Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mkuu mim naomba unipe mwanga. Kuna gari Vw Touran ya mwaka 2007, 1380cc, CIF yake ni US$3,225 hadi bongo. Je hii itaweza kugharimu kiasi gani kwenye mambo ya kodi, clearance, exercise duty na mengine kiujumla hadi kukabidhiwa ufunguo. Natanguliza shukrani kwa wote jukwaani.

Hio kodi yake ni usd 2987
Hapo utaongeza usd 800 ya mambo ya clearing, port charges na registration. Chench yaeza baki hapo.
 
Msaada kwa wanaojua haya magari makubwa nataka kujua tofauti kati ya Scania highline,Scania Streamline,Na scania Topline. Doesnt matter whether ni G series au R series.
 
Ni jini La Mafuta,unaendesha huku roho inakuuma!

Zinakula kawaida tu wala sio kivile kama watu wanavyosema, ujue wakati mwingine ulaji wa mafuta unatokana na uendeshaji wa dereva, sijakataa kama inakula mafuta hapana, kula inakula lakini si kama watu wanavyoeneza.
 
Zinakula kawaida tu wala sio kivile kama watu wanavyosema, ujue wakati mwingine ulaji wa mafuta unatokana na uendeshaji wa dereva, sijakataa kama inakula mafuta hapana, kula inakula lakini si kama watu wanavyoeneza.

Ni kweli kabisa/upo sahihi..
 
Wadau,

Naombeni ushauri kuhusu hii gari,

Mazda Tribute

Nahitaji kujua kuhusu uimara wake

Upatikanaji wa spare parts

Changamoto zake katika matumizi

Fuel consumption

03.jpg02.jpg01w.jpg
 
Hivi kwann malor huwa yanainua yale matair ya nyuma? Na huinuliwa kwa mfumo gani?
 
Wakuu kuna wenye magari wanapata shida sana na berti zao walizofunga kwenye magari..Kwa ushauri wa bure kabisa na mahali ukatakapoenda kuchukua betri wasiliana nami kwa namba 0757848484
 
Hivi kwann malor huwa yanainua yale matair ya nyuma? Na huinuliwa kwa mfumo gani?

Idea nzima ya kunyanyua matairi ni kupunguza matumizi ya matairi hayo kipindi ambacho gari halijabeba mzigo, kumbuka malori yana matairi Mengi si kwa ajili ya urembo ,ni kutokana na mizigo mizito yanayobeba. ,ilikiwa tupu kunakuwa hakuna umuhimu wa kuyatembeza yote,

Mifumo ya kunyanyua matairi iko miwili , kutegemeana na aina ya suspension zilizotumika , kwa steel suspension mfumo unaotumika ni hydraulic , kwa air suspension mfumo unaotumika huwa ni wa electronic solenoid ambayo kimsingi huwa ni hewa . kwa bahati mbaya sina uwezo wa kuielezea humu jamvini, ila ni mifumo rahisi Sana Kama unaielezea kwa vitendo .
Kwa kuongezea tu , kuna aina mbili za kunyanyua matairi,mid lift na tag axle
mid lift , hii hunyangua tairi za mbele ya diff,
Tag axle ,hunyanyua tairi za nyuma ya diff,
Mid lift huwa inanyanyua tairi ikiwa empty tu, Tag axle huwa inanyanyua hata Kama Ina mzigo , idea ni kuongeza mkandamizo kwenye diff, Kama itatokea kuteleza .nk, na ndio sababu tag axle huwa zinatumika Sana kwenye rough roads.
 
Chukua hizi corolla carina Ti na akina Duet na cami hizi nyingine za kisasa kina Porte na Siensta ni majanga

Nina swali la ufahamu hapo mkuu mshana jnr na wengine wenye majibu. Kwa kuangalia tu kwa macho na hata kwa mbali waweza tofautisha kati ya carina ti na si? Na je zina tofauti gani kitaalam? Nauliza kwa sababu nilienda kutafuta taa ya carina ti kwenye duka la spea used na gari nilikuwa nalo, nilipomwuliza muuzaji nahitaji taa ya carina ti akaniuliza gari ndo ile?, akasema ile siyo ti ni si wamepiga chata tu.... Kweli sijajua hadi leo hii yangu ni ti au si. Kwenye kadi ya gari imeandikwa carina ti.
 
Nina swali la ufahamu hapo mkuu mshana jnr na wengine wenye majibu. Kwa kuangalia tu kwa macho na hata kwa mbali waweza tofautisha kati ya carina ti na si? Na je zina tofauti gani kitaalam? Nauliza kwa sababu nilienda kutafuta taa ya carina ti kwenye duka la spea used na gari nilikuwa nalo, nilipomwuliza muuzaji nahitaji taa ya carina ti akaniuliza gari ndo ile?, akasema ile siyo ti ni si wamepiga chata tu.... Kweli sijajua hadi leo hii yangu ni ti au si. Kwenye kadi ya gari imeandikwa carina ti.

Kuna wakati uzoefu unahusika na kuna wakati ni total misleaded kadi huandikwa kilichomo kwenye gari kama ni Ti ni Ti tu labda iwe ni typing error ya TRA kitu ambacho ni kigumu mno kutokea
 
Msaada kwa wanaojua haya magari makubwa nataka kujua tofauti kati ya Scania highline,Scania Streamline,Na scania Topline. Doesnt matter whether ni G series au R series.

Tofauti hapo ni cabins na bei kama unanunua lori jipya. , ie, Kama unanunua used kwa ajili ya kazi zako , nunua cabin yoyote unayoona budget yako inaweza,

Top line ni kwa ajili ya safari ndefu kwa madereva Wawili , zina vitanda viwili, makabati Mengi kwa ajili ya kuhifadhia vitu , reserve kwa ajili ya kuweka freezer ,cofee maker na microwave.

Highliner hii ni ya pili kwa ukubwa inatumika katika mazinyira Kama ya top liner ila Ina nafasi kidogo.

Stream liner hii hasa sio cabin type , ila ni jinsi gani cabin inawezo wa kupenyesha Upepo ili kupunguza ukinzani , na hivyo kupunguza matumizi ya mafuta, kwa maana hiyo streamline inaweza kuwa Highline , top line au normal cabin.
 
Back
Top Bottom