Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 38,283
- 97,793
Za huku njema kabisa sijui wewe na familia?Habari nzuri Shemeji, za huko...
Nadhani pia kuna shida mahala katika malezi ya watoto wa sasa.Habari za muda huu wana jamvi
Naandika uzi huu nikiwa kwenye daladala nikirejea nyumbani kutoka kwenye "mihangaiko" ya Kila siku
Ndani ya daladala nmekaa karibu na wakina mama wawili wakipare(nimesikia wakiongea kipare). Hawa kina mama wanaelezana kuhusu tabia mbaya za mabinti zao waliohitimu vyuo ambao umri unaenda na hawajapata kazi Wala hawajachumbiwa.
Kinachowauma zaidi ni tabia ya Hawa "mabinti" kushinda ndani na kutizama movie muda wote badala ya kutoka nje watembee tembee huwenda wakakutana na "ngekewa".
Namnukuu mmoja akisema "Yani Bora wa kwako hata kanisani anaenda, Mimi huyu wangu hatoki hata kwenda dukani hataki, hana hata marafiki akatembee huko anaweza akapata mume njiani lipo lipo tu"
Wadogo zangu wa kike jitahidini kutembea tembea mama zenu wanataka muolewe mtazeekea ndani.
😀 😀 😀Kuna siku tulikuwa na mjadala kati ya Ke na Me wakihitimu chuo ni yupi msoto wake unakuwa wa kutisha
1. Wa kike anashinda ndani kutizama Tv, ila anasimakia shuguli za jikon ambapo chakula kula uhakika
2. Wa kiume huwa tunajifungia chumbani, na watu wakikuchoka watapika watakula bila kukustua ili baadae waseme tulijua ulitoka.
Ila msoto wa baada ya chuo heshima kwake, ukiwaza na kidgree chako cha kukariri notes za community development na huku jamii ilokujaza bichwa ukiwa chuoni kwamba ww ni msomi, ndo unaanza kujitusi,
Watakuambia mtaji ndio shida.Ungewaambia hao wamama kuwa kuolewa sio ajira, wawasisitize mabinti zao kufanya hata biashara ndogondogo.
Watoto wa siku hizi hata ''skrapa'' hawaokoti , miaka ya nyuma watoto wanatafuta pesa tangu shule ya msingi ila ilikuwa mbaya wananogewa sana mpaka wamnaacha shule ...Sasa hivi hata kesi za child labour hakuna kama zamani ndio inafanya watu wabweteke mpawa wawe wakubwa.Nadhani pia kuna shida mahala katika malezi ya watoto wa sasa.
Nakumbuka wakati sisi tunakua, tulikua na marafiki wengi sana kutokana na mtindo wa maisha wa kipindi kile. Na hii ilikua ni kwa watoto wa kike na wakiume. Michezo mingi sana ya outdoors ilikuwa inatukutanisha na kupelekea kujenga urafiki ambao uliendelea mpaka tumefika sekondari na wengine hadi vyuoni nk.
Ukiacha hayo, pia kulikua na matukio mengi ya kuwaleta vijana pamoja kama madisko vumbi, concert, mabonanza ya mitaani, mechi za mpira, sinema, matamasha nk kwahiyo ilikua ngumu mtu kukaa tu ndani.
Siku hizi watoto tunawalea indoors. Mtu anasoma kuanzia msingi mpaka chuo kikuu hata mtaa anaoishi haujui vizuri maana anapanda gari asubuhi na jioni, hana marafiki, hana cha kufanya, hana pa kwenda, starehe yake kubwa ni kuangalia tv na kulala! Hii ni hatari sana kwa kizazi kinachokuja sijui tutakua na watu wa aina gani?
Mkuu hapo kwenye 'hata vyuma hawaokoti' nimecheka sanaWatoto wa siku hizi hata ''skrapa'' hawaokoti , miaka ya nyuma watoto wanatafuta pesa tangu shule ya msingi ila ilikuwa mbaya wananogewa sana mpaka wamnaacha shule ...Sasa hivi hata kesi za child labour hakuna kama zamani ndio inafanya watu wabweteke mpawa wawe wakubwa.
Makadirio wanaomaliza chuo ni miaka 22 na kuendelea hapa hawana mbinu yoyote ya kupata pesa, akifikiria maisha ya chuo then aanzie chini basi anaona jau sana.
