KERO Mabwawa ya Mabibo (Dar) yanahatarisha afya za Wananchi, yanatiririsha maji yenye kemikali za Viwanda kwenye makazi ya Watu

KERO Mabwawa ya Mabibo (Dar) yanahatarisha afya za Wananchi, yanatiririsha maji yenye kemikali za Viwanda kwenye makazi ya Watu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
photo_2024-11-09_12-32-31 (2).jpg

photo_2024-11-09_12-32-33 (2).jpg
Licha ya wahusika kujenga mabwawa eneo la Mabibo kwa lengo la kuweka usalama wa kuhifadhia majitaka yanayodaiwa kutokea viwandani lakini Wananchi wapo hatarini kuathirika na maji hayo kutokana na kutiririka kwenye makazi na kutoa harufu kali za kemikali.

Wengi uenda tukawa tunafahamu mabwawa yaliyopo Mabibo Mwisho karibia na Chuo cha NIT, katika kipindi ambacho nimeishi maeneo ya pale karibu na yalipo Mabwawa nimekuwa nikisikia harufu kali ya kemikali lakini baada ya kudodosa huku na kule nilifahamishwa kwamba yale maji yanatoka kwenye Viwanda vilivyopo maeneo ya Urafiki.

Mabwawa hayo yapo matano ambayo yanahifadhi maji machafu na kuyatiririsha katika mwelekeo mwa yalipo makazi, ambapo ikitokea mvua zimenyesha maji hayo usambaa hadi kwenye makazi jambo ambalo ni hatari kwa afya za Wananchi.

Najiuliza kulikuwepo na sababu zipi za kuweka mabwawa hayo ingali maji hayo yanaachwa yaelekee kiholela kwenye mijereji inayokatiza kwenye makazi ya Wananchi bila kuwepo na miundombinu rafiki.
photo_2024-11-09_12-32-34.jpg

photo_2024-11-09_12-32-26.jpg
Pia mabwawa hayo yanazalisha harufu mbaya hasa za kemikali ambazo zinaweza kuwaathiri wananchi hususani wakazi ambao wanalizunguka eneo hilo kutokana mabwawa hayo kuwa wazi.

Nitoe wito kwa mamlaka ikiwemo NEMC kufuatilia kwa ukaribu suala hilo ambalo linahatarisha sana usalama wa Wananchi kupitia mazingira niliyoeleza.

Ni muhimu miundombinu ikaboreshwa kwa kuzingatia teknolojia bora ambazo zinaweza kufanya maji taka hayo kuhifadhiwa na kutiririshwa bila kuleta athari kwa wananchi.
photo_2024-11-09_12-32-31.jpg
photo_2024-11-09_12-32-30.jpg
photo_2024-11-09_12-32-27.jpg
 
Mabwawa yapo toka Miaka ya 1990s hizo kemikali umeziona leo? Njoo Manzese/Tandale Uwanja wa fisi ishuhudie demu 500
 
Licha ya wahusika kujenga mabwawa eneo la Mabibo kwa lengo la kuweka usalama wa kuhifadhia majitaka yanayodaiwa kutokea viwandani lakini Wananchi wapo hatarini kuathirika na maji hayo kutokana na kutiririka kwenye makazi na kutoa harufu kali za kemikali.

Wengi uenda tukawa tunafahamu mabwawa yaliyopo Mabibo Mwisho karibia na Chuo cha NIT, katika kipindi ambacho nimeishi maeneo ya pale karibu na yalipo Mabwawa nimekuwa nikisikia harufu kali ya kemikali lakini baada ya kudodosa huku na kule nilifahamishwa kwamba yale maji yanatoka kwenye Viwanda vilivyopo maeneo ya Urafiki.

Mabwawa hayo yapo matano ambayo yanahifadhi maji machafu na kuyatiririsha katika mwelekeo mwa yalipo makazi, ambapo ikitokea mvua zimenyesha maji hayo usambaa hadi kwenye makazi jambo ambalo ni hatari kwa afya za Wananchi.

Najiuliza kulikuwepo na sababu zipi za kuweka mabwawa hayo ingali maji hayo yanaachwa yaelekee kiholela kwenye mijereji inayokatiza kwenye makazi ya Wananchi bila kuwepo na miundombinu rafiki.
Pia mabwawa hayo yanazalisha harufu mbaya hasa za kemikali ambazo zinaweza kuwaathiri wananchi hususani wakazi ambao wanalizunguka eneo hilo kutokana mabwawa hayo kuwa wazi.

Nitoe wito kwa mamlaka ikiwemo NEMC kufuatilia kwa ukaribu suala hilo ambalo linahatarisha sana usalama wa Wananchi kupitia mazingira niliyoeleza.

Ni muhimu miundombinu ikaboreshwa kwa kuzingatia teknolojia bora ambazo zinaweza kufanya maji taka hayo kuhifadhiwa na kutiririshwa bila kuleta athari kwa wananchi.
Hao siyo wananchi wa kawaida, ni haki yao kuendelea kuishi hapo. Ukiwapima hao wananchi utaona wana DNA za Kambale.
Hao wananchi ndiyowaeyafuata hayo mabwawa hapo, sababu kwa DNA zao hayo ndiyo mazingira rafik kwao.
 
Back
Top Bottom