Mada maalum kwa wanandoa

Mada maalum kwa wanandoa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Ni siku nyingine tena imepita, tumerudi salama majumbani mwetu, kuungana tena na wapendwa wetu, familia na watoto pia. Baadhi yetu hatujarejea, tuko mishe na viti virefu, baadhi tuna sababu za msingi na nyumbani wanafahamu na tumewapa taarifa, wanatusubiri watupokee kwa upendo, kwa furaha kwa bashasha kuu.

Baadhi hali ni tofauti, hatungependa kuchelewa nyumbani, tungependa tuwahi, tuungane na familia, tuimalize jioni kwa furaha kuu kabla hatujaungana kwa dinner na maombi ya usiku, lakini hali ni tofauti. Tunapoteza muda nje saa zisogee ili tukifika tu ni chakula kuoga na kulala, tunakimbia kero na malumbano yasiyoisha.

Ndoa haina furaha, ndoa haina amani, majuto ni mengi mno moyoni. Kila mmoja anajutia kivyake, hakuna upendo tena, hakuna kuaminiana tena, ni mwendo wa kutuhumiana na kuviziana. [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]Baba ana chumba chake, mama naye ana chake, ama la chumba ni kimoja lakini kila mmoja ana kitanda chake.

Hakuna upendo, hakuna sharing, hakuna majadiliano ya changamoto, ya maumivu ya kushinda na kushindwa, ya kutiana moyo na kufarijiana, kila mtu kivyake, kila mtu na lwake. [emoji144][emoji144][emoji144][emoji144][emoji24][emoji17][emoji17][emoji17]

Karibuni wanandoa wote, ni mada ya kupeana faraja na kushare maumivu. Itambueni nguvu ya kuongea, kuongea hupunguza maumivu mengi, kupitia mada hii utajiona hauko pekeyako na pengine utaona kuwa kumbe wewe una nafuu kubwa ukisikia ya mwenzako. Jisikie huru ufunguke.

Funguka kwenye ndoa yako iliyoumizwa na kujeruhiwa sana, iliyotiwa vidonda na makovu ya kila aina;
~ Ya usaliti,
~ Ya kuchapiwa,
~ Ya kusingiziwa,
~ Ya kunenewa mabaya,
~ Ya kudharauliwa kutukanwa na kudhalilishwa.

~ Funguka upate nafuu,
~ Funguka upate faraja,
~ Funguka upunguze sumu mwilini,
~ Funguka upate kupona sasa.

Karibuni wanandoa wote.

Jr[emoji769]
 
Kiupande wangu nahisi kuongea na mhusika ni vizuri zaidi kuliko kusema hapa japo hatuonani wala kuwajua wenza wetu ni kama kuanika siri za ndani nje

Binafs ndio nimeingia huku, Allah atuzidishie mapenzi na uvumilivu
 
Nadhani kwenye ndoa mkiwa mnatoana 'out' inapunguza mambo mengi sana,sasa unakuta bi. mkubwa alipokuwa binti 'out' zilikuwa nyingi,ameanza kuchuja (mtoto 1,2,3 n.k) hakuna 'out' hapo lazima utengeneze bomu tu.Jamani tuende nao 'out' ata kama wamezeeka,itasaidia sana.
 
Kila la kheri wenye ndoa.

Mahisiano niliyopitia nyuma yalinifanya nikafunga mlango wa ndoa, ila mahusiano ya sasa na Dadii ni paradiso na tukigombana tunaambiana ukweli waziwazi usoni bila kuoneana aibu.

Kesho yake tunakumbatiana kama kawaida, Mahaba yetu matamu sitamani ndoa tena....
 
Kwenye ndoa kuna mambo mengi sana.
Kuna wakati mkeo anakuwa rafiki yako.
Wakati mwingine anakuwa adui yako.
Wakati mwingine anakuwa boss wako vice versa is also true.

Wakati mwingine mume unakuwa polisi na mke mfungwa vice versa is also true
Wakati mwingine chumbani kunageuka ulingo wa masumbwi na watoto washangiliaji

Wakati mwingine mnakuwa majirani kila mtu hajui kinachoendelea kwa jirani yake

Wakati mwingine mnakuwa mtu mmoja indivisible being

Wakati mwingine mmoja anakuwa Mtoto na mwingine ni mzazi.

Na haya ndiyo huwa maisha yetu ya kila siku ndoani.

Asikwambie mtu hakuna Kitu kinachoongeza heshima na hadhi ya mtu kama ndoa.

Onyo. Usiulizie matumizi ya hela za mkeo jifanye huoni yanayoendelea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila la kheri wenye ndoa.

Mahisiano niliyopitia nyuma yalinifanya nikafunga mlango wa ndoa, ila mahusiano ya sasa na Dadii ni paradiso na tukigombana tunaambiana ukweli waziwazi usoni bila kuoneana aibu.

Kesho yake tunakumbatiana kama kawaida, Mahaba yetu matamu sitamani ndoa tena....
[emoji144][emoji144][emoji144][emoji144][emoji144]

Jr[emoji769]
 
Back
Top Bottom