Mada maalum ya ndege toka FB

"VITA GHARAMA, VITA HASARA"

Ndege ya serikali ya Sudan #Ilyushin Il-62M yenye usajili [emoji1232] ST-PRA imeteketea kwa moto.

Picha za satelaiti zilizokusanywa asubuhi ya jana (Aprili 17, 2023) huko #Khartoum, #Sudan, zinaonyesha uharibifu unaotokana na mapigano yanayoendelea kati ya makundi hasimu ya kijeshi ya Sudan.

Pichani ni Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa #Khartoum ambapo angalau ndege 14 zimeteketea na nyingine nyingi kuharibiwa.

[emoji328]Picha:
nav-nav
Maxartechnologies
 
Nchi mbalimbali ikiwemo Marekani, Ufaransa na Uingereza zinaendelea kuondoa raia wake huko #Khartoum nchini Suadan kufuatia mapigano yanayoendelea.
Miongoni mwao pia wapo Wareno, Waitaliano, Wapoland, Ireland, Mexicans, Venezuela, Colombia na Argentina, Japan, pamoja na Wahispania.

Ndege mbalimbali za mizigo za kijeshi Boeing C-17 globemaster-ii na Lockheed C-130 Hercules na ndege nyingine zimeonekana kutua #Djibouti karibu na mpaka wa Sudan kama sehemu salama la kuanzia zoezi la uhamishaji raia wao.

[emoji328]&Chanzo:
@MinisterioDefensa/tweeter
bbc
@TheScotsman
@iNews
 
Jibu la chemsha bongo:
Pichani ndege mkubwa ni Tai au 'Eagle' na anawakilisha ndegevita aina ya F-15 'Eagle' chini.
Ndege wadogo wanne ni shorwe au 'Sparrow' na wanawakilisha makombora ya anga ya masafa ya kati aina ya AIM-7 'Sparrow'
Picha ya nyoka 'sidewinder' inawakilisha kombora za anga za masafa mafupi aina ya AIM-9X 'Sidewinder'

Pongezi kwa wote waliojaribu.
Angalau mmoja ametaja F-16 'Falcon' badala ya F-15 'Eagle'
 
Huu ni mfumo wa chumba/viti vya kufyatua nje marubani (Ejection Seat) katika ndege ya kijeshi ya General Dynamics F-111A 66-0017, baada ya kupata hitilafu.

Meja “Sandy” Marquardt na Kapteni Joe Hodges wakiwa bado wapo ndani ya chumba baada ya kufika ardhini.

Mfumo huo hutumia muamvuli (parachute) kufyatua marubani nje ya ndege ili kuweza kufika chini salama oale inapopata hitilafu au kulengwa na adui.
 
NDEGE MPYA YA KIJESHI URUSI YAANGUKA NA KUUA WATATU

***
Kama ulipitwa kutazama A to Z kuhusu uzamiaji ndege, hatari, vifo pamoja na uchambuzi mdogo kuhusu ndege ya Boeing C17 Globemaster-iii kupitia video, bofya link ifuatayo:
***

Ndege mpya ya kijeshi ya Urusi #Ilyushin Il-112V imeonekana kuwaka moto injini ya kulia wakati wa majaribio kisha kuanguka karibu na #Moscow Jumanne, vyombo vya habari vya Urusi viliripoti, ikinukuu United Aircraft Corporation.

Ndege hiyo ilikuwa na watu watatu ndani wakati wa ajali.
Taarifa iliyowekwa kwenye Twitter na waundaji wa ndege hiyo #UAC ilisema hakuna aliyenusurika.

Watu hao watatu walikuwa mhandisi wa majaribio ya ndege #NikolaiKhludeyev, rubani wa majaribio #DmitryKomarov, na rubani wa majaribio #NikolaiKuimov, shirika la habari la serikali la Urusi TASS liliripoti.
UAC imesema kuwa itachukua hatua muhimu kusaidia familia za marehemu.

UAC iliwaambia waandishi wa habari Jumanne kwamba moja ya injini za ndege hiyo iliwaka moto, TASS iliripoti.

"Kulingana na taarifa za mwanzo na video iliyonasa mubashara tukio hilo inaonesha ajali ya Il-112V ilitanguliwa na moto kwenye injini ya kulia'.

Ndege hiyo ilianguka ilipokuwa ikikaribia kutua karibu na uwanja wa ndege wa #Kubinka.
Kisha ikalipuka baada ya kupiga chini.

Il-112V ni ndege nyepesi ya usafirishaji wa kijeshi inayotengenezwa na Ilyushin Aviation Complex, ambayo ni sehemu ya United Aircraft Corporation.
Ndege inaweza kubeba hadi tani tano za wa wafanyakazi, silaha, au mizigo mingine.

Ndege hiyo mpya imekusudiwa kuchukua nafasi ya ndege za zamani za Antonov An-26.
Urusi imekuwa ikifanyia kazi ndege hiyo tangu 2014 na ilipaa mara yake ya kwanza mnamo Machi 2019 na bado ipo katika muendelezo majaribio.

Imeripoti,
#Insider
 
Ndege ya mizigo #Astral #Aviation Boeing 727-200 yenye usajili EY-627 zamani 5Y-MWM ya 1976 ilipitiliza mwisho wa barabara ya kuruka/kutua ndege namba 13 huko Juba Sudan Kusini na kusimama kwenye ardhi laini.

Inasemekana ndege hiyo ya mizigo iliwasili kutoka Paloch kwa ajili ya uokoaji wa Wasudan 300 wana9kimbia mapigano.

@aviationsafety/tweeter
 
Kwa mujibu wa Kamusi, tafsiri ya neno la kiingereza 'CAPTAIN' kwa lugha ya kiswahili ni 'NAHODHA'

'NAHODHA' ni CHEO au KIONGOZI, na mara nyingi hupewa mtu anaye ongoza kikosi cha jeshi, Meli, Ndege, Timu za michezo n.k
(Be the captain of a Ship, Aircraft, Military segment, or Sports team).

1>'Nahodha' wa Timu za michezo mara nyingi unaweza kumtambua kwa kuvaa kidani mkononi chenye alama 'C' (Captain)

2>'Nahodha' wa Meli mara nyingi unaweza kumtambua kwa kutazama alama ya vistari vinne begani au kwenye mikono ya Suti pamoja na alama ya Nanga (4 stripes/Bars & Anchor).

3>'Nahodha' wa kikosi cha Jeshi (la kisasa) mara nyingi unaweza kumtambua kwa kutazama alama ya nyota tatu begani.

4>'Nahodha' wa Ndege mara nyingi unaweza kumtambua kwa kutazama alama ya vistari vinne begani au kwenye mikono ya Suti.

#AdminMkuu
 
Ndege nyingi zimeonakana kuchukua tahadhali ya kupita mbali na anga ya Sudan kiujumla.
Jana ndege nyingine ya Emirates, Boeing777 "EK248" iliyokuwa ikitoka Rio De Janeiro kuelekea Dubai, pia ilibadili njia na kutua Addis Ababa kabla ya kuendelea na safari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…