Mada ya wanyama

Aseee hii ndo kwanza naona leo
 
Uzito wa ulimi wa nyangumi ni sawa na tembo mmoja. Katika wanyama wakubwa wa mwenyezi mungu basi nyangumi ndio mnyama mkubwa hapa ulimwenguni. Kwa wastani ukubwa wa nyangumi wa bluu ni sawa na tembo watatu mpaka wanne. Kama akikua vizuri basi urefu wake unaweza kufika futi 100 huku uzito wake ukiwa ni tani 200 au kwa kilogramu ni kg kati ya Laki moja 130 mpaka 150.

Som zaidi ⬇️
 
Kunguru ni moja ya ndege mwenye ubongo mkubwa zaidi wenye akili zaidi na ujanja zaidi. Kunguru wamebarikiwa milio 30 ambayo hutumia kuwasiliana pindi watakapo ona kuna chakula mahali.
 
Wanauwezo wa kupanga mipango ya maisha japo ukiwaona huwa na sifa ya uoga pia wakiona chakula wakila na kusaza huwa hawakiachi bali hukiifadhi kwa kukificha na kukila baadae. Hii inaonesha uwezo wa kujitambua
Wanasayansi wanasema kuwa ubongo wa kunguru ni sawa na mtoto wa miaka saba pia wengine wakasema uwezo wao wa ubongo upo sawa na sokwe.
 
Fahamu ya kuwa kunguru ukimuona huwezi mtambua huyu ni yupi yule ni yupi ila wao wanauwezo wa kukujua vizuri kuwa wewe ni juma wewe ni suma kwahiyo kam jana ulimpiga na jiwe basi anauwezo wa kukufahamu na kukuwekea kinyongo kwa muda mpaka wa mwezi mmoja.
 
Tukimuangalia ndege mwingine anaeitwa Flamingo
Huyu kajaaliwa uwezo wa kula huku kichwa chake kimegeuka chinijuu ambapo chakula chake kinapatikana katika maji yenye kina kifupi.
 
Tukimwangalia mdudu anaeitwa mende huyu ukimkata kichwa hafi kwa muda huo huo itamchukuwa siku saba kuweza kufa tena kwasababu ya kukosa chakula kwani mdomo wake upo kichwani hivyo kwasababu ya kukosa chakula kwa muda mrefu atakufa, swali ni kwanini hafi baada ya kuondoa kichwa? Jibu ni kuwa moyo wa mende haupo kichwani upo kwenye kiwiliwili chake ndio maana hata ukiondoa kichwa chake basi ataendelea kuishi kwa kipindi cha muda flani.
Usahihi
Sababu ya Mende kuendelea kuishi kwa muda baada ya kukatwa kichwa inatokana na njia zake upumuaji kuwa mwilini badala ya kichwani kama viumbe wengine wengi
 
Kuna kiumbe maarufu zaidi ambae anapendwa kutumia na binadamu anaitwa Mbwa. Mbwa anauwezo wa kunusa mara laki moja ya binadamu jambo hili limepelekea binadamu kuweza kutumia mbwa katika kazi mbalimbali kama utafutaji wa mabomu ya kutega na mambo mbali mbali mengi zaidi.
 
Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…