binti kiziwi
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 11,201
- 28,642
Nilienda wilaya fulani, nikachukua hotel karibu na highway, ni barabara kubwa na ina mitaro mipana. Sasa kwakuwa tax huwa inanichukua hotelini, i mean natoka mlango wa hotel namkuta dereva tax ananisubiri napanda nasepa na kurudi hivyo hivyo nashuka tu mlangoni, siku kadhaa...
Siku moja nimechelewa sana kurudi nimerudi saa tano usiku nilijisemea muda huu dereva tax atakuwa kwake kalala simpigii anifuate, nikaulizia daladala nikapanda wakanishusha kituo karibu na hotel, natakiwa kuvuka barabara ndio niende hotelini, basi ile nasubiri magari yaishe ili nivuke nikawa naziangalia taa za magari (huwa nikipigwa na taa machoni naona giza) basi ile magari yameisha tu nikafanikiwa kuvuka kwa speed kidogo kumbe macho bado yanagiza upande wa pili nikawa sioni vizuri nikabiringita nikaingia mtaroni moja kwa moja [emoji3]. Dah bahati mtaro haukuwa mchafu, nikanyanyuka angalia huku na kule hakuna mtu zaidi ya magari yanayopita barabarani, nikajikung’uta nikavua viatu maana nilishindwa kupanda ukuta wa mtaro.... huyo nikarudi zangu hotelini, nilivaa minskirt miguu ilikuwa wazi nikachunika kiasi kwenye miguu.
Sasa kesho yake dereva kanifuata kama kawaida, akaniuliza jana ulirudi saa ngapi nikamwambia mapema tu ila niliona nisikupigie, akanambia jana tulikuwa tumepaki mahali fulani tukakuona umebiringita umeingia mtaroni dah! Niliona aibu sana maana nilijua hakuna mtu aliyeniona jana na hata kama wameniona watu wanaopita na magari hawanijui, kumbe niliona nilivobiringita miguu juu [emoji3]
Siku moja nimechelewa sana kurudi nimerudi saa tano usiku nilijisemea muda huu dereva tax atakuwa kwake kalala simpigii anifuate, nikaulizia daladala nikapanda wakanishusha kituo karibu na hotel, natakiwa kuvuka barabara ndio niende hotelini, basi ile nasubiri magari yaishe ili nivuke nikawa naziangalia taa za magari (huwa nikipigwa na taa machoni naona giza) basi ile magari yameisha tu nikafanikiwa kuvuka kwa speed kidogo kumbe macho bado yanagiza upande wa pili nikawa sioni vizuri nikabiringita nikaingia mtaroni moja kwa moja [emoji3]. Dah bahati mtaro haukuwa mchafu, nikanyanyuka angalia huku na kule hakuna mtu zaidi ya magari yanayopita barabarani, nikajikung’uta nikavua viatu maana nilishindwa kupanda ukuta wa mtaro.... huyo nikarudi zangu hotelini, nilivaa minskirt miguu ilikuwa wazi nikachunika kiasi kwenye miguu.
Sasa kesho yake dereva kanifuata kama kawaida, akaniuliza jana ulirudi saa ngapi nikamwambia mapema tu ila niliona nisikupigie, akanambia jana tulikuwa tumepaki mahali fulani tukakuona umebiringita umeingia mtaroni dah! Niliona aibu sana maana nilijua hakuna mtu aliyeniona jana na hata kama wameniona watu wanaopita na magari hawanijui, kumbe niliona nilivobiringita miguu juu [emoji3]