Elections 2010 Mabinti watumiwa kumrushia Mbowe kombora!

Elections 2010 Mabinti watumiwa kumrushia Mbowe kombora!

Status
Not open for further replies.
Hawa wasichana wanafahamika sana katika ile mitaa ya kujiuza usiku hapa jijini Dar. Huyo Dada mwenye mdomo uliorefuka kama samaki chuchunge anaishi Sinza kumekucha. Wapo katika biashara hawana lolote jipya.

Aha! Ina maana CCM iawatumia wajiuzao?
 
Aha! Ina maana CCM iawatumia wajiuzao?

Kama CCM inakodi mabasi na malori kuwabeba watu ili wafike katika mikutano yao pamoja na kuwapa pesa kati ya sh 5,000 - 20,000 itashindwaje kuwanunua hawa machangudua aka kuku wa kienyeji?

 
Ahhh! CCM Dah! Hiki chama kinani chekeshaga sana kipindi cha uchaguzi. Ki Ukweli kinaweza SIASA.
 
hizi ni siasa za maji machafu . kama kampeni zimefika mpaka hapa kweli kazi ipo

CCM maji shingoni mwaka huu. Naona huko aliko jangili wa uchumi wa nchi yetu Rostam Azizi and the Co.hawapati hata usingizi wakiwaza mbinu za kumchafua Slaa na wenzake. Uzuri wananchi walishagundua hii kitu hawadanganyiki mwaka. People's Power.
 
Hawa wasichana wanafahamika sana katika ile mitaa ya kujiuza usiku hapa jijini Dar. Huyo Dada mwenye mdomo uliorefuka kama samaki chuchunge anaishi Sinza kumekucha. Wapo katika biashara hawana lolote jipya.

Kweli CCM iko mahututi kama alivyo mgombea wake - yaani inawatumia hadi machangudoa ! Anyway they do have a lot in common kwani kikubwa kinachotafutwa ni pesa - tizama wanavyojitembeza na kujipitishapitisha, mabango hadi kuta za vyoo ! Lakini people's power itahakikisha wanalala chali.
 
Huyu mwenye username ya mstahiki ndo huyo kaicreate au katumwa kuicreate????
Yatakuwa ni makosa kama tukiendelea kujidanganya kuwa nchi yetu ni salama, CCM na wafuasi wao naona badala ya kuzungumzia ishues au kupanch hoja zinazokihuissisha chama chao na ufisadi wao wamemua kujibu kwa personal attacks, huu mkakati wa kupandikiza chuki hauna maana yoyote. Wasira anasimama anasema Slaa ni mbumbumbu wa uchumi eti sababu atatoa elimu bure, huu ni ukosefu wa busara, angeweza kusimama jukwaani na kupangua hoja kwamba elimu bure haiwezekani kwa sababu moja,mbili,tatu, na kuendelea... Hii ndi siasa kuliko wao wanasingizia wenzao kuongea matusi wakati wao wanayaporomosha.

huyu mama ntiliye mambo ya Slaa na mkewe yeye yanamuhusu nini,. au ndi huko tu kutumiwa?? na hao mabinti wanaonekana kabisa kutunga hayo maneno wanayojaribu kuyakukumbuka. Ni uppuzi kusema GDP ya tanzania ni Biolioni 24. Hizo bilioni 24 ni US Dollar au Tsh??
Aliyeandaa tangazo hili arudi akajifunze upya hapa kachemka,
 
Kwa hiyo all the attacks that CCM has against CHADEMA are Josephine na hii???????????? Du!!!!! these should be last kicks of a dying horse!
 
Tanzania kushindwa kuendelea miaka yote hii pamoja na rasilimali zetu ni kutokana na kutawaliwa na watu wasiotumia akili kama hawa wa CCM waliotumia njaa ya hawa innocent girls ili sura zao zitumike kueneza uongo usiokuwa na maana. Kwa nini basi wasiseme wao CCM wanachukua ruzuku ya kiasi gani na zinatumikaje kama wanataka kuwa wakweli.

Hii ni dalili ya wazi kuwa CCM ikishindwa uchaguzi itafanya vurugu za aina yoyote ile ili waendelee kubaki madarakani.
 
Kwa hiyo all the attacks that CCM has against CHADEMA are Josephine na hii???????????? Du!!!!! these should be last kicks of a dying horse!
Na hii imebuniwa na Makamba akasema itakapotoka tu Mbowe kwisha kazi, kweli sasa wameishiwa wanatangatanga mara yuko Iringa mjini kesho kesharuka Musoma keshokutwa anarudi Makete siku inayofuata Pemba yaani mradi anazunguka hewani hana lolote.
 
mbona siielewi hii video.... wanahamasisha ngono au kampeni!! "ETI LILE FATAKI LAKO VIPI "....


