Machifu na wakuu wa makabila nchini ni machawa pro max. Hata historia inawasuta baadhi

Machifu na wakuu wa makabila nchini ni machawa pro max. Hata historia inawasuta baadhi

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Kwa mfano anatoka Makamu Mwenyekiti wa (Chanzo Cha Matatizo) CCM kwenea Ntwara, akifika huko anasimikwa uchifu, akija mwenyekiti wa hicho kijiwe naye anasimikwa uchifu.

Mara utasikia wazee na machifu wa Songwe wamemsimika uchifu mkuu wa mafisadi huku wakimpa sifa kem kem.

Numejiuliza, taratibu za kupata mkuu wa machifu ama mkuu wa kabila fulani zimekuwa holela namna hii? Tunajua ili mtu awe chifu, kwanza lazima awe mzaliwa wa kabila ama ukoo husika, pili ajue mila, desturi na taratibu za kabila husika hususan miiko na maadili ya jamii husika.

Anapaswa kuwa na nguvu ya ziada inayounganisha imani na matumaini ya jamii hiyo.

Sasa hawa machifu waliojisimika kwa hila wamekuwa wanagawa gawa uchifu kama zawadi kwa wanasiasa wakiamini watafaidika kiukwasi na hulka hiyo. Wengi wa hawa machifu waliingia kwa hila during German colonialism, waliingizwa uchifu ili kuwabomoa na kuwafuta machifu wa kweli na haki kwa jamii husika. Wale wote walioisaliti jamii na kabila zao kwa kuwauza machifu waliokuwa wanapambana kutotawaliwa, walizawadiwa uchifu.

Tukubali kwamba, usaliti dhidi ya jamii huzalisha maafa kwa jamii husika.

Toka lini Mkojani akatawala ziwani? Toka lini wa Ziwani akatawala milimani?

Gete gete, tugende baghosha
 
Tukubali kwamba, usaliti dhidi ya jamii huzalisha maafa kwa jamii husika.

Toka lini Mkojani akatawala ziwani? Toka lini wa Ziwani akatawala milimani?
Una hoja mkuu.

Uchief wa kupeana ni usanii tu.
 
Una hoja mkuu.
Inasikitisha kuona tunaishi kama manamba ndani ya nchi huru.

Mtu hajui ABC za ukoo na kabila halafu anatawaza uchifu. Tena wanajua uchifu unarithishwa kizazi kwa kizazi, lakini leo wanampa huyu, kwesho wanampe yule ilimradi wauze sura kwenye picha.
 
Inashangaza sana hawajaacha tu hio asili ya uchawa
 
Inasikitisha kuona tunaishi kama manamba ndani ya nchi huru.

Mtu hajui ABC za ukoo na kabila halafu anatawaza uchifu. Tena wanajua uchifu unarithishwa kizazi kwa kizazi, lakini leo wanampa huyu, kwesho wanampe yule ilimradi wauze sura kwenye picha
Hayo huwa ni maigizo tu na wanasiasa wanapitia humo humo kujikosha kwa raia.
 
Wengi wa hawa machifu waliingia kwa hila during German colonialism, waliingizwa uchifu ili kuwabomoa na kuwafuta machifu wa kweli na haki kwa jamii husika. Wale wote walioisaliti jamii na kabila zao kwa kuwauza machifu waliokuwa wanapambana kutotawaliwa, walizawadiwa uchifu....
Fact.

Taratibu itaeleweka.
 
Mara utasikia chifu hangaya, mara chifu mkomile, mara chifu msofe, huko kote ni kujikombakomba kwa wanasiasa tu. Hizi regime za kichifu ni za kipuuzi tu toka zama za ukoloni
 
Mara utasikia chifu hangaya, mara chifu mkomile, mara chifu msofe, huko kote ni kujikombakomba kwa wanasiasa tu. Hizi regime za kichifu ni za kipuuzi tu toka zama za ukoloni
Wengi walisaini mikataba ya kuuza ardhi zao kwa wakoloni na wengi walishiriki kuuza watumwa yaani ndugu zao kuwauza kwa slave riders
 
Back
Top Bottom