Madai ya Katiba Mpya: Viandaliwe vipeperushi kuhusu umuhimu wa Katiba Mpya na visambazwe mitaani na sehemu zenye mikusanyiko

Madai ya Katiba Mpya: Viandaliwe vipeperushi kuhusu umuhimu wa Katiba Mpya na visambazwe mitaani na sehemu zenye mikusanyiko

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Mbali na kutumia mitandao na makongamano au mikutano kudai Katiba Mpya, nashauri wanaharakati, wanasiasa na wadau wengine waandae vipeperushi vyenye kueleza umuhimu wa katiba mpya na kuvisambaza kadri inavyowezekana.

Vipeperushi vieleze mapungufu yaliyoko katika katiba ya sasa na hatari au athari zake kwa makundi mbalimbali katika jamii mfano wafugaji, wakulima,wafanyakazi n.k bila kusahau madhara yake kwa nchi nzima.

Vipeperushi vieleze mifano ya madhara tuliyopata kutokana na hii Katiba kama vile chaguzi za hovyo kama ule wa mwaka jana, madaraka makubwa ya Raisi kama kuvunjia watu nyumba Kimara lucha ya kuwa na zui la mahakama, n.k.

Mfano mwingine uwe ni watumishi wa umma kukaa miaka sita bila ya nyongeza ya mishahara ya kisheria ya kila mwaka enzi za Magufuli, n.k.

Vipeperushi yaliyotokea kwenye zao la korosho kulikotona na maagizo ya mtu mmoja mwenye madaraka makubwa, n.k.

Vipeperushi vigusie mauji,wizi,ufisadi na jinsi katiba hii inayowezesha watawala kuwalinda wahalifu wa vitendo hivi, n.k.

Kwa kifupi, yako mengi ya kuelezwa sambamba na kutaja faida tutazozipata kutokana na Katiba Mpya iwapo itapatikana

Vipeperushi visambazwe sokoni, misikitini, mashuleni, vyuoni, kwenye mabasi na daladala na sehemu nyingine zenye mikusanyiko.

Kwa kifupi, zitumike mbinu, njia na resource zote zilizopo katika mapambano haya ya kudai Katiba Mpya bila kuchoka.

Hakuna mjomba wala shangazi kutoka nje ataekuja kutusaidia katika mapambano haya, bali ni sisi watanzania wenyewe kwa umoja wetu.

Pamoja tutashinda.Itachukua muda gani, hiyo si hoja.

Penye nia, pana njia.

NB:Kudai Katiba Mpya, kusambaza vipeperushi vya aina hiyo, si kosa, bali ni kutekeleza na kuutumia uhuru wa Katiba hii tuliyonayo kivitendo zaidi.
 
E5tTtHJWEAAuzmp.jpeg
kama haya pia ni mazuri sana ili watu wajue umuhimu wake
 
Mbali na kutumia mitandao na makongamano au mikutano kudai Katiba Mpya, nashauri wanaharakati, wanasiasa na wadau wengine waandae vipeperushi vyenye kueleza umuhimu wa katiba mpya na kuvisambaza kadri inavyowezekana...
Naikiwezekana juhudi zielekezwe zaidi maeneo ya pembezoni ambako,uelewa ,pamoja na upatikanaji wa taarifa sahihi na kwa wakati ni hafifu.
 
Hakika,

Haya kumekucha!! Hima hima vijana mliomaliza vyuo vikuu nchini mliopo majumbani na vyuoni jitokezeni kudai katiba yenu mpya kwa ustawi wa Taifa lenu nafasi pekee ndiyo hii.

Tanzania inajengwa na nyie vijana.
 
Nani atagharamia hivyo vipeperushi ikiwa maji dumu moja mia tano?

Ukijitambua usiende kwenye mikutano ya waongo.
 
Si mlikuwa mnamtukana Magufuli?

Si mlisema mama anaupiga mwingi na sasa ufipa mnapumua?

