Mada maalum ya ndege toka FB

Mada maalum ya ndege toka FB

Hii sio Taswira nzuri kwenu Air Tanzania
 
de12224c-8d4b-41ec-9de6-261955e87b53.jpeg
 
JE, NDEGE INARUDI NYUMA?

Ndege nyingi za sasa zina mfumo wa kurudi nyuma #reverse' ambao mara nyingi hutumika kupunguza kasi wakati ikitua (#Braking).

Kwa baadhi ya ndege za 'Mapangaboi' #Propeller hutumia panga zake kubadili umbile (#angle) hivyo badala ya kuvuta hewa kwenda nyuma inasukuma kuelekea mbele na kusababisha ndege kupunguza kasi yake pale inapotua.

Hali kadhalika na kwenye injini zenye mfumo wa #Jet huwa zinafungua injini katikati na kubadili uelekeo wa hewa inayosukumwa nyuma kuvuja na kulazimishwa kuelekea mbele.

Baadhi ya Injini za mfumo wa 'jet nyingine zinafungua vimilango vyake vidogo katikati au nyuma ya injini.

Ndege nyingi kubwa zina mifumo mitatu ya kupunguza mwendo #braking ikiwemo

1>#Reverse' ya Injini au #Reverse_Thrust

2>'Brake' za matairi na

3> #Ground_Spoilers au #Speedbrake' ambazo ni bapa zinazo nyanyuka juu ya mbawa.

Hivi vyote mara nyingi hufanya kazi kwa pamoja ili kupunguza kasi ya ndege inapotua ili kusimama haraka kwakuwa hutua na kasi kubwa sana.
Kasi ya kutua ndege kama #MD11 ikiwa imejaa mzigo hata Gari yako yenye speed 260km/h haifukuzi.

Brake zote za kukinzana na upepo {spoilers na reverse thrust} husaidia kutozipa mzigo mkubwa 'brake' za matairi ambazo huweza kupasua tairi, kuharibika, kuwaka moto au mda mwingine kuteleza kama barabara #Runway ikiwa imetuama maji endapo kama zitatumika pekee bila msaada wa #brake' nyengine.

Licha ya kukinzana na upepo juu ya mbawa, 'spoilers/speedbrake' pia husaidia kukandamiza ndege chini hivyo tairi kushika barabara vizuri wakati zinakamata 'brake kupunguza mwendo.

Sasa kwanini ndege haitumii 'Reverse' kujitoa kwenye Maegesho?
badala yake inasukumwa kurudi nyuma (#Pushback) na vigari maalumu #Tow_Truck/#Tug

1>Kuepuka kelele kali za 'reverse'

2>Kuepuka ulaji mafuta

3>Kuepuka hatari ya ndege kugongana na vitu vingine nyuma.

4>Kuepuka uharibifu wa injini kwa kunyonya taka na vumbi kwasababu upepo wa 'reverse' hutokea pembeni ya injini kwa kasi kubwa kuelekea mbele ya injini.

5> Reverse ni mfumo wa dharura ambao kiufundi haishauriwi kutumika hovyo kwasababu hewa yake inapitia sehemu za injini ambazo ni rahisi kupata uharibifu.

#Admin
Credit
#boldmethodView attachment 2620053
Kinachorudi nyuma ni ndege au mzunguko wa injini?
 
 
Nimekuwa nikisoma zaidi habari za Ndege hii iliyotengenezwa Tanzania. Nimekubali imetengenezwa Tanzania. Bado sijapata jibu kama imetengenezwa na Watanzania, na endapo utaalamu na teknolojia iliyotumika ipo mikononi mwa Watanzania. Naomba kujua.
Nawasilisha!
20241007_215437.jpg
 
Kampuni kubwa ya kutengeneza Ndege ya Embraer, imetangaza mpango wake mpya wa kutengeneza ndege ya kwanza ya Abiria inayotumia akili bandia (AI) kujiendesha ambayo haitokuwa ikiendeshwa na Rubani katika safari zake zote.

Mpango huo umezinduliwa katika hafla ya Jumuiya ya Kitaifa ya Usafiri wa Anga na Biashara huko Orlando, Florida Nchini Marekani ambapo Ndege hiyo haitokuwa na chumba cha Marubani kama ilivyozoeleka kwenye Ndege tulizonazo sasa na badala yake itakuwa na chumba kama sebule ndogo ambacho Abiria wanaweza kukaa na ku-njoy maisha wakiwa angani ( kama inavyoonekana kwenye picha ).

Madirisha ya Ndege hiyo iliyopewa jina la ‘Ndege ya siku zijazo’ yatakuwa madirisha ya kipekee kwani yatakuwa na ‘touch screen’ ili kumuwezesha Abiria kupata urahisi wa kufanikisha hitaji lake lolote kwa wakati wowote.

Haya ni maono tu ambayo ndio kwanza yametangazwa na Kampuni hii ambayo inashika namba tatu kwa utengenezaji wa Ndege Duniani baada ya Boeing na Airbus, ni maono ambayo yamekuja wakati huu ambao tayari Dunia inashuhudia Magari yanayojiendesha yenyewe yakiwa barabarani huko Marekani na kufanya shughuli za kila siku zikiwemo TAXI za kubebea abiria huko San Francisco, tazama picha zaidi hapa instagram.com/p/DA1T9pUiTjh/…
20241008_033027.jpg
 
Shirika la Ndege la Air France limesitisha safari nyingine za ndege katika Bahari Nyekundu, baada ya Rubani kuona "Kitu Kinang'aa" katika Urefu wa Juu mapema leo wakati wa Safari ya Kawaida. Kitu hicho kinaaminika kuwa kilikuwa ni Kombora la Ballisti lililorushwa na Houthis nchini Yemen, huku Ndege kadhaa zikielekezwa Kwengwa au Kuelekezwa Kwingine kufuatia Tukio hilo.

20241104_194414.jpg
 
Ripoti ya uchunguzi imehitimisha kuwa nahodha wa ndege aina ya ATR 72-600 ya shirika la ndege la Binter Canarias alifunga breki ya kuegesha ndege wakati ikiwa angani kwa sababu ilikuwa inazuia mwonekano wa picha aliyokuwa akijaribu kupiga.

Marubani hao walisahau kuachia breki kabla ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Las Palmas, Uhispania, na kusababisha uharibifu wa matairi na ringi mnamo tarehe 9 Agosti 2023.

Ndege ya Binter Canarias NT501, ATR 72-600, ilitua kwenye njia ya 03L kwenye Uwanja wa Ndege wa Las Palmas de Gran Canaria (LPA) ikiwa kwenye breki ya maegesho na kupasua tairi na ringi.

Ripoti inasema, wakiwa usawa wa futi 8000, marubani wa ndege walianza kupiga picha kwenye chumba cha marubani na katika kinasa sauti cha chumba cha marubani, nahodha alisikika akisema, "Sitaki hiyo ionekane kwenye picha"

Baada ya kufunga breki hiyo, walisahau kufungua na kusalia hadi wakati wa kutua, na kwa bahati nzuti hakukuwa na ripoti ya majeruhi katika tukio hilo.

Chanzo;
FB_IMG_1732296950058.jpg
 
Back
Top Bottom