Kwa kuwa mimi ni mtaalam wa communications, nitafafanua nia mbaya iliyotumika kumpaka matope Mbowe na chama chake, CHADEMA, kama ifuatavyo:

1. Kwanza, kuna innuendo (dhana mbaya) kwamba "lile fataki lako" ambalo ni la "CHADEMA", yaani "Mwenyekiti wa CHADEMA", Freeman Mbowe, anajihusiha na vitendo vya kushiriki ngono na "watoto", kwani kwenye picha, ni dhahiri kwamba hawa ni watoto, tena ambao hawazidi umri wa miaka 22! Ni watoto.

2. Dhana ya pili ni kwamba Mwenyekiti wa CHADEMA anachukua Shs. Milioni 10 kati ya Shs. Milioni 60 za ruzuku inayotolewa serikalini kwa CHADEMA. Je, kuna ushahidi wowote juu ya hili? Je, ni kweli?

3. Dhana ya tatu ni kwamba, Shs. Milioni 10 kati ya Shs. Milioni 60 i sawa na asilimia 16-17.

4. Dhana ya nne ni kwamba, kwa mujibu wa madai hayo, kutoka kwenye pato la taifa, CHADEMA inachukua Dola Milioni 400, kwa mtazamo wa mgao kutoka kwenye GDP (Gross Domestic Product, au Pato la Taifa).


Napenda kuwajibu hawa mafisadi kama ifuatavyo:

1. Kuhusu hao mabitinti, WAMEJIDHALILISHA wenyewe - kwa umalaya wao - kwani, kutokana na ukweli kwamba WAMELIPWA ili kupayuka maneno yasiyo na msingi, ambazo ni kashfa kubwa, wamedhihirisha kwamba wao ni mashabiki wa matendo ya UFATAKI! Kwa hiyo, kama ni maigizo, walikuwa WANAFANYA KWELI, kwamba wao wanashiriki ngono na watu wazima! Madai ya kwamba Mbowe anajihusisha na vitendo hivyo hayana msingi, kwani hakuna ushahidi wowote ule uliotolewa, wa maandishi au picha. Hii ni CHARACTER DEFAMATION, Mbowe anaweza kuamua kumchukulia hatua yeyote yule ambaye amediriki kusambaza tangazo hili chafu, au hata (kwa mtazamo wa ushahidi wa mazingira), kuishtaki mahakamani CCM na kudai fidia ya kuchafuliwa jina. Kwa hao mabinti, hawa ni sehemu ya KIZAZI KILICHOPOTEA (GENERATION LOST), na kwa upande wa Tanzania, WAKO WENGI wa aina hii! Tusitarajie lolote jema kutoka kwao! Wamepotea njia, kamwe hawatarejea kwenye mstaari! IMEKULA KWAO!

2. Nijuavyo mimi, chama chochote cha siasa hupata ruzuku kutokana na uwingi wa wabunge wake na madiwani wake. Ushahidi unaotakiwa hapa ni kwamba ITHIBITISHWE kwamba CHADEMA inapokea ruzuku ya Shs. Milioni 60 kila mwezi, na ushahidi huu anapaswa kuutoa Katibu wa Bunge na/au Msajili wa Vyama vya Siasa. Pili, ithibitishwe, kwa mujibu wa Kanuni na/au Katiba ya CHADEMA, kwamba Mwenyekiti wake anastahili kulipwa Shs. Milioni 10 kila mwezi, kama mshahara wake, na uthibitisho huo ufanyike kwa kutumia hati rasmi za malipo za CHADEMA. Vinginevyo, hii ni kashfa nzito, ambayo inakwenda moja kwa moja mahakamani.

3. na 4. Hizi nazijibu kwa pamoja. HAKUNA USHAHIDI uliooneshwa kwamba CHADEMA ina haki ya kupata Dola Milioni 400, ambazo ni asilimia 16-17 za Pato la Taifa. HAKUNA USHAHIDI wa moja kwa moja kuihusisha CHADEMA na malipo hayo, kwani, HAKUNA USHAHIDI wala HAKUNA SHERIA iliyopitishwa na Bunge kuidhinisha vyama vya siasa kulipwa kutokana na pato la taifa. HAKUNA. Kama CHADEMA wangekuwa wanapokea Dola Milioni 400, hata kwa mwaka, kama ruzuku, hawangekuwa na haja ya kudai mabadiliko serikalini, wala kugombea urais, kwani pesa hizo zingeweza kutekeleza ilani yote ya uchaguzi, na pesa nyingi kubakia. Dola Milioni 400 ni takriban sawa na Shs. Bilioni 700 za Kitanzania!


Aliyeandika "script" ya tangazo hilo la kifisadi ni mtu anayejiona kuwa ni MJANJA, kumbe ni mpumbavu! Najua, wapo watu WATAKAOAMINI kwamba ni kweli, malipo ya Mbowe ni sawa na Dola Milioni 400 kwa mwezi. Huu ni ujinga uliopitiliza hadi kufikia ujuha na uzuzu, hatimaye kuwa upumbavu na upunguani! Mtu mwenye akili timamu hawezi kutoa madai yasiyo na kichwa wala mguu kama haya!

Mimi ni mchumi, na hoja hii ya GDP haioneshi uhusiano wa moja kwa moja kwa CHADEMA na Pato la Taifa la Tanzania. CHADEMA inahusika kwa namna gani na GDP ya Tanzania?

