Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kobe jitu, unaambiwa kobe na mamba ndio wanyama wakongwe zaidi duniani. Walikwepo tokea enzi za dinosaursJonathan ndiye mnyama mzee zaidi duniani anayejulikana. Alizaliwa mnamo 1832 na kwa sasa ana umri wa miaka 187. Ameishi WW1 na WW2, Mapinduzi ya Urusi, wafalme saba kwenye kiti cha enzi cha Uingereza, na marais 39 wa Amerika... [emoji7]View attachment 2361213
Kuna ndege wanaitwa cuckoo sifa yao kubwa ni kuvamia viota vya ndege wengine, pengine hii sifa na wewe ndiyo unaijua. Wasumbufu, wakorofi n wana ubabe hivi.
Tabia nyingine ya cuckoo ni kutopenda kulea mayai yao na vifaranga vyao. Now logic itakufanya ujiulize kama hawalei ni nani wanalea? Jibu ni simple, ndege wengine hua wanalea mayai ya cuckoo.
You see cuckoos hutafuta kiota ambacho tayari kina mayai kisha cuckoo jike huenda kutaga hapo na kuyeya. Ndege mwenye kiota ataatamia mayai, atalisha vifaranga kisha siku ikifika atashangaa kuna kibaba kipo hapo hakielewi na amekilisha tangu kichanga, by that time katakua kanaweza kupaa so katajiondokea.
Now siyo kila ndege ni wajinga au siyo? Wengine wataangalia na kugundua hichi siyo kifaranga changu so ataanza kukatenga kwa kutokapa chakula ambapo cuckoos huteua genge la ndege kadhaa ambao humtembelea yule mama ndege aliyegoma kulisha kifaranga cha cuckoo na kumshushia kipigo.
Mostly baada ya hapo huyu kifaranga hulishwa vyema kabisa mpaka anakua na kuondoka zake.
Pembe,meno hukaa kinywaniYale unayoyaona kwa tembo siyo pembe bali ni meno yaliyotokeza nje. Kama binadamu anavyoweza kutumia zaidi mkono wa kushoto au kulia, tembo kuna jino anapenda kutumia zaidi.