar Tech.

Namkumbuka tena Marando kule Laskazone Tanga alivyoamlisha taa zizimwe na meza ya Mwenyekiti wakati huo Mrema Ikabinuliwa ili uchaguzi uvurugike. Nikiunganisha na sakata lake la kuwania Ubunge wa EAC alivyopigiwa kampeni la nguvu na CCM, mmhuu sijui labda mimi ndiye simwelewi vizuri huyu jamaa.

Lakini all in all sina tatizo na Marando kujiunga Chadema kwa vile naelewa ndani ya Chadema kuna watu makini watakuwa wameangalia pros and cons. Namjua Marando ni mwanamageuzi halisi aliyepotea, atulie aonekane anakijenga chama kama alivyotulia Lwakatare, vinginevyo kama atakuja na lake atajulikana muda si mrefu, Chadema huwa haichelewi kumwonyesha mtu mlango.


Heshima kwako Luteni,

Mkuu hoja zako zimesimama kweli na zitaendelea kusimama kwasababu moja kubwa haujaweaka hata chembe moja ya unafiki.Mkuu kuna watu wanajaribu kuipotosha historia ya mageuzi hapa Tanzania kwasababu eti Mabere kahamia CHADEMA !.Nikikumbuka jinsi Marando alivyosaidiwa na dola Tanga ili uchaguzi usifanyike leo hii anaitwa mwanamageuzi nazidi kuwashangaa kama sio kustaajabu.Nikikumbuka vyama vyama vya upinzani vilikuwa na mgombea wao wa nafasi ya ubunge wa EA lakini Marando kwa msaada mkubwa wa CCM na dola alishinda ubunge nazidi kuwashangaa wanaomwona Mabere ni shujaa wa mageuzi.

Mabere Marando atabaki kuwa ni mtu hatari sana katika siasa za mageuzi hapa Tanzania hajalishi kama kaenda CHADEMA au karejea CCM.
 
Mhhh................kazi kweli kweli, lakini MMJ katusaidia kuwa yeye sio ajenti wa TISS. Labda yeye anaweza kujenga hoja vizuri kiasi cha kufanya hata dola au CCM (ubunge wa EAC) wamuunge mkono. Kuna sredi mmoja nilisema niliwahi kumuuliza Marando kama Mrema anatumiwa na CCM alikataa kabisa, alisema ila anweza kuwa anatumika bila yeye kujijua. Mimi namuamini Marando maana angeweza kumpakazia Mrema kuwa anatumika na CCM( bila shaka wakati huo hakujua). Kumbukeni vurugu za NCCR mageuzi zilikuwa baada ya uchaguzi wa 1995, kama Marando angetaka kumhujumu Mrema angefanya wakati huo, mbona alimuunga mkono kwa dhati?. Shida ilianza alipoambiwa akasome ili ajiandae kwa uchaguzi wa mwaka 2000.
 
Back
Top Bottom