Ama kweli, maji yameifika shingoni CCM! Inatapatapa, inatapatapa sana, na kadri inavyozidi kutapatapa, kumbe ndivyo inavyozidi kuharibu!

Huu ni mfano mwingine wa jinsi ujinga unavyopitilia hadi kuwa UPUNGUWANI na UHAYAWANI! Haiyumkini tukatarajia UONGOZI BORA kwa watu wanaodiriki kusema uongo kama huu!

Wanasheria wangu, Tundu Lissu na Mabere Marando, mna kazi ya kuipeleka CCM kwa Tume ya Uchaguzi (NEC) na pia Mahakama Kuu, kupinga ukiukwaji wa Kanuni za Maadili ya Uchaguzi na kudai fidia!

-> Mwana wa Haki

P.S. Unaweza kuwadanganaya watu wachache mara chache, lakini huwezi kuwadanganya watu wote mara zote!
 
Video imetengenezwa na CHADEMA na inasambazwa na CHADEMA wenyewe.

Hatudanganyiki lakini tunaendelea kudanganya.:lol:


CHADEMA wana sababu gani za KIJINGA NA KIPUMBAVU kutumia rasilmali zao (fedha, watu, taaluma, teknolojia, etc.) kutengeneza uchafu huu? Kama ni umaarufu tayari wanao, na ndio unaoitia kiwewe CCM!

Kaka, nadhani unahitaji kuleta ushahidi USIOPINGIKA hapa, kuthibitisha madai yako! What is the motive and benefit for CHADEMA to engage in these sewerage-politics?
 
Si ajabu hata hao mabinti hawaelewi GDP ni nini, waulize utasikia. Slaa una kazi baba, hii elimu ya bure ni muhimu sana. Naamini hata hawa mabinti wakiipata watakushukuru.
 
DUh ....hii ya leo kali!

haya matangazo nayo hwa yanarushwa hewani wapi? au ndio youtube tu?
 

Aisee, nimewapenda ghafla these chicks, i need them for the GROUP THINGIE. Maana wanaonekana wanauza naniliu zao hawa and am ready to bid.
Yaani ntakesha nao

Kuhusu hako kafilam walikokatengeneza ni another malipo ya kulaliwa usiku kucha na vibabu vya ccm
 
Last edited by a moderator:
CCM wanajimaliza kiulaini. Inapotokea mtu mmoja wa upinzani anaingia CCM tunasikia makelele meeeeeengi kwenye vyombo vya habari. Lakini wanaoihama CCM vyombo vichache sana vinatangaza. Sasa CCM wanabuni mbinu mpya kila siku za majitaka. Tusubiri wiki mbili za mwisho wa makampeni, maana CCM wanachokoza wasikie mlio wa kiberiti, ili warudi kujisafisha. Lakini tutaona kama wiki mbili za mwisho zitatosha kurudi kujisafisha nchi nzima? Chadema na CUF za mwaka huu sio kama za miaka mitano iliyopita. Watu wanaona bayana. Ofcourse kila chama na kasoro zake, sio malaika. After all hata Shetani alikuwa namba 2 kutoka nafasi ya Mungu, lakini kasoro zilkujaonekana na hatimaye akadondoka. Iskariote pia.

CCM wakubali kwamba dunia inabadilika kwa kasi Mbinu za wizi wa kura walizotegemea miaka yote wajipange upya mwaka huu. Nchi haiwezi kwenda mbele kwa porojo nyingi na kuweka vizingiti kwa wengine. Vyama vya upinzani safari hii na elimu bure na tiba bure ni kete itakayowainua sana mwaka huu hata kule vijijini. Nawashauri sasa wapinzani wasambae vijijini kote wakajionyeshe, watumie udhaifu wa CCM kuogopa midahalo kwa kujiimarisha. Yawezekana kabisa ccm wanajisokotea kamba yao wenyewe ya kujinyongea, kama sio leo basi sio mbali sana. Iliwezekana Malawi, Kenya na Zambia kuwaengua mapapa waliodhani hakuna mwingine, kwa nini isiwe Tanzania? Natamani CCM nao wajifunze kutoka kwa wenzao wakiwa pembeni, maana wanavyo viswahili vingi sana ukiwaambia makosa yao wanapokuwa kwenye kiti, wanadhani wanazo akili kuiko mtu yeyote. Wote walisoma na kutibiwa bure, sasa wamegeuka wanajenga maprivate na watoto wao wanawapeleka ughaibuni kusoma au kwenye shule wanazofundisha watu kutoka ughaibuni ati ni bora zaidi, hali wakidhoofisha elimu za watu wa chini na kurithishana uongozi katika mtandao wa familia zao kama vile Tanzania ya sasa ni nchi ya kifalme.

Hao mabinti wana njaa kali, ofcourse wakipata chao wanaishia, mwingine akiwalipa waseme exactly the opposite watafanya kweli. Usicheze na njaa, hakuna mtu mzima wala hekima kwenye njaa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom