Mada ya wanyama



Vunjajungu ni mdudu hatari sana kwa wadudu, mijusi na ndege wadogo. Huwa anakamata chakula na miguu yake ya mbele yenye miiba miiba na kuanza kumla sekundee hiyo hiyo, hivyo chakula kinakuwa bado kinaishi wakati kikiliwa.

Huwa wanakula hata vunjajungu wenzao. Wakati wa show, wa kiume anabidi apige mahesabu ya calculus anapompanda wa kike maana mara nyingi akiingia vibaya akakamatwa na wa kike, wa kike anakuwa anamla wa kiume akiwa anaendelea na tendo.

Inasemekana kichwa na kiwiliwili vinajitegemea, hivyo kichwa kinaweza kuwa kinaliwa huku kwa chini wa kiume aneandelea na majukumu ya ndoa. Mara chache huwa wa kiume anaweza kutoroka baada ya tendo la ndoa.
 
Inasemekana kichwa na kiwiliwili vinajitegemea, hivyo kichwa kinaweza kuwa kinaliwa huku kwa chini wa kiume aneandelea na majukumu ya ndoa. Mara chache huwa wa kiume anaweza kutoroka baada ya tendo la ndoa.[emoji23]
 
Nyegere ama Honey Badger

Huyu jamaa ni mkorofi sana na haogopi chochote. Anapambana mpaka na simba na anajulikana na wanyama wengine kama mnyama mkorofi mpaka wengi huwa wanaamua kuachana nae tu, ingawa ana kamwili kadogo.

Anapenda asali na huifuata hata sebuleni kwa nyuki, na wakimdunga hasikii chochote maana ana ngozi ngumu sana. Chakula chake kingine pendwa ni nyoka na nge. Sumu zao hazina madhara kwake, yeye akikutana nao ni kushambulia tu na kula.




Kitu cha ajabu nilichojifunza ni kuwa duma wamevolve kuzaa watoto wanaofana na nyegere. Evolution iliwafundisha kuwa nyegere huwa hasumbuliwi na boya yeyote hivyo wakaevole ku mimic/camouflage kama nyegere.Duma ni dhaifu kulingana na wengine kama chui, simba, nk hivyo hawezi kutegemea ubabe wake, ikabidi atafute namna kwa evolution. Mama duma huwa analazimika kuwaacha watoto wake akienda kuwinda hivyo watoto wanakuwa hatarini zaidi mama akiwa mbali. Hivyo basi kwa kuwa watoto wa duma wana nywele nyeupe mgongoni, kwa mbali wanaoneka kama nyegere kwa maadui, nao maadui wakiwaona wanajisemea tu 'daah, nyegere wale, tuachane nao tu', hivyo vitoto vya duma vinapona.

 
Kwahiyo hao watoto wa duma wanaishi kwa gharama za Nyegere au sio, yn kwa kiswahili tunawaita chawa wa Nyegere.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…