#COVID19 Madagascar yakubali kupata chanjo ya Covid-19

#COVID19 Madagascar yakubali kupata chanjo ya Covid-19

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

Madagasca

Madagascar imeamua kubadili mtazamo wake juu ya kukabiliana na virusi vya corona na kujumuika na jitihada za kimataifa kupata chanjo ya corona.

"Kuna hatua kadhaa ambazo inabidi kupitia kabla ya kupata chanjo hiyo lakini kujisajili ndio jambo la msingi na hatua muhimu kabla ya kupata chanjo hiyo, lakini tayari tuko kwenye hatua muhimu katika usajili," Waziri wa Afya Prof Jean Louis Rakotovao alisema kwenye video aliyoiweka kwenye ukurasa wa wizara yake wa Facebook.

Awali Madagascar ilionesha kutokuwa na nia ya kushiriki katika jitihada za kupokea chanjo. Ilidai kuwa ni bora kutumia dawa ya asili inayofahamika kama Covid-Organics.

Dawa hiyo ambayo iko katika mfumo wa chai au vidonge iliitangazwa na Rais wa taifa hilo bwana Andry Rajoelina kuwa ndio dawa ya corona.

Hata hivyo hakuna tiba ya virusi vya corona, Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani.
 
Watanzania tuthamini vya kwetu
 
BADO NAAMINI COVID 19 NI UGONJWA WA KUTENGENEZA KWA MASLAHI YA MABEBERU NA WAUZA CHANJO

PIA VILEVILE NI BIO-WEAPON
So long as Unaamini na unapisha imani yako kama imani na sio kujua / Kufahamu (ni Haki Yako)

So long as Unaamini kwa kuchukua tahadhari zilizopo kutoka kwa wataalamu wanavyokwambia na sio Imani zako (pia its all good)

In short chochote ambacho hakina madhara kwa jamii inayokuzunguka sio mbaya (ila kama hizo imani zako ukitaka wanaokuzunguka pia waziamini kwa kuwashinikiza)..., well... utakuwa umekosa hekima na ustaarabu...
 
So long as Unaamini na unapisha imani yako kama imani na sio kujua / Kufahamu (ni Haki Yako)....
Bado mimi binafsi (nafsi ya kwanza umoja-mimi) haimaanishi mawazo yangu yanashinikiza wengine wasichukue tahadhari au kujikinga

Nimeona niweke hili sawa
 
BADO MIMI BINAFSI (NAFSI YA KWANZA UMOJA-MIMI) HAIMAANISHI MAWAZO YANGU YANASHINIKIZA WENGINE WASICHUKUE TAHADHARI AU KUJIKINGA

Nimeona niweke hili sawa
Mkuu don't shout nakusikia mkuu

Kwahio hio Bio Weapon walitengeneza ili wajipige wenyewe ? Ukizingatia Afrika hawajawa affected kama European and American Countries kwahio kwa kufuata logic huenda hio weapon tumetengeneza sisi Africans au watu wa Antarctica ?
 
Mkuu don't shout nakusikia mkuu ?

Kwahio hio Bio Weapon walitengeneza ili wajipige wenyewe ? Ukizingatia Afrika hawajawa affected kama European and American Countries kwahio kwa kufuata logic huenda hio weapon tumetengeneza sisi Africans au watu wa Antarctica ?
Bio weapons pia zingie hufeli why not? Vita vya kiuchumi sio mchezo and sishangai kila kukicha kunaibuka "strains" / Aina mpya za COVID 19
 
Bio weapons pia zingie hufeli why not? Vita vya kiuchumi sio mchezo and sishangai kila kukicha kunaibuka "strains" / Aina mpya za COVID 19
Basi hao (wasiojulikana ambao wewe huenda unawajua) they are not all that bright, kwa mbinu zote ambazo wangeweza kutumia wanatumia mbinu hii risky ambayo kuwezekana kwake ni majaliwa na toss of a coin?

Pili tukifuata mtiririko huo basi ni Pfizer ndio walitengeneza sababu mpaka sasa ndio wana chanjo ambayo ni more effective...,

Tatu, utengeneze virus ambayo ni gharama/ risky ili upate pesa ukijua kabisa hata ukitengeneza chanjo kuna wengine wengi ambao watacopy unachofanya na wenyewe kunufaika na kazi yako ngumu na hatari, huoni hapo kichwani zitakuwa hazikutoshi ?

Nne, kwahio hapa tuseme ni corporations ndio zilifanya hii conspiracy (sababu ni corporations which are big pharmaceuticals) ukisema nchi je unadhani gharama ya uchumi kwa nchi kwa miaka hii ni ndogo kusema kwamba hii chanjo itakuwa imerudisha pesa pamoja na madhara yaliyotokea?

In short hata kama hii Virus ilitokea maabara (which is possible) lakini it was un-intended. Mistakes do happen uzembe wa mtu katika experimentation (kwa motive ya to do good) inaweza ikasababisha unintended results. Binadamu are not that clever kuweza kucheza hii multi dimensional chess with so many unknowns (na yoyote anayejaribu lacks common sense)
 
BADO NAAMINI COVID 19 NI UGONJWA WA KUTENGENEZA KWA MASLAHI YA MABEBERU NA WAUZA CHANJO

PIA VILEVILE NI BIO-WEAPON
HATA MIMI NAAMINI NI WA KUTENGENEZA...ILA UMESHAINGIA SOKONI LAZIMA TUPATE CHANJO TU....WAPIGE HELA ZAO..
 
Ni suala la muda tu kwa hayo yanayotokea kwa serikali ya Antananarivo kutokea pia kwa serikali ya Dodoma...
 
BADO NAAMINI COVID 19 NI UGONJWA WA KUTENGENEZA KWA MASLAHI YA MABEBERU NA WAUZA CHANJO

PIA VILEVILE NI BIO-WEAPON
Mabeberu kivp? Mbona China wana zao.. India wana zao.

Then unaposema maslahi ni yapi? Mbona US yenyewe uchumi umeporomoka na makampuni kufungwa sababu ya Covid? Au hujui hta chanjo ipo ya bure kabisa sasa wanafaidika nini hao mabeberu ilihali hta pesa za chanjo wanatoa wao??

Kuna mahali wamekataza nchi kutengeneza chanjo zao? Nadhani inferiority complex inatutesa waafrika.
 
Yaani nilikuwa nakuheshimu ila kwa hili napata ukakasi,yaani unaamini maneno ya upuuzi wa Jiwe na Genge lake?aibu naona Mimi.
Mkuu hta mimi nimemshangaa sana... Member mkongwe hivi mwenye credibility kubwa naye anaingia mkenge wa wanasiasa?

Eti Bio weapon.... Yaani wasituue kupitia ARV wanazotupa bure waje kutuua wazi wazi hivi? Kazi kweli kweli
 
Mkuu hta mimi nimemshangaa sana... Member mkongwe hivi mwenye credibility kubwa naye anaingia mkenge wa wanasiasa?

Eti Bio weapon.... Yaani wasituue kupitia ARV wanazotupa bure waje kutuua wazi wazi hivi? Kazi kweli kweli
Jiwe na wakina Kabudi walaaniwe
 
Rais wa Madagascar Ande Rajoelina aliyeutangazia ulimwengu kuwa amegundua dawa ya Corona , amenyoosha mikono na kukubali kuagiza , kupokea na kutumia kinga ya Corona nchini mwake . Mytake muda Ni mwalimu mzuri sana.
 
Back
Top Bottom