Machache niliyoyaona kwenye mechi ya Arsenal vs Olympiacos

Machache niliyoyaona kwenye mechi ya Arsenal vs Olympiacos

Cytochrome p450

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2019
Posts
5,638
Reaction score
15,044
Leo Arsenal imetolewa rasmi kwenye michuano ya kombe la Europa League baada ya kupigwa nyumbani kwake mabao 1-2, mechi ikienda hadi kwenye dakika za nyongeza na mwishowe tukishuhudia Arsenal ikitolewa kwa aggregate ya magoli (2-2)

Binafsi kama mpenzi wa soka la ulaya, yafuatayo ni machache kati ya mengi niliyoyaona kwenye timu ya washika bunduki (The Gunners)

1. Lacazette hafai kuwepo kwenye timu ya Arsenal

Wakati anakuja alifanikiwa kuonyesha kiwango kizuri ambacho mimi kama mdau wa soka la kulipwa nilikikubali kwa asilimia nyingi. Wengi walikuwa wakimuita Fighter kwa jinsi alivyokuwa akijiyoa kwa ajili ya timu. Ila ukweli uliopo sasa ni kwamba jamaa kabakia NDEVU tu, hatishi tena.

2. Pepe sio mchezaji wa kiwango cha Arsenal

Nilikuwa mgumu sana kukataa hili ila sasa naliona nikiniumbua moyoni. Niliamini sababu ya mazingira mapya ndio iliyomfanya mpaka asiperform vizuri, ila sasa kwa mbaali namuona kama Gervinho anakuja hivii! Mara anakataa!!

3. Mustafi ni mchezaji wa timu ndogo

Sijui Arteta kapata ushujaa gani wa kumuamini yule jamaa. Kwanza hajiamini hata kidogo. Naona watu wanamsifia siku hizi, ila kwangu mimi nikimuona nazuta picha ya dumu la petrol tu. Muda wowote.

4. Timu yote ni ya kubadili isipokuwa wachezaji wawili (2) tu

Hao ni kipa, Leno pamoja na Auba. Waliobaki wote sio hadhi ya Arsenal.

Nihitimishe tu kwa kusema, Arsenal kwa stage iliyofikia haitakiwi kushiriki mashindani makubwa yeyote ie. UEFA Champions League/Europa League. Kwa sasa ni bora wazingatie kwenye kuboresha timu zaidi. Nafikiri itakuwa na ushindani zaidi baada ya misimu miwili au mitatu.

Nawaza itawezaje kupata World Class Players kama haitoshiriki mashindano makubwa kama UEFA? Jibu sipati.

Timu kama Liverpool nayo ilipitia vipindi vigumu kama hivi, lakini wakapata kujijenga na sasa imerudi kwenye game.
Tunaona hakuna wachezaji mizigo tena kwenye timu kama Liverpool.

Tumpe muda Mikel, labda anaweza akaleta mabadiliko.

Mimi sio mwandishi mzuri, ila kwa hapo nilipojitahidi nadhani ujumbe umefika.
 
Mie nilishaacha kuangalia game zetu za arsenal toka alivyoanza kuboronga Mr. Bean Wenger!

Si Arsernal tu, hata Man na, chelsea, wamekuwa na mpira mbovu usiovutia kabisa!

Waliobaki ma mpira wao ni Liva, Toten na City kwa mbali.

Nimeamua Bora niandalie Movie kuliko live match ya timu hizi.
 
Yaani niliacha kuifuatolia Arsenal miaka minne iliyopita. Ni timu inaomiliki wachezaji wanaostahili kucheza ligi kuu ya Zanzibar.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nina miaka 8 sijawahi kufuatilia mechi za arsenal wala kuingia kibandaumiza kuangalia Arsenal japo mimi Gunners napenda kuangalia Real Madrid mechi zao sana na Manchester City.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie nilishaacha kuangalia game zetu za arsenal toka alivyoanza kuboronga Mr. Bean Wenger!

Si Arsernal tu, hata Man na, chelsea, wamekuwa na mpira mbovu usiovutia kabisa!

Waliobaki ma mpira wao ni Liva, Toten na City kwa mbali.

Nimeamua Bora niandalie Movie kuliko live match ya timu hizi.
Totenham ya Morinyo ondoa kabisa hapo.

Imekua timu ya kupaki basi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
huyu Auba anaweza kuondoka msimu ujao,anajitahidi kufunga ila team haishindi.Tumpe muda Arteta aweke wachezaji anao wataka. Kuna wachezaji wanakuja vizuri hasa bwana mdogo Bukayo Saka, bora mwalimu ampange Martinel kuliko LACA.
 
Mie nilishaacha kuangalia game zetu za arsenal toka alivyoanza kuboronga Mr. Bean Wenger!

Si Arsernal tu, hata Man na, chelsea, wamekuwa na mpira mbovu usiovutia kabisa!

Waliobaki ma mpira wao ni Liva, Toten na City kwa mbali.

Nimeamua Bora niandalie Movie kuliko live match ya timu hizi.

Man U ina improve, niamini mimi kwanza usajili anaoufanya ole ni wa kipekee hajasajili galasa hata moja hadi sasa na anawachezaji wengi Makinda, hivyo timu imeanza upya from the scratch!
 
Mie nilishaacha kuangalia game zetu za arsenal toka alivyoanza kuboronga Mr. Bean Wenger!

Si Arsernal tu, hata Man na, chelsea, wamekuwa na mpira mbovu usiovutia kabisa!

Waliobaki ma mpira wao ni Liva, Toten na City kwa mbali.

Nimeamua Bora niandalie Movie kuliko live match ya timu hizi.
tangu Mourinho aende Spurs, timu ile inacheza kama Abajalo ya Sinza!
 
Tz ina watalaam wengi wazuri wa soka ila cha ajabu ligi yetu na timu yetu ya taifa ni mbovu hakuna mfano.
 
Back
Top Bottom