Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Hii ya kwangu inawaka muda wote,yaani ukiwasha engine tu baada ya dk 10 tu taa inawaka.
Kafanye diagnosis tafadhali hizi gari hazitaki guess work na kama ni timing belt na taa inawaka muda wote basi inakaribia kwisha kabisa sasa
 
Wakuu.

Gari yangu aina ya mark II grand yenye engine ya 1G-FE vvt-i beams 2000 ina tatizo la kuniwashia taa ya "check engine" tatizo linaweza kuwa ni nini?

Hivi engine oil ikipungua kidogo inaweza kuwa ndo kisababishi?

Msaada tafadhali.
mashine zipo mkuu kuna ishu nyingi sana zinazoweza kusababisha taa hiyo kuwaka.
mm naweza kukwambia ni oxygen sensor.
lkn unachotaka tukifanye ww ni ubashiri tuu mkuu.halafu kibaya umesema tuu taa inawaka lkn je hakuna tatizo jingine hujagundua tofauti yoyote?
 
Ok asante nilichofanya ni guess work bila kuzingatia model ya gari
mm ndio maana nasema kila siku unanunua gari ya milion kuanzia 5 unatumia simu ya kuanzia laki 3 ambayo inauwezo wa kudiagnosis gari yako cha kununua ni ile obd 2 blue tooth ambayo bei yake ni ndogo sana haifiki hata laki 1 au ukanunua code leder ambayo nayo haifiki hata laki na nusu au laki kwaajili ya kufanyia chekup gari yako.vi sign vidogo vidogo ukatatua.ukija kuuliza hapa iwe ni maswali je lambda sensor au knock sensor or throttle sensor au sijui catalic converter ndio kitu gani na je ipo wapi au kwenye gari yangu.au unaweka fault code na kuomba msaada wa fafanulio.
 
Naomba mnisaidie kujua utofauti wa Timing Belt na Fern Belt. Alafu izo zote zinabadirishwa baada ya kilometer ngapi?
 
Naomba mnisaidie kujua utofauti wa Timing Belt na Fern Belt. Alafu izo zote zinabadirishwa baada ya kilometer ngapi?
Nazungumzia kwa uzoefu hiyo timing belt ndio inayofanya engine ifanye kazi na feni belt ni kwa ajili ya feni ya mfumo wa kupoza joto kwenye engine na kiyoyozi
Timing belt original hubadilishwa baada ya km laki moja, feni belt sina ujuzi kivile lakini ikichoka utajua tuu
BTW gari za kisasa zina sensors kwenye kila kitu hivyo kwenye shida itakupa warning
 
Naomba mnisaidie kujua utofauti wa Timing Belt na Fern Belt. Alafu izo zote zinabadirishwa baada ya kilometer ngapi?
timing belt ni belt ambayo huwa inaunganisha mzungusho kati ya camshaft na crank shaft na inategemeana na aina ya gari kama ni gari ya disel basi huwa inazungusha pia fuel pump.hii belt huwa ndani ya front cover kuiona ni mpaka ufunguwe front cover.

lakini fen belt yenyewe huwa izungusha otonelta,water pump,stering power,compressor hapo inaweza ikawa 1 au 2 au hata 3 inategemeana na aina ya gari na kuna vingine hapo vinaweza kupungua pia au kuongezeka kutokana na aina ya gari.

juu ya ubadilishaji ni baada ya kutembelea kilomita laki 1 hii ni timing belt lkn nayo inategemeana ni gari aina gani zingine km zikikaribia tuu huwa inaku warring kuna taa huwa inawaka.

fen belt hazinaga mda unapofanya servirce basi yakupasa ukague kma zimeanza kuchoka unabadili
 
honda_check01.jpg
honda crossroad anaye zijua hizi gari matatizo yake
 
Mkuu Lege naomba msaada wako.
Gar yangu inashida ambayo nimeshindwa kugundua ni kitu gani, kuna muda na muda tena mara chache.
Nikizima kuja kuwasha inazingua mpaka ni boost. Nikahisi terminal haziko nimebadili lakini bado.
Na dalili za kutokea hivyo huwa inaonyesha. Kuna saa kama natembea nimewasha taa mwanga unakuwa una vibrate hata kwenye dashboard inaonyesha mwanga wake hautulii na sterling inakuwa ngumu. Ila nikitembea tembea inapotea.
Na hili tatizo limeanza siku ambayo nili park pale tazara na gari kugoma kuwaka mpaka nikamuita fundi wangu anitolee sterling lock ili tulitoe maeneo hayo kwasababu walituambia watu pale kuwa key less car zinasumbua kuwaka maeneo ya Tazara mpaka zitoke hapo.
Na kweli tulitoka pale hadi tmk na tulipo washa gari ikawaka na fundi kurudishia ile lock. Lakini tatizo likaanza siku hyo hyo mara sterling kuwa ngumu saa nyingine mara zikizma kusumbua kuwaka.
Sasa inanipa tabu kiongozi. Msaada wako naamini utakuwa ushakutana na shida kama hizi.
Natanguliza shukrani mkuu Lege.

Mkuu, sijajua ni gari gani unayo lakini kama gari yako inatumia "BELT" moja kuzungusha Power Steering, Altenator na AC Compressor basi inaweza kuwa belt ndio ishu. Maana yangu ni kwamba belt ya gari haizunguki vizuri kuzungusha alternator ili ichaji betri, na kwamba pia haizungushi steering hydrolic...
 
Kumekuwa na mada nyingi kuhusu mambo yote yahusuyo magari, nikaona basi na sisi tuwe na Uzi huu ambapo habari zote zihusuzo magari kuanzia kuchagua, kuagiza, kuuza, kubadili nyaraka, matengenezo utunzaji na kadhalika.

Watu wengi wametapeliwa kwenye mauzo na manunuzi, kwenye nyaraka, kwenye vipuri kwenye matengenezo na hata matumizi.

Kwa Uzi huu basi kila mwenye ujuzi, uzoefu, ushauri au mwenye maswali na tatizo lolote linalohusiana na magari hapa ndio pawe uwanja wake

Karibuni sana

Ushauri: Jinsi ya kununua gari iliotumika ndani ya Tanzania


Tahadhari kali kwa nyote mlio na magari binafsi; chunga sana na waambie wengine!

USHAURI: Ununuaji wa magari...

View attachment 225786
Hi, nataka kununua gari toyota ISIS cc 1998 D4 engine. Tafadhari mwenye uzoefu nayo na ushuri pia, nini utafunaji wake wa mafuta nk.
 
Hi, nataka kununua gari toyota ISIS cc 1998 D4 engine. Tafadhari mwenye uzoefu nayo na ushuri pia, nini utafunaji wake wa mafuta nk.
Check na Lege atakufafanulia vizuri,ni D4 ni engine nzuri na za kisasa ila mafundi wengi hawako familiar nazo.
 
sio kweli mkuu .kwenye hiyo gari aliyoitaja hakuna kitu kama hiyoo
Lege naomba ufafanuzi nataka nunua gari Toyota ISIS cc 1998 D4 Engine, ushauri tafadhari juu ya gari hii. Au Mazda Primacy MPV cc 2000. All this is 7 seat Family size MPV.
 
Wakuu engine ya gari yangu ilikuwa inagonga kwenye piston nikaamua kubadilisha engine nilinunua nyingine ya mtumba ambayo mailage yake azidi 40,000km.

Sasa shida yangu ilikuwa kuchange mailage ya gari ili iendane na engine.
 
inawezekana upo wapi na je gari yako ni aina gani na inatumia dashboard /cluster ya digital or analog??
 
Back
Top Bottom