Kuna mfumo wa maisha ya Tanzania MUNGU ameuweka ila hautumiki, na kama umetumika ni 2% ya software yake imetumika! Waache waendelee kung’ang’ania 🎓 wakati la saba wanaendelea kula mema ya Tanzania life improvement Software tuliyowekewa na MUNGU!Kuna siku tulikuwa na mjadala kati ya Ke na Me wakihitimu chuo ni yupi msoto wake unakuwa wa kutisha
1. Wa kike anashinda ndani kutizama Tv, ila anasimakia shuguli za jikon ambapo chakula kula uhakika
2. Wa kiume huwa tunajifungia chumbani, na watu wakikuchoka watapika watakula bila kukustua ili baadae waseme tulijua ulitoka.
Ila msoto wa baada ya chuo heshima kwake, ukiwaza na kidgree chako cha kukariri notes za community development na huku jamii ilokujaza bichwa ukiwa chuoni kwamba ww ni msomi, ndo unaanza kujitusi,
Unajua naona kama mipango ya serikali inalenga kuwasabotage watoto wa kike miaka hii[emoji848]Hali ya upatikanaji wa ajira imekuwa tete kutokana na wahitimu wengi kuwepo mitaani bila kuajiriwa na haijulikani watapata ajira lini. Kuna msoto mkali kwa wahitimu na serikali haina mkakati wa kuajiri kwa haraka wahitimu ili wasidode mitaani. Unaweza ukadoda mitaani miaka hata mitano au zaidi kama hutajiongeza kutafuta fursa zingine nje ya taaluma uliyosomea. Kwa mabinti wenye ndoto za kuwa na familia/watoto ni bora wakaingia kwenye ndoa haraka kabla ya umri kupanda. Wakiwa ndani ya ndoa wataendelea kusaka ajira walizozisomea kuliko kusubiri mpaka wapate ajira ndio waolewe, watachakaa na kuonekana ni wakongwe na hawatazaa wakiolewa. Kama hawataki kuolewa basi wazae tu na wapenzi wao kisha wakubali changamoto za usingo mama
Sio lazima uandaliwe mazingira. Umepelekwa ahule mpaka chuo kikuu sasa hapo unataka mazingira ganj labda mengine kamanda?Hao wamama wamezaaa watoto wameshindwa kuwaandalia mazingira mazuri wanawaza kuwaozesha...akili za kipumbavu sana hii
Usichokifahamu kuna ajira halafu kuna namna ya kuishi. Wewe hapo ukiwa na shida kuna watu wanakupa msaada bila masharti ya kuwapelekea wadhamini wala dhamana yoyote wanakusaidia sababu wanakujali na wewe ni sehemu ya Maisha yao, unaka kunambia hawa watu ni taaisisi au kampuni ya mikopo na wanalipa kodi serikalini kwa wanavyokusaidia? [emoji848]Ungewaambia hao wamama kuwa kuolewa sio ajira, wawasisitize mabinti zao kufanya hata biashara ndogondogo.
Sio kila mtoto anakua na uwezo wa kuingia mtaani na kupambana wengine mpaka washikwe mkono.Sio lazima uandaliwe mazingira. Umepelekwa ahule mpaka chuo kikuu sasa hapo unataka mazingira ganj labda mengine kamanda?
Ni kwel uko sahihi kamandaSio kila mtoto anakua na uwezo wa kuingia mtaani na kupambana wengine mpaka washikwe mkono.
Zamani wazee wetu walikua smart sana kwenye kuwajua tabia watoto wao, ambae mwenye uelekeo wa kusoma atapelekwa shule nzuri za private mpaka mambo yake yaende sawa na Kwa wale ambao mambo ya shule hayapandi kichwani atakua mazingira ya home anasaidiana na mzee kuchunga ng'ombe na kulima baada ya mda anaoa home wanampa shamba na mifugo kidogo siku zinaenda maisha yake yanakua vzr
Kutaka urahisi wa maisha ndio sababu iliyowafanya waende shule in the first place ili wapate ajira wapate mali haraka sasa mission ndio imeshakuwa impossible lazima wachakae kiakili na kimwili.Inasikidisha kwakwel.
Lakin baya zaidi ni kwamba vijana wengin wanakosa utayari wa kujitoa , hata ukiwapa kazi hawana morali wala juhudi wala nidhamu, unaishia kuwaangaliaa na kusikitika.
Maisha ya fasta fasta kwa kiwango kikubwa yamewaathiri, hawana utayari kabisaaa wa kujipa muda wa kuhangaikia jambo mpaka likae sawa.