Season ya nyumbu migration imeanza rasmi
 
Yaani kwa hili hata kama serikali itakosa hela
Watu tutajitolea tu ilimradi watu waupate ujumbe wa umuhimu wa katiba mpya!
Jirani zetuBurundi waliingia mfukoni kuwezesha kupatikana kwa Katiba yao mpya,iweje sii matajiri tena Donor country.
 
Si mlikuwa mnamtukana Magufuli?

Si mlisema mama anaupiga mwingi na sasa ufipa mnapumua?

Season ya nyumbu migration imeanza rasmi
Naona una hasira, machungu na frustrations.

Pole sana.
 
Kuna wimbi la tatu la kovidi tulieni jamani🤸🐒
 
Wanachama wa NSSF kuwekewa masharti Magumu kwa Kizingiti cha Fao la KUJITOA

KATIBA MPYAA HAIEPUKIKI
 
Jirani zetuBurundi waliingia mfukoni kuwezesha kupatikana kwa Katiba yao mpya,iweje sii matajiri tena Donor country.
Na Burundi "ya Katiba mpya" sasa ipo huru, matatizo yaliyosababishwa na "katiba mbaya" yamekwisha, ama sio? ☺️
 
Na Burundi "ya Katiba mpya" sasa ipo huru, matatizo yaliyosababishwa na "katiba mbaya" yamekwisha, ama sio? ☺️
Katibu jukwaani tufahamishane,changamoto,ubora na udhaifu wa Katiba yao mpya iliyochangiwa na raia ili kufanikisha malengo ya kitaifa kizalendo.
 
Nani atagharamia hivyo vipeperushi ikiwa maji dumu moja mia tano?

Ukijitambua usiende kwenye mikutano ya waongo.
Kwani nani huwa anagharamia zile kofia za kijani na fulana kila baada ya miaka 5?
 
Mbali na kutumia mitandao na makongamano au mikutano kudai Katiba Mpya, nashauri wanaharakati, wanasiasa na wadau wengine waandae vipeperushi vyenye kueleza umuhimu wa katiba mpya na kuvisambaza kadri inavyowezekana.

Vipeperushi vieleze mapungufu yaliyoko katika katiba ya sasa na hatari au athari zake kwa makundi mbalimbali katika jamii mfano wafugaji, wakulima,wafanyakazi n.k bila kusahau madhara yake kwa nchi nzima.

Vipeperushi vieleze mifano ya madhara tuliyopata kutokana na hii Katiba kama vile chaguzi za hovyo kama ule wa mwaka jana, madaraka makubwa ya Raisi kama kuvunjia watu nyumba Kimara lucha ya kuwa na zui la mahakama, n.k.

Mfano mwingine uwe ni watumishi wa umma kukaa miaka sita bila ya nyongeza ya mishahara ya kisheria ya kila mwaka enzi za Magufuli, n.k.

Vipeperushi yaliyotokea kwenye zao la korosho kulikotona na maagizo ya mtu mmoja mwenye madaraka makubwa, n.k.

Vipeperushi vigusie mauji,wizi,ufisadi na jinsi katiba hii inayowezesha watawala kuwalinda wahalifu wa vitendo hivi, n.k.

Kwa kifupi, yako mengi ya kuelezwa sambamba na kutaja faida tutazozipata kutokana na Katiba Mpya iwapo itapatikana

Vipeperushi visambazwe sokoni, misikitini, mashuleni, vyuoni, kwenye mabasi na daladala na sehemu nyingine zenye mikusanyiko.

Kwa kifupi, zitumike mbinu, njia na resource zote zilizopo katika mapambano haya ya kudai Katiba Mpya bila kuchoka.

Hakuna mjomba wala shangazi kutoka nje ataekuja kutusaidia katika mapambano haya, bali ni sisi watanzania wenyewe kwa umoja wetu.

Pamoja tutashinda.Itachukua muda gani, hiyo si hoja.

Penye nia, pana njia.

NB:Kudai Katiba Mpya, kusambaza vipeperushi vya aina hiyo, si kosa, bali ni kutekeleza na kuutumia uhuru wa Katiba hii tuliyonayo kivitendo zaidi.
Kwani katiba mpya yenyewe inasemaje?
 
Back
Top Bottom