Macho yako yanaona kama mimi? Mimi naona kama DSM fursa za kupiga pesa ni nje nje

Soma mpaka mwisho wa niliyoyasema. Inasikitisha mkongwe kama wewe kukurupuka na kufuata mkumbo.
Mwisho umesema usahihishwe, au sivyo?

Hakuna njia bora ya kusahihishwa kwenye biashara kama kuifanya wewe mwenyewe

Biashara siyo kitu "stagnant", biashara ni "dynamic", kama kucheza ngoma, midundo yake ndiyo inakupa timing ukatike vipi.

Ingia uwanjani ukatike halafu utavyotunzwa ndivyo utavyoelewa ulifanya sawa au si sawa.

Jifunze kusoma na kuelewa unachokisoma.

Kanisome tena kwa utuvu halafu jifunze kusafisha utumbo uliokuja nao.
 
mvuv

Mkuu naomba fanya risechi ya kutosha ,,umeandika mchele dar ni 2700 hyo bei ipo dar maeneo gan?* nmetembea masoko ya ilala,tandika,tandale nmekutana na mchele mpaka wa 1500
 
Kuna usafiri wa wewe mwenyewe, pakufikia(Accommodation) kwa siku kadhaa, kula kwa siku kadhaa
Acha woga, mwenzio kafanya utafiti, wewe fungua macho na kuchangamkia FURSA , Dar kuna nafasi ya kuchanua kimaisha kupitia biashara. Tubadilike watz tuondoe woga
 
Mzee baba kimahesabu hesabu zako hazijabalance, mzani umeegamia upande mmoja hesabu zako zina Profit pekee hazina loss account. Mchanganuo huu unahitaji kujua changamoto pia za biashara husika na namna ya kuikuza biashara yenyewe iwe kubwa! mvuv
 
Shukrani kwa mchango wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…