Machozi ya Mkizi

Masokotz

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2018
Posts
3,713
Reaction score
6,121
1
Amani kwenu Nyote,Na Utukufu kwa Muumba
Yeye Aloumba Vyote,Na Kuvipatia Unyumba
Kwake Vyarudi Vyote,Hata visivyo unyumba
Machozi ya Mkizi,Huoshwa na Bahari

2

Maisha Masikitiko,Mtiririko wa Matatizo
Wakati mwingine Vituko,Utafikiri ni Maigizo
Popote pale Uliko,Uitafutapo tuzo
Machozi ya Mkizi,Huoshwa na Bahari
3
Kili mja ni chake,Imemganda Huzuni
Atafuta kilicho chake.Aondokane na Uduni
Kila mtu na wa kwake,Aso wake wa huzuni
Machozi ya Mkizi,Huoshwa na Bahari

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…